• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
KARAGWE DISTRICT COUNCIL
KARAGWE DISTRICT COUNCIL

United Republic of Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KARAGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na dira
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
        • Sekondari
        • Msingi
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Mazingira na Taka ngumu
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Ufugaji na Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Inayokuja
    • Iliyotekelezwa
    • Inayoendelea
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Taarifa
    • Sheria
    • Mpango mkakati
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha

Idara ya Elimu Sekondari

SECONDARY EDUCATION
The district has a total of 36 Secondary Schools with a total of 18583 students (7138 Boys and 9445 Girls).

The issue of rehabilitation and construction of classrooms and teacher houses have been an importantfocus.  The strategy for construction of classrooms and teachers’ houses has changed from a true paidconstruction to cost sharing arrangement with community contribution taken to the maximum.   This hasproved to be an effective and cost efficient strategy to increase the number of classrooms, teachers’ houses, and latrines.  It has also reinforced community ownership of schools and capabilities inaddressing problems. 

CLASSROOM  TEACHERS  RECRUITMENT AND DEPLOYMENT

For the year 2024, the Secondary Education division has a total of 506 teachers in 28 Government schools. There is a shortage of 190 teachers (144 science teachers and 46 social studies teachers)




TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA KAZI ZA IDARA YA ELIMU YA SEKONDARI KWA MWAKA 2023/2024

 

1.0 UTANGULIZI

Wilaya ina jumla ya Shule za Sekondari 36 zenye jumla ya wanafunzi 18583 (Wavulana 7138 na Wasichana 9445 kama ilivyochanganuliwa kwenye jedwali lifuatalo.

IDADI YA SHULE ZA SEKONDARI NA WANAFUNZI

KWA MWAKA 2024

SHULE

IDADI YA SHULE

WAVULANA

WASICHANA

JUMLA

SHULE ZA SERIKALI
28
7,201
8,123
15,324
SHULE ZA BINAFSI
08
1,937
1,322
  2,259
JUMLA KUU
36
9,138
9,445
18,583

 

1.1       IDADI YA WALIMU

            Kwa mwaka 2024 divisheni ya Elimu sekondari ina jumla ya walimu 506 katika shule 28 za Serikali. Kuna upungufu wa walimu 190 (Walimu wa masomo ya Sayansi ni 144 na wa masomo ya jamii ni 46).

1.2       IDADI YA WATUMISHI MAKAO MAKUU

Wapo jumla ya 4

  • DSEO       - Afisa Elimu Sekondari Wilaya
  • DSAO       - Afisa Elimu Taalum Sekondari Wilaya
  • DSLO       -Afisa Elimu Vifaa na Takwimu Sekondari Wilaya
  • DSNEO    -Afisa Elimu Maalum Sekondari Wilaya
  • Hakuna Afisa Elimu ya Watu Wazima Sekondari


2.0       MIUNDOMBINU MUHIMU 

Ifuatayo ni hali halisi ya uwepo wa miundombinu katika shule za Sekondariza Serikali.

Na.

AINA YA MAJENGO

MAHITAJI

UPUNGUFU

%

1
Madarasa

408

34

8.3

2
Matundu ya vyoo wanafunzi

670

338

50

3
Matundu ya Vyoo walimu

63

25

39

4
Nyumba za walimu

506

400

79

5
Majengo ya Utawala

28

10

35

6
Maktaba

28

15

53

7
Bwalo

28

25

89

8
Hostel – Wav

28

20

71

9
Hostel-Was

28

20

71

10
Vyumba vya maabara

78

44

56

11
Majiko

28

20

71


2.1       MIUNDOMBINU INAYOENDELEA KUJENGWA HADI SASA

2.1.1   Ujenzi wa shule mpya ya Mkoa ya Wasichana Kagera River kwa jumla ya Tshs. 4,100,000,000/= toka SEQUIP.      

2.1.2 Ujenzi wa shule mpya ya Kata ya Bugene kwa jina Omurushaka Sekondari kwa jumla ya Tshs. 584,029,000/= toka SEQUIP.

2.1.3 Ujenzi na ukamilishaji wa madarasa na matundu ya vyoo kwa Tshs. 125,000,000/= toka SEQUIP kwa shule za Kituntu, Nono, Kayanga, Nyakahanga, Kiruruma na Chakaruru.

2.1.4   Pia idara imepokea jumla ya Tshs. 2,085,000,000/= Januari, 2024 za ujenzi wa vyumba vya madarasa 63, ukamilishaji ujenzi wa vyumba vya madarasa 18 na ujenzi wa matundu ya vyoo 88 katika shule za sekondari 18.


3.0       UWEPO WA VITABU SHULENI

            Vitabu shuleni vinanunuliwa kwa fedha ya Elimu (Capitation grand). Hadi Januari 2024 uwiano wa kitabu kwa mwanafunzi kwa masomo ya Sayansi ni 1:2 na masomo ya sayansi jamii ni 1:3.

4.0       CHANGAMOTO

4.1       Upungufu wa watumishi unaoathiri utendaji kazi. Kuna upungufu wa walimu 190 ikiwa walimu wa masomo ya Sayansi 146 na masomo ya Sayansi jamii ni 46. Aidha hakuna Afisa Elimu Watu Wazima.

4.2       Upungufu wa miundumbinu muhimu kama vile nyumba za walimu, hosteli, majengo ya utawala, maktaba na samani.

4.3       Ukosefu wa watumishi wa kuajiriwa upande wa kada za uhasibu, ukarani, uboharia, ulinzi, upishi na Mwandishi Mwendesha Ofisi (Secretary).

4.4       Jamii kutoona muhimu sana wa kuchangia chakula shuleni kwa watoto wao na hivyo kupelekea wanafunzi kusoma wakiwa na njaa. Hii husababisha utoro na kuporomoka kwa ufaulukatika mitihani mbalimbali ikiwemo ya Taifa.

4.5       Baadi ya shule kukosa viwanja vya michezo  kutokana na mazingira, pia ufinyu wa maeneo.



5.0       MIKAKATI YA KUBORESHA ELIMU KATIKA SHULE ZA SEKONDARI

            Kwanza ni jambo la kujivunia kuwa ufuulu unapanda kwa mwaka. Mwaka 2023 matokeo ufaulu ni 94.4% na kidato cha nne ni 95%. Lengo la Taifa ni ufaulu wa 85% Divisheni ya Elimu Sekondari inalenga kuboresha Elimu hasa kupandisha ufaulu kwa kutumia mikakati ifuatayo:-

5.1       Kuendelea kuelimisha jamii kuwa jukumu la kujenga au kukamilisha miundombinu shuleni ni la wananchi wote.

5.2       Kutoa elimu kwa jamii/wazazi/walezi kuchangia chakula shuleni cha watoto wao.

5.3       Kufanya ufuatiliaji shuleni wa mara kwa mara ili kuhakikisha walimu wanafundisha ipasavyo na kutatua matatizo yao kwa wakati.

5.4       Kuomba Serikali iajiri walimu pungufu na kuhamasisha jamii kuendelea kuajiri walimu na watumishi wengine wa muda.

5.5       Kufundisha kwa bidii na kukamilisha mada kikamilifu kwa muda.

5.6       Kufanya mitihani ya majaribio nay a ushindani ili kuwapima na kuamsha  ari ya wanafunzi katika usomaji na ujifunzaji.

5.7       Kuhimiza na kuhamasisha michezo shuleni.



Mwl. JOHNBOSCO PAUL
KNY; AFISA ELIMU SEKONDARI 

HALMASHAURI YA WILAYA YA KARAGWE



Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO YA ASILIMI 10 October 04, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI KADA YA DEREVA II NA WAANDISHI WAENDESHA OFISI II September 30, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI WASAIDIZI KUMBUKUMBU DARAJA LA II NA MTENDAJI WA KIJIJI WA III October 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI February 21, 2022
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MASHINDANO YA UMISETA NGAZI YA WILAYA YAFUNGULIWA RASMI KARAGWE DC

    June 04, 2025
  • DED MSANGA ASISITIZA NIDHAMU KWENYE MASHINDANO YA UMITASHUMTA NGAZI YA MKOA.

    May 25, 2025
  • TIMU YA MENEJIMENTI KARAGWE DC YAKAGUA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO WILAYANI HUMO.

    May 23, 2025
  • KARAGWE DC YAJIPANGA VYEMA KUUWAKILISHA MKOA WA KAGERA KWENYE MASHINDANO YA UMITASHUMTA NGAZI YA TAIFA.

    May 23, 2025
  • Angalia zote

Video

SHIRIKI UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 KARAGWE TUMEJIPANGA
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • History
  • Dira na Dhamira
  • Fomu za mbalimbali
  • NEEMA INAKUJA KWA WAKULIMA
  • FEDHA ZILIZOPOKELEWA KWA AJILI YA MFUKO WA JIMBO

Viunganishi vihusishi

  • NECTA
  • UTUMISHI
  • TOVUTI YA TAIFA
  • TAMISEMI
  • FFARS
  • SALARY SLIP

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    KARAGWE KAGERA TANZANIA

    Anuani ya posta: BOX 20 KARAGWE

    Simu: 028-2227148

    Simu ya mkononi: 028-2227148

    Barua pepe: ded@karagwedc.go.tz ded.karagwedc@kagera.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright©2017 karagwedc. All rights reserved.