KITENGO CHA TEHAMA NA UHUSIANO.
Majukumu ya Kitengo cha Teknolojia ya Habari, Mawasiliano na Uhusiano
TAARIFA YA UTENDAJI NA UWAJIBIKAJI WA KITENGO CHA TEHAMA KWA MWAKA WA FEDHA 2016/2017
UTANGULIZI:
Kitengo cha TEHAMA kina jumla ya watumishi wanne (04) ambao ni kama ifuatavyo:
Na.
|
Jina la Mtumishi
|
Wadhifa
|
01.
|
Beatus Joseph Nyarugenda
|
Mchambuzi wa Mifumo ya kompyuta na Mkuu wa Kitengo
|
02.
|
Frank Itogo Ruhinda
|
Afisa Habari
|
03.
|
Geofrey Archard Kazaula
|
Afisa Habari
|
04.
|
Innocent Emmanuel Mwalo
|
Afisa Habari
|
Katika kipindi cha mwaka wa fedha 2016/2017, Kitengo cha TEHAMA kilitekeleza shughuli zifuatazo: Kusimamia shughuli za kila siku za kitengo cha Tehama, kuhudhuria vikao na mikutano mbalimabili kwa kuwakilisha kitengo cha Tehama, kuendelea kusimamia na kuratibu mifumo mbalimbali ya TEHAMA ikiwa ni pamoja na kufanya maandalizi ya kufunga Mfumo wa Kuratibu shughuli za Hospitali na kuendelea na maboresho ya Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe.
2.0 Shughuli hizo zilitekelezwa kama ifuatavyo:
2.1 Utekelezaji wa shughuli za kila siku za kitengo cha Tehama
Kwa kipindi cha mwaka wa Fedha 2016/2017, tumeendelea kutekeleza shughuli mbalimbali za Kitengo
cha Tehama hususani kufanya marekebisho ya vifaa mbalimali
Vya kieelectronics kama vile Kompyuta, printers scanner
mashine Photocopy nk ikiwa ni pamoja na kutoa ushauri wa
kitaalamu juu ya matumizi ya vifaa hivyo,
Aidha tumeweza kufanya marekebisho madogomadogo ya vifaa mbalimbali katika idara na vitengo vyote, marekebisho hayo madogomadogo yamefanyika kwa takribani kompyuta 20, printer 3, na baada ya marekebisho hayo madomadogo tumebaini kompyuta nane, printer sita na photocopy mashine nne ambazo zinahitaji marekebisho makubwa
4 Vikao na Mikutano Mbalimbali
Kwa kipindi hiki tumehudhuria vikao vyote vilivyohusisha kitengo hivyo tuliweza kuhudhuria vikao vyote vya kisheria ikiwemo CMT, Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango, pia na kikao cha kazi cha maandalizi ya kufunga mfumo wa Kuendesha shughuli za Hospital katika Kituo cha Afya Kayanga
5.Kufunga mfumo wa Kuendesha Shughuli za Hospitali
Katika kuboresha ukusanyaji wa mapato ya ndani na katika kuboresha shughuli za utoaji wa Huduma ya Afya ikiwa ni pamoja na kutekeleza maagizo ya Serikali juu ya ufungaji wa mfumo wa kukusanya mapato ya Hospital vituo vya Afya na Zahanati, tiyari tumeanza kufanya maadalizi ya kufunga mfumo huo katika kituo cha Afya Kayanga ikwa ni pamoja na kufanya upembuzi yakinifu kwa kushilikiana na shilika la MDH na Wizaraya ya Afya ambao tiyari umekwishafanyika na sasa tupo kwenye hatua za mwisho za ufungaji wa mfumo huo ambapo tunategemea Kuwa Mfumo utakuwa umeanza Kufanya kazi ifikapo mwezi December 2017
6. Kukusanya na kuandika habari ambazo ziliweza kutolewa kwa vyombo mbalimbali vya Habari kama vile radio, mbao za matangazo na tovuti ya Halmashauri ya wilaya Karagwe.
Ninawasilisha.
Beatus Nyarugenda
MKUU WA KITENGO CHA TEHAMA
HALMASHAURI YA WILAYA
KARAGWE
KARAGWE KAGERA TANZANIA
Anuani ya posta: BOX 20 KARAGWE
Simu: 028-2227148
Simu ya mkononi: 0754653409
Barua pepe: ded@karagwedc.go.tz ded.karagwedc@kagera.go.tz
Copyright©2017 karagwedc. All rights reserved.