• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
KARAGWE DISTRICT COUNCIL
KARAGWE DISTRICT COUNCIL

United Republic of Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KARAGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na dira
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
        • Sekondari
        • Msingi
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Mazingira na Taka ngumu
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Ufugaji na Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Inayokuja
    • Iliyotekelezwa
    • Inayoendelea
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Taarifa
    • Sheria
    • Mpango mkakati
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha

Ukaguzi wa ndani

Kitengo cha Ukaguzi wa ndani kimeanzishwa chini ya kifungu 45 (1) cha sheria ya fedha ya mamlaka ya Serikali za mitaa Na 13 ya mwaka 1982.Kitengo hiki kinatekeleza majukumu yake kwa kushirikiana na Kamati ya Ukaguzi.


KITENGO CHA UKAGUZI WA NDANI

MUUNDO, MAJUKUMU, WAJIBU NA UTOAJI HUDUMA

UTANGULIZI:

  Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani katika Halmashauri kimeundwa kwa mujibu wa Sheria ya fedha za Serikali za Mitaa Na. 9 (1982) Kf. 45 (1), Memoranda ya Fedha ya Serikali za Mitaa (2009) Kf. 13(1-2) na 14(1-10), sheria ya Manunuzi ya Umma Na. 7 (2011) na marekebisho yake ya mwaka 2016 Kf. 48 (2). Sheria ya fedha za umma na.6 (2001) na marekebisho yake ya mwaka 2010, Mwongozo wa ukaguzi wa ndani wa serikali za mitaa wa mwaka 2019 na mwongozo wa kimataifa wa ukaguzi wa ndani wa mwaka 2017 na mwongozo wa mchakato wa ukaguzi wa ndani wa mwaka 2016.

 Kitengo kwa sasa kina jumla ya watumishi 2 ambao ni:-.

Ramadhani Omari Samizi -    Mkaguzi wa Ndani

Ferdinand Bishashara     -       Mkaguzi wa Ndani

     RASILIMALI ZA KITENGO

     Kitengo kina rasilimali za kufanyia kazi ambazo ni komputa 2, printer 1, viti 2, meza 3, makabati 2, shelf 2 na gari 1 aina ya Toyota landcruiser pickup station wagon.

     NYARAKA ZA OFISI

     Kitengo cha ukaguzi kina nyaraka mbalimbali za ofisi kama vile jalada la ukaguzi wa ndani kwa ajili ya taarifa za ukaguzi mbalimbali, Memoranda ya Fedha ya mwaka 2009, Memoranda ya uhasibu ya mwaka 2009, Jalada la vielelezo, mpango wa ukaguzi wa mwaka.

 SHUGHULI MUHIMU ZINAZOENDELEA

Katika kusimamia mpango kazi wa mwaka 2023/2024 shughuli muhimu zinazoendelea ni kuanza kazi za ukaguzi wa miradi ya maendeleo pamoja na kuwasilisha taarifa ya ukaguzi wa ndani robo ya pili.

  Kulingana na muundo wake, Kitengo kinawajibika moja kwa moja kwa Mkurugenzi Mtendaji katika kuwasilisha taarifa zake na kwa muundo uliopo sasa kitengo cha Ukaguzi wa Ndani kina hadhi ya Idara kamili.

  Sera ya kitengo ni kutoa huduma zake kwa wadau wake kwa ubora wa hali ya juu kwa kuzingatia miongozo, sheria, kanuni, maadili, uadilifu na kwa maarifa bila upendeleo bali kuweka mbele maslahi ya wadau wanaotegemea huduma zetu.

  MAJUKUMU YA KITENGO

Majukumu ya Kitengo makubwa ni mawili ambayo ni  kutoa ushauri wa ndani   

(Internal consulting) na kutathimini mifumo ya udhibiti wa ndani (assurance

and appraisal) juu ya raslimali fedha na nyinginezo katika Halmashauri. Lakini

kufikia majukumu hayo mawili kazi hizo hufanyika.

Kuandaa mpango kazi wa Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani wa mwaka kuandaa mipango ya Ukaguzi.

Kutoa ushauri juu ya uboreshaji na uimarishaji wa mifumo ya ndani.

Kutoa ushauri juu ya kubaini maeneo yenye vihatarishi vikubwa katika utendaji kazi wa kufikia malengo ya Idara, Kitengo au Halmashauri nzima.

Kutoa taarifa za matokeo ya ukaguzi kwenye menejimenti ili hatua za kuimarisha ufanisi zichukuliwe.

Kufanya ukaguzi maalum kuhusu tuhuma zinazotolewa au zilizopo.

Kuwezesha kamati ya Ukaguzi kufanya kazi zake kwa ufanisi.

Kufuatilia na kutoa ushauri juu ya menejimenti kuhakikisha hoja za Mkaguzi wa nje zinajibiwa kwa wakati.

Kuandaa maeneo yenye kuhitaji kukaguliwa kwa kuzingatia umuhimu na athari zake kwa Halmashauri.

Kuandaa mipango ya ukaguzi wa miradi kwa kuzingatia thamani ya fedha.

Kushughulikia kazi zingine zitakazo agizwa na Mkurugenzi Mtendaji bila kuathiri nafasi ya majukumu yake katika utendaji kazi wake.

WADAU WA KITENGO

Kutokana na umuhimu wake kitengo kina wadau mbalimbali wa ndani na nje ya taasisi

yetu ambao ni:-

Serikali kuu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mtaa, Wizara ya Fedha, Afya, Kilito, Maji, Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu).

Menejimenti (Baraza la Madiwani, Mkurugenzi Mtendaji, Wakuu wa Idara na Vitengo).

Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe.

Wadi (Wazabuni na Wakandarasi)

Asasi zisizo za Kiserikali.

Wananchi wa Wilaya ya Karagwe.

 

HALI YA UTOAJI HUDUMA

Kitengo kinafanya kazi katika kupitia na kutoa taarifa kuhusu usimamizi wa mapato na matumizi, raslimali mali na watu, utawala bora, ushirikishwaji na uwazi katika manunuzi ya umma.

Mawanda ya utendaji kazi wa kitengo ni  mpana na katika kutekeleza kazi zake kwa ufanisi uwezeshwaji wa dhati kutoka kwenye menejimenti hauna budi kufanyika.

FURSA ZILIZOPO:

Kitengo kina fursa mbalimbali ambazo inazitumia kuongeza ufanisi na ubora wa huduma kazi na kwa Halmashauri kwa ujumla. Baadhi yake ni kama ifuatavyo:-

Kitengo cha Ukaguzi wa ndani kilipata gari la kufuatilia miradi na taasisi ngazi za chini.

Kuwepo kwa mfumo wa kompyuta wa kutunza taarifa za fedha.

Idara nyingi kuwa na vitendea kazi vya kompyuta ambazo zinarahisisha upatikanaji na utunzaji wa taarifa kwa wakati.

Ushirikiano wa dhati toka kwa baadhi ya wakuu wa idara kuwezesha kitengo kutekeleza majukumu yake kikamilifu.

Watumishi kuruhusiwa kuhudhuria mafunzo na semina kwa ajili ya kuboresha ufahamu na taaluma.

Ikama ya kitengo cha Ukaguzi wa ndani kutofikiwa


HITIMISHO:

Tunapenda kutoa shukrani kwa wadau wetu mbalimbali kwa ushirikiano mkubwa tunaoupata na kutuwezesha kufanya kazi zetu. Baadhi ya wadau tunaofanya nao kazi kwa ukaribu ni Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji, Wakuu wa Idara, Baraza la Madiwani, Kamati zote za Kudumu, Kamati ya Ukaguzi, Ofisi ya Katibu Tawala Mkoa wa Kagera, Ofisi ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Serikali Mkazi Kagera na Ofisi ya mkaguzi mkuu wa ndani wa serikali.



Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO YA ASILIMI 10 October 04, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI KADA YA DEREVA II NA WAANDISHI WAENDESHA OFISI II September 30, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI WASAIDIZI KUMBUKUMBU DARAJA LA II NA MTENDAJI WA KIJIJI WA III October 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI February 21, 2022
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KAMATI YA LISHE YAKETI KUJADILI UTEKELEZAJI WA AFUA ZA LISHE, KIPINDI CHA ROBO YA TATU 2024/2025.

    April 22, 2025
  • KUELEKEA MSIMU WA KAHAWA 2025/2026: MAAFISA UGANI KARAGWE DC WAPEWA MAFUNZO ILI KUWASAIDIA WANANCHI KUONGEZA THAMANI YA ZAO HILO.

    April 11, 2025
  • WALENGWA WA TASAF KARAGWE DC WANUFAIKA NA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA KIFEDHA WALIZOANZISHA.

    March 17, 2025
  • DC LAIZER AWATAKA WANAWAKE WA KARAGWE KUJIIMARISHA KIUCHUMI.

    March 08, 2025
  • Angalia zote

Video

SHIRIKI UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 KARAGWE TUMEJIPANGA
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • History
  • Dira na Dhamira
  • Fomu za mbalimbali
  • NEEMA INAKUJA KWA WAKULIMA
  • FEDHA ZILIZOPOKELEWA KWA AJILI YA MFUKO WA JIMBO

Viunganishi vihusishi

  • NECTA
  • UTUMISHI
  • TOVUTI YA TAIFA
  • TAMISEMI
  • FFARS
  • SALARY SLIP

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    KARAGWE KAGERA TANZANIA

    Anuani ya posta: BOX 20 KARAGWE

    Simu: 028-2227148

    Simu ya mkononi: 028-2227148

    Barua pepe: ded@karagwedc.go.tz ded.karagwedc@kagera.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright©2017 karagwedc. All rights reserved.