• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
KARAGWE DISTRICT COUNCIL
KARAGWE DISTRICT COUNCIL

United Republic of Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KARAGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na dira
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
        • Sekondari
        • Msingi
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Mazingira na Taka ngumu
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Ufugaji na Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Inayokuja
    • Iliyotekelezwa
    • Inayoendelea
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Taarifa
    • Sheria
    • Mpango mkakati
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha

DC LAIZER ATAKA UTAMADUNI WA WANAFUNZI KUPANDA MITI WANAPOANZA SHULE KUENDELEZWA.

Imewekwa: February 1st, 2026

DC LAIZER ATAKA UTAMADUNI WA WANAFUNZI KUPANDA MITI WANAPOANZA SHULE KUENDELEZWA.

Mkuu wa Wilaya ya Karagwe Mhe. Julius Kalanga Laizer amewataka Maafisa Elimu na Wakuu wa Shule kuhakikisha wanaendeleza utamaduni wa Wanafunzi kupanda miti wanapoanza shule na kuendelea kuusimamia kipindi chote watakachokuwa eneo hilo lengo likiwa ni kutunza na kuboresha Mazingira ya shule yao pamoja na kutengeneza historia zao binafsi  na shule hiyo.

Wito huo umetolewa mapema leo Januari 31, 2026 katika Shule ya Sekondari Omorushaka ambapo Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe ilihitimisha wiki ya upandaji miti ambayo ni sehemu ya Kumuunga mkono Kiongozi na Mdau wa Kulinda na Kutunza Mazingira Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye Januari 27 aliadhimisha Siku yake ya kuzaliwa kwa kauli mbiu isemayo “Uzalendo ni Kutunza Mazingira, Shiriki Kupanda Miti” pamoja na kuongoza zoezi la upandaji miti ya matunda katika eneo la Bungi Kilimo, Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar.

“Kupanda miti ni jambo moja na kuitunza miti hii ni jambo lingine hivyo nikuombe mwalimu mkuu uisimamie hii miti 500 tuliyopanda leo ikuwe na kustawi. Tumeamua kupanda miti kwenye shule hii kama sehemu ya kuenzi na kuheshimu juhudi za Dkt.Samia Suluhu Hassan za kuendelea kuboresha Sekta ya Elimu kwenye Wilaya yetu  ikiwemo kutujengea Shule mpya, Tunamtia moyo na kumpongeza kwa Kazi ambayo wote tunaiona Shule nzima hii ni mpya si jambo dogo, Tunamshukuru sana” Alisema Mhe.Laizer

Naye, Afisa Misitu wa Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe Bi.Dotto Massanja amesema kuwa Halmashauri hiyo inaunga mkono kauli ya Uzalendo ni pamoja na kupanda miti  na kutunza mazingira kwa kuhakikisha inaendelea kutoa elimu kwa Wananchi kujijengea tabia ya kupanda miti kwenye maeneo yao hasa ya matunda na kuacha kukata miti hovyo pia amesema kuwa wameamua kuchagua Shule hiyo ili kuijengea mazingira ya kuvutia na kutengeza vivuli ambavyo watoto watavitumia kujisomea.

Kwa upande wake, Mwanafunzi wa Kidato cha nne Shule ya Sekondari Omorushaka Bi. Neema Renatus  ameishukuru Serikali kwa kuichagua shule yao kwaajili ya zoezi hilo kwasababu kupindi cha kiangazi Wanafunzi walikosa maeneo yenye vivuli kwaajili ya kupumzika na kujisomea anaamini miti hiyo itamaliza changamoto hiyo pia itasaidia kwenye uzalishaji wa hewa ya oksijeni na kupunguza hewa ya ukaa pamoja na kupendezesha Mazingira ya shule yao.

Hata hivyo, Mhe.Laizer amewapongeza Wananchi wa Wilaya ya Karagwe kwa kushiriki zoezi la upandaji miti kwa wiki nzima kwenye maeneo tofauti tofauti hadi siku ya leo (Kilele) pia ametoa wito kwa Wananchi wa Wilaya ya Karagwe kuendelea kupanda miti majumbani kwao hasa ya matunda ili kuboresha lishe na afya ya familia, kuimarisha mazingira na kukabiliana na mabadiliko ya tabia ya nchi.

Matangazo

  • TANGAZO LA USAILI WA WAANDAAJI WA MAUDHUI MTANDAONI WILAYA YA KARAGWE February 02, 2026
  • TANGAZO LA KAZI YA MWENYEKITI WA BODI YA AJIRA January 20, 2026
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MAHOJIANO September 17, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI September 19, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • DC LAIZER ATAKA UTAMADUNI WA WANAFUNZI KUPANDA MITI WANAPOANZA SHULE KUENDELEZWA.

    February 01, 2026
  • MADIWANI 32 KARAGWE DC WAIANZA SAFARI YA UTUMISHI KWA WANANCHI (2025 - 2030) RASMI LEO.

    December 02, 2025
  • DC LAIZER AONGOZA KIKAO CHA TATHIMINI YA MKATABA WA LISHE KWA NGAZI YA KATA KWA ROBO YA KWANZA JULAI-SEPTEMBA

    November 14, 2025
  • DED MSANGA AKAGUA NA KUTEMBELEA MIRADI MBALIMBALI YA MAENDELEO

    September 29, 2025
  • Angalia zote

Video

ZIARA YA WALIMU KATIKA HIFADHI YA TAIFA NGORONGORO
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • History
  • Dira na Dhamira
  • Fomu za mbalimbali
  • NEEMA INAKUJA KWA WAKULIMA
  • FEDHA ZILIZOPOKELEWA KWA AJILI YA MFUKO WA JIMBO

Viunganishi vihusishi

  • NECTA
  • UTUMISHI
  • TOVUTI YA TAIFA
  • TAMISEMI
  • FFARS
  • SALARY SLIP

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    KARAGWE KAGERA TANZANIA

    Anuani ya posta: BOX 20 KARAGWE

    Simu: 028-2227148

    Simu ya mkononi: 028-2227148

    Barua pepe: ded@karagwedc.go.tz ded.karagwedc@kagera.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright©2017 karagwedc. All rights reserved.