• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
KARAGWE DISTRICT COUNCIL
KARAGWE DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KARAGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na dira
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
        • Sekondari
        • Msingi
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Mazingira na Taka ngumu
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Ufugaji na Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Inayokuja
    • Iliyotekelezwa
    • Inayoendelea
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Taarifa
    • Sheria
    • Mpango mkakati
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha

Usafi na Mazingira


IDARA YA MAZINGIRA NA UDHIBITI TAKA NGUMU (ENVIRONMENT AND SOLID WASTE MANANGEMENT)

1.0: UTANGULIZI

Idara ya Mazingira na takangumu ni Idara mpya iliyoundwa mwaka 2013 kwa lengo la kuimarisha usafi wa mazingira na Hifadhi/utunzaji wa mazingira kuanzia ngazi ya Kaya,Kitongoji, Kata, Tarafa, Wilaya, Mkoa  hadi Taifa. Kutokana na asili ya kazi za idara hii na mwongozo wa serikali, wataalam wa Idara hii wanapaswa kuwa na taalum ya Afya-mazingira  kwa ajili ya kusimamia shughuli za usafi wa mazingira na wengine kuwa na taaluma ya  Mazingira na Misitu  kwa ajili ya kusimamia shughuli za hifadhi na utunzaji wa mazingira.

Hii ni kulingana pia, na matakwa ya kitaaluma na maelekezo ya sheria ya usimamizi wa  mazingira Na. 20, ya 2004 na mpango kazi wa taifa wa hifadhi na usimamizi wa mazingira, 2013 – 18, likiwemo suala la udhibiti wa uchafuzi wa mazingira, yaani, ardhi, hewa, kelele na uthibiti taka, pamoja na shughuli za kutathmini athari za mazingira. Uhundaji wa idara hii pia, utarahisisha uendeshaji, utendaji, utaratibu, mawasiliano na ushiriki wa wadau mbali mbali, wakiwemo wananchi, ambao ndiowalegwa wa huduma hizi za mazingira.

Wataalamu wa idara hii ni; wanasayansi  wa mazingira (enviroment  scientists) wahandishi mazingira ( environment engineers, sanitation  engineers, public health engineers) na maafisa afya (environmental health scientists).

2.0:MAJUKUMU YA IDARA

2.1: HIFADHI YA MAZINGIRA

2.1.1 Utunzaji/Uhifadhi wa Mazingira na Bioanuai (Environmental Conservation and Biodiversity)

  • Kutenga maeneo ya Upandaji miti, Majani,Maua, ukatiaji miti na Upendezeshaji Mazingira (Planting of trees, plants, grass, flowers, prunning of trees and beautification) na kusimamia kampeni ya Taifa ya upandaji miti.
  • Kuhamasisha jamii kushiriki na kuratibu upandaji miti,  Majani,Maua, ukatiaji miti na Upendezeshaji Mazingira (Planting of trees, plants, grass, flowers, prunning of trees and beautification) pamoja na utekelezaji wa mashindano ya Tuzo ya Rais ya kuhifadhi vyanzo vya maji, kupanda na kutunza miti katika Halmashauri husika.
  • Kuhamasisha jamii kupanda miti, majani na maua , kukatia majani na miti na kupendezesha Miji na maeneo mbalimbali.
  • Kuandaa na kufuatilia utekelezaji wa mipango ya Halmashauri ya usimamizi wa Mazingira kwa kuzingatia mpango kazi wa Taifa wa Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira.
  • Kuandaa na kusimamia  utekelezaji wa sheria ndogo na miongozo na ya  kulinda mazingira ikiwa ni pamoja na bioanuai, ardhi, mazingira ya mito, bahari na mabwawa
  • Kuweka  mfumo wa kukusanya taarifa za mazingira utakao husisha ngazi ya halmashauri hadi kitongoji/ mtaa.
  • Kubaini maeneo ya hatari yanayohitaji usimamizi maalumu na kumshauriwaziri mwenye dhamana ya usimamizi wa mazingira kuhusu njia bora zinazoweza kutumika.
  • Kuandaa taarifa ya hali ya mazingira ya maeneo yao zitakazo jumlishwa katika ripoti ya taifa ya hali ya mazingira,
  • Kupendekeza maeneo yanayoweza kutangazwa kuwa maeneo ya hifadhi ya taifa ya mazingira na kufuatilia utekelezaji wa mipango ya usimamizi wa mazingira ya hifadhi,
  • Kusimamia utekelezaji wa vyanzo vya maji kwa kudhibiti utekelezaji wa shughuli yoyote inayoweza kuletaa athari katika maeneo mito, maziwa, bahari na mabwawa,
  • Kusimamia  na kutekeleza sera ya taifa ya mazingira, sheria ya usimamizi wa mazingira kuhusu maswala ya hifadhi ya bioanuai yaliyobainishwa katika sera, sheria, kanuni,miongozo,mikakati, mipango na program za kisekta, na
  • Kutekeleza mikakati, mipango na program ya mikataba ya kitaifa  na kanda inayohusiana na hifadhi ya bioanuai,
  • Kuandaa anakutekeleza program za kutoa elimu kuhusu hifadhi endelevu ya bioanuani katika maeneo ya Halmashauri,
  • Kubaini bioanuai zilizopo katika halmashauri yetu na hali ya iliyoharibifu na uhifadhi wake,
  • Kuweka na kusimamia mikakati ya kuongoa ardhi iliyoharibiwa na kuzuia uharibifu wa bioanuai,
  • Kusimamia utekelezaji wa mipango ya matumizi bora ya ardhi ya halmashauri ,
  • Kuandaa na kutekeleza mikakati, mipango na program za halmashauri kwa kuzingatia mkakati wa kitaifa wa kihifadhi bioanuai
  • Kuadaa na kutekeleza mikakati, mipango na program za halmashauri kwa kuzingatia mkakati wa matumizi salama ya teknolojia ya kisasa (biosafety)
  • Kutekeleza mfumo wa upashanaji habari juu ya bioanuai na matumizi salama ya bioteknolojia ya kisasa,
  • Kuhamasisha matumizi ya teknolojia ya nishati mbadala pamoja na majiko banifu.
  • Kuandaa na kutekeleza miradi mbalimbali kuhusu usimamizi wa hifadhi ya mazingira.
  • Kutoa mapendekezo na kufuatilia hatua za kukabiliana na uharibifu wa maeneo yaliyoathirika kutokana na shughuli za uchumi zisizo endelevu (kama uchimbaji madini, kilimo, ujenzi, ufugaji nk) NA
  • Kusimamia na kutekeleza kazi nyingine zitakazoelekezwa na mamlaka za juu.

2.1.2 Udhibiti Uchafuzi wa Mazingira (ardhi, maji, hewa na sauti) (pollution contro: land, water,air and sound)

  • Kuandaa na kutekeleza programu za kutoa elimu ya mazingira kwa jamii kuhusu njia bora za kudhibiti uchafuzi wa mazingira na athari zake,
  • Kuweka na kusimamia amri za kudhibiti/ kuzuia  kelele,  mitetemo na uchafuzi wa hewa unaosababishwa na moshi, gesitaka au gesi za sumu, kutoka vyanzo mbalimbali kama vile makazi, viwanda, uchimbaji wa madini na vyombo vya usafiri,
  • Kuweka miongozo ya kupunguza athari za uchafuzi wa hewa ya ndani ya makazi (in-door pollution) inayosababishwa na shughuli mbalimbali kama vile matumizi ya nishati ya kuni, vinyesi vya mifugo na uchomaji wa madini ya zebaki,
  • Kuandaa na kusimamia miongozo ya kutenganisha maeneo ya makazi ya watu, ofisi na taasisi za elimu na shughuli za kiuchumi kama vile ujenzi wa viwanda, madampo ilikudhibiti athari kwa afya na mazingira,
  • Kuandaa miongozo ya ujenzi wa miundombinu ya taka katika maeneo ya biashara, viwanda na shughulinyingine za kiuchumi naya usimamizi wake ilikuhakikisha hali ya usafi na kudhibiti viumbe waharibifu na uzagaaji wa taka ,
  • Kuweka na kusimamia miongozo ya usimamizi wa majitaka katika miundombinu ya hifadhi, kusafirisha na kutibu majitaka kwa kushirikiana na mamlaka  husika,
  • Kufuatilia uzingatiaji wa viwango vilivyowekwa vya majitaka yanayomwagwa kwenye mazingira ili kukidhi viwango vya mazingira,
  • Kusimamia uzingatiaji na utekelezaji wa viwango vya mazingira vya taifa na kuweka vigezo vya kupima uharibifu wa mazingira.
  • Kufuatilia na kuthamini athari za uchafuzi wa mazingira katika makazi, viwanda, migodi, biashara,kilimo na ufugaji.
  • Kusimamia na kutekeleza sera ya taifa mazingira, sheria ya usimamizi wa mazingira kuhusu masuala ya tathmini ya athari kwa mazingira na tathmini ya kimkakati yaliyobainishwa katika sera, sheria, kanuni, miongozo, mikakati, mipango na program za kisekta , na
  • Kufuatilia na kuthamini athari za uchafuzi wa mazingira katika makazi, viwanda, migodi,ujenzi, biashara, kilimo na ufugaji.

2.1.3 Tathmini ya Athari kwa Mazingira-TAM (Environmental Impact Assessment-EIA)

  •  Kuandaa tathmini ya kimkakati kwa mazingira kwa mipango na program za halmashauri zinazotakiwa kufanyiwa tathmini hiyo kama zilivyobainishwa katika sheria ya usimamizi wa mazingira na kanuni zake,
  • Kufuatilia utekelezaji wa utaratibu wa tamthini ya kimkakati ya mazingira katika maeneo yao na kutoa ushauri kwa Mkurugenzi wa mazingira ofisi ya kaimu wa Rais 
  • Kufuatilia utekelezaji wa utaratibu wa Tathmini ya Adhari  kwa mazingira (TAM) katika maeneo yao kwa shughuli zinazotakiwa kufanyiwa TAM kama zilivyobainishwa katika sheria ya usimamizi wa mazingira na kanuni zake,
  • Kufuatilia utekelezaji wa mipango na masharti ya TAM kwa kila shughuli/ mradi uliofanyiwa tathmini hiyo au kukaguliwa na kutoa ushauri kwa Mkurungenzi Mkuu wa baraza la hifadhi na usimamizi wa mazingira,
  •  Kushirikisha umma katika maamuzi yanayoweza kuathiri mazingira katika uandaaji wa sera, mikakati, mipango program na sheria zinazohusu mazingira katika maeneo yao,
  • Kufanya utafiti/ uchunguzi wa uharibifu  au athari kwa mazingira unaosababishwa na shughuli za kiuchumi na kijamii katika maeneo yao na kutoa taarifa kwa Mkurugenzi mkuu wa baraza la hifadhi na usimamizi wa mazingira ,
  • Kufuatilia na kutoa ushauri kuhusu maeneo yaliyoathirika kutokana na shughuli  za uchumi zisizoendelevu kama vile uchimbaji madini holela,uvuvi haramu, kilimo kisichokuwa endelevu,ujenzi holela , ufugaji wa kuhamahama  usio zingatia uwezo wa malisho n k.
  • Kusimamia/ kuratibu utekelezaji wa kazi na kamati za mazingira na kamati za kudumu za halmashauri zisizoanzishwa na sheria ya usimamizi mazingira ngazi ya Halmashauri hadi kitongoji/ mtaa
  • Kuandaa na kutekeleza mikakati, mipango na program za Halmashauri kwa kuzingatia mkakati wa kitaifa wa kuhimili na kukabiliana na mabadiliko ya tabia ya nchi.
  • Kuandaa na kutekeleza mikakati, mipango na program za halmashauri kwa kuzingatia program ya kitaifa ya kukabiliana na kuenea kwa hali ya jangwa na ukame,
  • Kuandaa nyezo na kutoa elimu ya mazingira kwa jamii kuhusu sheria ya usimamizi wa mazingira  na kanuni zake, mikakati ya kuhimili na kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi, mikakati ya kukabiliana na kuenea kwa hali ya jagwa na ukame.
  • Kutekeleza mikakati, mipango na program ya mikataba ya kimataifa na kanda ya mazingira inayohusiana na kemikali, taka za sumu na udhibiti wa uchafuzi.
  • Kusimamia na kutekeleza sera ya taifa ya mazingira, sheria ya usimamizi wa mazingira kuhusu masuala ya udhibiti wa uchafuzi wa mazingira na yaliyobainishwa katika sera, sheria, kanuni, miongozo, mikakati mipango na program za kisekta; na.
  • Kusimamia na kutekeleza kazi nyingine zitakazoelezwa na mamlaka ya juu.
  • UDHIBITI  WA TAKA NGUMU
  • Usafishaji na ukusanyaji taka ngumu kutoka kwenye majengo, maeneo ya wazi, barabara na mifereji ya kuondoa maji ya mvua (Clearing Of Buildings, Open Spaces, Roads And Drainages)
  • Kuweka mfumo wa miundombinu isiyoathiri afya na mazingira ya usimamizi wa taka kuanzia zinapozalishwa hadi zinapotupwa kwa kuzingatia utenganishaji, ukusanyaji na uhifadhi, urejezaji, utekelezaji katika matanuru maalumu na utupaji katika madampo ya kisasa,
  • Kubuni mbinu za kupunguza taka na kusimamia utekelezaji wake ili kupunguza uchafuzi wa mazingira .
  • Kufanya tafiti/ uchunguzi ili kubaini aina ya taka zinazozalishwa kutoka katika masoko, makazi maeneo ya biashara na taasisi kubuni njia bora za kupunguza, kutenganisha, kuhifadhi na kutupa taka.
  • Kusimamia usafi katika mifereji ya kukusanya maji ya mvua na kuhakikisha inafanya kazi muda wote.
  • Uhifadhi wa muda, Uchambuzi na usafirishaji taka ngumu (Sold waste storage, sorting, transportation)
  • Kuweka na kusimamia miongozo ya usimamizi wa taka ngumu katika miundombinu ya kuhifadhi, kusafirisha na kutekeleza na kutupa taka ngumu kwa kushirikiana na mamlaka husika.
  • Kuandaa na kusimamia miongozo ya kutenga maeneo kwa ajili ya kukusanya taka kwa muda ili kuhakikisha kuwa yana ukubwa wa kutosha na kudhibiti athari kwa jamii, afya na mazingira.
  • Kutenga maeneo maalumu ya kuanzisha vituo vya kukusanya, kuchakata na kuhifadhi taka zitokazazo na vifaa vya umeme na elekroniki, mafuta machafu na taka nyingine za sumu
  • Kutoa amri inayowataka wenye viwanda na maeneo ya biashara kutenga maeneo  ya kutisha, kuweka vifaa vya kutenganisha na kuhifadhi taka, mitambo ya kurejeleza na kurudufu taka ngumu ; na.
  • Kuweka vyombo vya kuhifadhi taka katika maeneo yote ya umma na kuhakikisha usafi wa maeneo hayo;

2.2.3. Uchambuaji Utupaji taka ngumu na Uendeshaji dampo la kisasa (Sorting And Sanitary Disposal Of Solid Waste And Dumpsite Management)

  • Kuainisha na kutenga maeneo maalum na ya  kutosha kwa ajili ya ujenzi wa dampo za kisasa
  • Kuweka nakusimamia miongozo ya utupaji wa mwisho wa taka ngumu na uendeshaji wa dampo za kisasa,
  • Kuweka tozo ya usimamizi wa taka inayozingatia gharama halisi ya huduma katika ukusanyaji hadi utupaji  katika madampo ya kisasa;na
  • Kutoa amri ya kuzuia  utupaji ovyo wa taka wa aina zote katika fukwe, maeneo ya wazi, mito na mifereji ya maji ya mvua

 



Matangazo

  • MATOKEO DARASA LA SABA 2022 December 01, 2022
  • WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA SEKONDARI 2023 December 14, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI July 09, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI February 21, 2022
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • ZAWADI

    September 26, 2022
  • WAJERUMANI WASAINI KITABU KWA DED

    September 26, 2022
  • KARAGWE YAPOKEA WAJERUMANI

    September 25, 2022
  • KAMATI YA FEDHA MAFUNZONI

    September 16, 2022
  • Angalia zote

Video

BARAZA LA MADIWANI LAWASIMAMISHA WATUMISHI
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • History
  • Dira na Dhamira
  • Fomu za mbalimbali
  • NEEMA INAKUJA KWA WAKULIMA
  • FEDHA ZILIZOPOKELEWA KWA AJILI YA MFUKO WA JIMBO

Viunganishi vihusishi

  • NECTA
  • UTUMISHI
  • TOVUTI YA TAIFA
  • TAMISEMI
  • FFARS
  • SALARY SLIP

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    KARAGWE KAGERA TANZANIA

    Anuani ya posta: BOX 20 KARAGWE

    Simu: 028-2227148

    Simu ya mkononi: 0754653409

    Barua pepe: ded@karagwedc.go.tz ded.karagwedc@kagera.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright©2017 karagwedc. All rights reserved.