IDARA YA MAENDELEO YA JAMII NA USTAWI WA JAMII
UTANGULIZI
MIKOPO
Halmashauri ya Wilaya Karagwe kupitia Idara ya Maendeleo ya Jamii imekuwa ikitoa mikopo kwa SACCOSS na vikundi vya wanawake na vjiana tangu 1998 kupitia mfuko wa mzunguko wa wanawake na vijana. Vikundi hivyo vimenufaika kwa kuboresha miradi yao ambayo imewapelekea kuinuka kiuchumi na kuboresha hali za maisha yao na pia kuongeza ajira kwa vijana.
Mikopo hii inatolewa kwa masharti nafuu ukilinganisha na taasisi nyingine zinazotoa mikopo.Vigezo vichache vinavyotumika ni kama ifuatavyo:-
Kuhusu suala la UKIMWI Idara ya maendeleo ya Jamii inahamasisha wananchi juu ya
UKIMWI.
Jukumu muhimu la idara pia ni kuhakikisha wananchi wanaelimishwa juu ya umuhimu wa kusajili vikundi.Kuanzia mwaka 2014,idara imeshasajili jumla ya vikundi 1046.Vigezo vya kusajili ni kikundi kuwa na katiba, kutambuliwa na ngazi za kijiji na kata, kuwa na wanakikundi wasiopungua watano.
USAJILI WA VIKUNDI.
Kwa mwaka wa fedha 2016/2017 kuanzia July 2016 hadi Machi 2017 jumla ya sh.159,000,000 ( Milioni mia moja hamsini na tisa elf tu) zilitolewa kwa vikundi 78 vya wanawake na vijana, tayari baadhi ya vikundi wameanza kurejesha ambapo kati ya Tsh 170,130,000 tayari zimerejeshwa Tsh 12,363,333/= bado 157,766,666/= .Vikundi vyote bado vipo ndani ya muda wa urejeshaji.
Aidha kwa Mwaka 2015/2016 jumla ya sh. 125,188,000 zilitolewa kwa vikundi 41 na SACCOSS 3. Kati ya fedha hizo 28,000,000 ni kutoka Wizara ya Sera, Bunge, Vijana Kazi, Ajira na Walemavu ni 97,188,000 ni kutoka mfuko wa mzunguko wa wanawake na vijana utokanao na mapato ya ndani. Kiasi kilichorejeshwa kwa mikopo hii hadi sasa ni sh. 2,7349,000 tu hivyo kiasi kinachodaiwa ni sh 97,839,000/= lakini bado wapo ndani ya muda wa urejeshaji na 62,188,000 ni za mizinga ambazo zitaanza kurejeshwa baada miezi 12,hii ni kutokana na uhalisia wa mradi wenyewe wa ufugaji nyuki. Kwa kuwa mkopo huo utarudishwa ndani ya miaka 2 ikiwa ni pamoja na riba ya 14%.
Kwa mwaka 2014/2015 jumla ya Tsh 67,500,000 zilikopeshwa kwa vikundi 12 na SACCOS 4, kati ya fedha hizo 20,000,000 ni fedha zilizopokelewa kutoka Wizara ya Sera, Bunge, Vijana Kazi, Ajira na Walemavu na 47,500,000 ni kutoka mfuko wa mzunguko wa wanawake na vijana utokanao na mapato ya ndani. Kiasi kilichorejeshwa hadi sasa ni sh. 67,341,700 hivyo kiasi kinachodaiwa ni sh. 5,483,300 Vikundi husika vimefikishwa mahakamani kwa kukiuka makubaliano kwa mujibu wa mkataba. Vikundi ambavyo mwenendo wao wa urejeshaji siyo mzuri wameshaandikiwa notisi ya siku 14 na taratibu za kuwafikisha mahakamani zimeanza.
HALI YA MIKOPO NA UREJESHAJI KUANZIA MWAKA 2014/2015 HADI MACHI 2017
Halmashauri ya Wilaya Karagwe ilianza kutoa mikopo kwa vikundi vya wanawake na vijana tangu mwaka 1998.Hadi kufikia March 2017 mfuko ulikuwa na thamani ya Tsh 333,196,893(Milioni mia tatu thelathini na tatu, laki moja na tisini na sita elfu na mia nane tisini na tatu tu).Kati ya hizo madeni sugu ni Tsh 30,776,900/=, Madeni yaliyopo ndani ya muda ni Tsh 304,898,060 na Benki kulikuwa na Tsh. 28,298,833/=. Aidha Halmashauri ilipokea mkopo wa Jumla ya TSH 48,000,000/= kutoka Wizara Wizara ya Sera, Bunge, Vijana Kazi, Ajira na Walemavu..
HALI HALISI YA MFUKO
Mfuko huu unapata mtaji kutokana na riba ambapo kila kikundi kinarejesha mkopo na asilimia 7% tu na mchango wa Halmashauri kutoka kwenye mapato ya ndani ambapo Halmashauri imekuwa ikichangia.Mfano, kuanzia mwaka 2014/2015 hadi Machi 2017 tayari Halmashauri imeshachangia jumla ya Tsh 165,998,900/=.Halmashauri inaendelea kuongeza kiasi cha kuchangia kadri ya maelekezo ya Serikali kwa nia njema ya kuuongezea nguvu mfuko na hivyo kuongeza wigo wa wanufaika,
MTAJI WA MFUKO WA WANAWAKE NA VIJANA
Utekelezaji wa dawati hili umeanza rasmi mwezi Machi 2017 baada ya mratibu kupewa mafunzo elekezi.Majukumu ya dawati hili ni pamoja na
DAWATI LA UWEZESHAJI WANANCHI KIUCHUMI
Maafisa vijana wanahamasisha vijana kuunda vikundi na Saccos.Wilaya ya Karagwe ina SACCOS 7 za vijana na vikundi 363 vya vijana vilivyosajiliwa. Idara pia iliwawezesha vijana kuandika maandiko ya miradi na kuyawasilisha wizara ya Sera, Bunge, Vijana Kazi, Ajira na Walemavu ambapo jumla ya TSH 48,000,000 zilitolewa kwenye vikundi. Hadi sasa jumla ya Tsh ….. zimesharejeshwa wizarani bado Tsh……… na mwisho wa kurejesha ni mwezi July 2018.
SHUGHULI ZA VIJANA
Halmashauri pia inagharimia wanafunzi wanaosoma shule za Mgeza mseto,Mkorani sekondari, Shinyanga sekondari kwa mahitaji ya shule na usafiri wa kwenda na kurudi shule.Jumla ya wanafunzi 86 wanasaidiwa.
Halmashauri ilitoa huduma za baiskeli 6 kwa watu wenye ulemavu wa viungo na watu wenye ulemavu wa ngozi 35 walipatiwa lotion(mafuta ya kupaka) kwa ajili ya ngozi yao.
Huduma za watu wenye ulemavu.
.
Jumla ya vituo vilivyosajiliwa 2 na vilivyo kwenye mchakato ni vituo vitano.
Huduma kwa vituo vya watoto wadogo
Huduma hizi hutolewa ili kuwawezesha watoto ambao wazazi wao wako kwenye migogoro kupata haki na mahitaji ya msingi.Jumla ya migogoro ya matunzo ipatayo 167 imeshughulikiwa kwa mwaka 2015/2016 hadi Machi 2017.
Huduma za migogoro ya matunzo
Ustawi wa Jamii, idara inasaidia kusuluhisha migogoro ya ndoa na inayoshindikana hupelekwa mahakamani kwa hatua zaidi za kisheria.Kwa mwaka wa fedha 2016/2016 hadi Machi 2017 jumla ya migogoro 197 imesikilizwa.
Huduma za usuluhishi wa ndoa zenye mifarakano.
SHUGHULI ZA USTAWI WA JAMII
Pia Idara inahudumia wathirika na waathiriwa wa UKIMWI kwa kuwapa vyakula na kuwalipia huduma ya matibabu kupitia mfuko wa CHF.Jumla ya watu….. wamepatiwa chakula na kaya ……. zimelipiwa bima ya Afya kwa mwaka wa fedha 2016/2017.
Hadi sasa Halmashauri imeshatekeleza yafuatayo:-
KARAGWE KAGERA TANZANIA
Anuani ya posta: BOX 20 KARAGWE
Simu: 028-2227148
Simu ya mkononi: 028-2227148
Barua pepe: ded@karagwedc.go.tz ded.karagwedc@kagera.go.tz
Copyright©2017 karagwedc. All rights reserved.