• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
KARAGWE DISTRICT COUNCIL
KARAGWE DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KARAGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na dira
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
        • Sekondari
        • Msingi
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Mazingira na Taka ngumu
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Ufugaji na Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Inayokuja
    • Iliyotekelezwa
    • Inayoendelea
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Taarifa
    • Sheria
    • Mpango mkakati
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha

Maendeleo ya Jamii

IDARA YA MAENDELEO YA JAMII NA USTAWI WA JAMII

 

 UTANGULIZI

  • Idara ya Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa jamii ni miongoni mwa Idara za Halmashauri. Idara ina vitengo kama vile  jinsia, wanawake na watoto, Utafiti na Mpango, UKIMWI, Kikosi cha Ufundi, Vijana,Ustawi wa Jamii, Mashirika yasiyokuwa ya Kiserikali na Dawati la uwezeshaji.Idara hii kupitia vitengo hivi  ina majukumu yafuatayo;-
  • 1.Kuratibu shughuli za kudhibiti UKIMWI, kuhamasisha jamii kupiga vita unyanyapaa na kuwatunza watu wanaoishi na VVU/UKIMWI,kuelimisha wananchi juu ya kujikinga na maabukizi mapya ya UKIMWI na kuanzisha miradi ya kiuchumi
  • 2. .Kuhamasisha jamii kujenga nyumba bora na kutumia technolojia sahihi na rahisi kwa kutumia enterblocking mashine
  • 3. Kukusanya takwimu za makundi tete vijijini na kuzitunza kwa matumizi ya maendeleo.
  • 4. Kutoa huduma za majaribio za ujenzi na tabia nzuri kwa waliotiwa hatiani na mahakama na kuwapa ushauri mbalimbali
  • 5.   Kushauri wenye matatizo ya kifamilia wanaojitokeza ili kupunguza migogoro katika familia
  •  6.  Kuratibu shughuli za vikundi vya wanawake na vijana ikiwa ni pamoja na kutoa mikopo midogomidogo.
  • 7.  Kuhamasisha wananchi kwa ajili ya kupanga na kutekeleza majukumu yao wenyewe
  • 8. Kuhamasisha jamii na makundi yote maalum kama wazee, vijana na watu wenye ulemavu kuanzisha miradi ya kujitegemea ikiwa ni pamoja na kuanzisha SACCOS na VICOBA.
  • 9. Kuratibu shughuli za asasi za kiraia pamoja na usajili wa vikundi vya kijamii.
  •  
  • Aidha, Idara ina  jumla ya watumishi 21 ikwa  CDO’s   5, CD-TECH    4, ACDO   8, YDO 2, SWO  1 na mwalimu wa watoto wadogo 1

 

MIKOPO

 

Halmashauri ya Wilaya Karagwe kupitia Idara ya Maendeleo ya Jamii imekuwa ikitoa mikopo kwa SACCOSS  na vikundi vya wanawake na vjiana tangu 1998 kupitia mfuko wa mzunguko wa wanawake na vijana. Vikundi hivyo vimenufaika kwa kuboresha miradi yao ambayo imewapelekea kuinuka kiuchumi na kuboresha hali za maisha yao na pia kuongeza ajira kwa vijana.

Mikopo hii inatolewa kwa masharti nafuu ukilinganisha na taasisi nyingine zinazotoa mikopo.Vigezo vichache vinavyotumika ni kama ifuatavyo:-

  • Uwepo wa kikundi kisichopungua watu watano ila wasiwe wanafamilia moja
  • Kikundi kiwe kinatambuliwa/kimesajiliwa na Halmashauri ya Wilaya Karagwe
  • Kikundi kiwe na mradi unaonendelea ili mkopo uongeze mtaji tu.
    • Vikundi vinavyojishughulisha na Kuweka na Kukopa vinapewa kipaumbele
    • Uhai wa kikundi kwa maana ya kuwa na  Uongozi ,katiba na mihitasari ya vikao.
  • Kuhusu suala la UKIMWI Idara ya maendeleo ya Jamii inahamasisha wananchi juu ya

     

    UKIMWI.

     

     

    Jukumu muhimu la idara pia ni kuhakikisha wananchi wanaelimishwa juu ya umuhimu wa kusajili vikundi.Kuanzia mwaka 2014,idara imeshasajili jumla ya vikundi 1046.Vigezo vya kusajili ni kikundi kuwa na katiba, kutambuliwa na ngazi za kijiji na kata, kuwa  na wanakikundi wasiopungua watano.

    USAJILI WA VIKUNDI.

     

    Kwa mwaka wa fedha 2016/2017 kuanzia July 2016 hadi Machi 2017 jumla ya sh.159,000,000 ( Milioni mia moja hamsini na tisa elf tu) zilitolewa kwa vikundi 78 vya wanawake na vijana, tayari baadhi ya vikundi wameanza kurejesha ambapo kati ya Tsh 170,130,000 tayari zimerejeshwa Tsh 12,363,333/= bado 157,766,666/= .Vikundi vyote bado vipo ndani ya muda wa urejeshaji.

     

     

     

    Aidha kwa Mwaka 2015/2016 jumla ya sh. 125,188,000 zilitolewa kwa vikundi 41 na SACCOSS 3. Kati ya fedha hizo 28,000,000 ni kutoka Wizara ya Sera, Bunge, Vijana Kazi, Ajira na Walemavu  ni 97,188,000 ni kutoka mfuko wa mzunguko wa wanawake na vijana utokanao na mapato ya ndani. Kiasi kilichorejeshwa kwa mikopo hii hadi sasa ni sh. 2,7349,000 tu hivyo kiasi kinachodaiwa ni sh 97,839,000/= lakini bado wapo ndani ya muda wa urejeshaji na 62,188,000 ni za mizinga ambazo zitaanza kurejeshwa baada miezi 12,hii ni kutokana na uhalisia wa mradi wenyewe wa ufugaji nyuki. Kwa kuwa mkopo huo utarudishwa ndani ya miaka 2 ikiwa ni pamoja na riba ya 14%.

    Kwa mwaka 2014/2015 jumla ya Tsh 67,500,000 zilikopeshwa kwa vikundi  12 na SACCOS  4, kati ya fedha  hizo 20,000,000 ni fedha zilizopokelewa kutoka Wizara ya Sera, Bunge, Vijana Kazi, Ajira na Walemavu  na 47,500,000 ni kutoka mfuko wa mzunguko wa wanawake na vijana utokanao  na mapato ya ndani. Kiasi kilichorejeshwa hadi sasa ni sh. 67,341,700 hivyo kiasi kinachodaiwa ni sh. 5,483,300 Vikundi husika vimefikishwa mahakamani kwa kukiuka makubaliano kwa mujibu wa mkataba. Vikundi ambavyo mwenendo wao wa urejeshaji siyo mzuri wameshaandikiwa notisi ya siku 14 na taratibu za kuwafikisha mahakamani zimeanza.

     

    HALI YA MIKOPO NA UREJESHAJI KUANZIA MWAKA 2014/2015 HADI  MACHI 2017

     

    Halmashauri ya Wilaya Karagwe ilianza kutoa mikopo kwa vikundi vya wanawake na vijana tangu mwaka 1998.Hadi kufikia March 2017 mfuko ulikuwa na thamani ya Tsh 333,196,893(Milioni mia tatu thelathini na tatu, laki moja na tisini na sita elfu na mia nane tisini na tatu tu).Kati ya hizo madeni  sugu ni Tsh 30,776,900/=, Madeni yaliyopo ndani ya muda ni Tsh 304,898,060 na Benki kulikuwa na Tsh. 28,298,833/=. Aidha Halmashauri ilipokea mkopo wa Jumla ya TSH 48,000,000/= kutoka Wizara Wizara ya Sera, Bunge, Vijana Kazi, Ajira na Walemavu..

    HALI HALISI YA MFUKO

    Mfuko huu unapata mtaji kutokana na riba ambapo kila kikundi kinarejesha mkopo na asilimia 7% tu na mchango wa Halmashauri kutoka kwenye mapato ya ndani ambapo Halmashauri imekuwa ikichangia.Mfano, kuanzia mwaka 2014/2015 hadi Machi 2017 tayari Halmashauri imeshachangia jumla ya Tsh 165,998,900/=.Halmashauri inaendelea kuongeza  kiasi cha kuchangia kadri ya maelekezo ya Serikali kwa nia njema ya kuuongezea nguvu mfuko na hivyo kuongeza wigo wa wanufaika,

    MTAJI WA MFUKO WA WANAWAKE NA VIJANA


    • Kuhakikisha wanaacha vitendo vinavyowaingiza katika hatari ya kupata maambukizi mapya.
    • Kupima kwa hiari ili waweze kufahamu afya zao na hivyo kujiunga na huduma za CCT na kwa wale watakaokutwa hawana Virus basi wachukue hatua za kujilinda zaidi.Jumla ya watu……… walipima VVU kwa mwaka 2016/2017.
    • Kuacha unyanyapaa kwa wale waliojiweka wazi.
  • Utekelezaji wa dawati hili umeanza rasmi mwezi Machi 2017 baada ya mratibu kupewa mafunzo elekezi.Majukumu ya dawati hili ni pamoja na

    DAWATI LA UWEZESHAJI WANANCHI KIUCHUMI

    Maafisa vijana wanahamasisha vijana kuunda vikundi na Saccos.Wilaya ya Karagwe  ina SACCOS 7 za  vijana na vikundi 363 vya vijana vilivyosajiliwa. Idara pia iliwawezesha vijana kuandika maandiko ya miradi na kuyawasilisha wizara ya Sera, Bunge, Vijana Kazi, Ajira na Walemavu ambapo jumla ya TSH 48,000,000 zilitolewa kwenye vikundi. Hadi sasa jumla ya Tsh ….. zimesharejeshwa wizarani bado Tsh……… na mwisho wa kurejesha ni mwezi July 2018.

    SHUGHULI ZA VIJANA

     

    Halmashauri pia inagharimia wanafunzi wanaosoma shule za Mgeza mseto,Mkorani sekondari, Shinyanga sekondari kwa mahitaji ya shule na usafiri wa kwenda na kurudi shule.Jumla ya wanafunzi 86   wanasaidiwa.

    Halmashauri ilitoa huduma za baiskeli 6 kwa watu wenye ulemavu wa viungo na watu wenye ulemavu wa ngozi 35 walipatiwa lotion(mafuta ya kupaka) kwa ajili ya ngozi yao.

    Huduma za watu wenye ulemavu.

    .

    Jumla ya vituo vilivyosajiliwa 2 na vilivyo kwenye mchakato ni vituo vitano.

    Huduma kwa vituo vya watoto wadogo

     

    Huduma hizi hutolewa ili kuwawezesha watoto ambao wazazi wao wako kwenye migogoro kupata haki na mahitaji ya msingi.Jumla ya migogoro ya matunzo ipatayo 167 imeshughulikiwa kwa mwaka 2015/2016 hadi Machi 2017.

    Huduma za migogoro ya matunzo

     Ustawi wa  Jamii, idara inasaidia kusuluhisha migogoro ya ndoa na inayoshindikana hupelekwa mahakamani kwa hatua zaidi za kisheria.Kwa mwaka wa fedha 2016/2016 hadi Machi 2017  jumla ya migogoro    197 imesikilizwa.

    Huduma za usuluhishi wa ndoa zenye mifarakano.

    SHUGHULI ZA USTAWI WA JAMII

    Pia Idara inahudumia wathirika na waathiriwa wa UKIMWI kwa kuwapa vyakula na kuwalipia huduma ya matibabu kupitia mfuko wa CHF.Jumla ya watu….. wamepatiwa chakula na kaya ……. zimelipiwa bima ya Afya kwa mwaka wa fedha 2016/2017.


    1. Kusimamia na kufuatilia  shughuli za uwezeshaji zinazofanywa katika kata na vijiji/mitaa katika Halmashauri.
    2. Kutafsiri na kusimamia utekelezaji wa sera na sheria ya Taifa ya uwezeshaji wananchi kiuchumi na mkakati wa Taifa wa Uwezeshaji wananchi kiuchumii katika halmashauri.
    3. Kukusanya taarifa na tafiti mbalimbali na kumshauri Mkurugenzi wa Halmashauri katika masuala ya uwezeshaji kiuchumi na ushiriki wa watanzania.
    4. Kuhakikisha fedha za uendeshaji zinatengwa katika bajeti kila mwaka juu ya masuala ya uwezeshaji.
    5. Kuhakikisha kuwa Halmashauri inahusisha suala la hifadhi ya mazingira na mabadiriko ya tabia ya nchi katika mipango ya maendeleo ya wilaya ili kuboresha mazingira ambayo nim muhimu katika suala zima la uzalishaji wa mazao ya kilimo,mifugo na uvuvi.
    6. Kubuni kutafuta vyanzo vya rasilimali kwa ajili ya shughuli za uwezeshaji katika hamashauri.
    7. Kuratibu na kuhamasisha uanzishwaji na uendelezaji wa vikundi vya kiuchumi kama SACCOS, VICOBA na vinginevyo vinavyosajiliwa na kutambuliwa toka ngazi ya Wilaya hadi Taifa.
    8. Kuwasilisha taarifa ya utekelezaji  kwa kamati ya uwezeshaji ya halmashauri na baada ya kuidhinishwa itumwe kwa mratibu wa Uwezeshaji Mkoa  na nakala kwa baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi.
    9. Kuhamasisha vikundi vya kijamii na kiuchumi kujisajili/kujirasimisha  na kufanya uzalishaji wenye viwango kama vya TBS, TFDA na kupata nembo ya utambuzi wa bidhaa(msimbomilia(Barcode)
    10. Kuandaa taarifa ya Maendeleo ya vyama vya ushirika hasa SACCOS na vikundi vya kiuchumi kama VICOBA vilivyopo katika Halmashauri.
    11. Kubuni fursa mbalimbali za uwekezaji katika Hamashauri
    12. Kufuatilia upatikanaji wa masoko ya bidhaa za kiuchumi
    13. Kushauri namna ya uboreshaji wa vituo vidogovidogo vya kibiashara hususani katika vijiji na mamlaka ya miji midogo.
    14. Kuhakikisha halmashauri inatoa kipaumbele (preferential treatment) kwa watanzania hasa wakazi wa kwenye Halmashauri katika utoaji wa Zabuni.
  • Hadi sasa Halmashauri imeshatekeleza yafuatayo:-


    • Halmashauri imeshaanzisha dawati la uwezeshaji wananchi kiuchumi ambapo Afisa wa Dawati ni Afisa Maendeleo ya Jamii kama mwongozo ulivyoelekeza.
    • Halmashauri imeisha zindua jukwaa la uwezeshaji wanawake  kiuchumi tangu tarehe 07/03/2018.
    • Timu ya menejimenti na kamati ya Ujenzi,Uchumi na Mazingira zimejengewa uwezo kupitia vikao vya kisheria vya Halmashauri

Matangazo

  • MATOKEO DARASA LA SABA 2022 December 01, 2022
  • WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA SEKONDARI 2023 December 14, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI July 09, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI February 21, 2022
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • ZAWADI

    September 26, 2022
  • WAJERUMANI WASAINI KITABU KWA DED

    September 26, 2022
  • KARAGWE YAPOKEA WAJERUMANI

    September 25, 2022
  • KAMATI YA FEDHA MAFUNZONI

    September 16, 2022
  • Angalia zote

Video

BARAZA LA MADIWANI LAWASIMAMISHA WATUMISHI
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • History
  • Dira na Dhamira
  • Fomu za mbalimbali
  • NEEMA INAKUJA KWA WAKULIMA
  • FEDHA ZILIZOPOKELEWA KWA AJILI YA MFUKO WA JIMBO

Viunganishi vihusishi

  • NECTA
  • UTUMISHI
  • TOVUTI YA TAIFA
  • TAMISEMI
  • FFARS
  • SALARY SLIP

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    KARAGWE KAGERA TANZANIA

    Anuani ya posta: BOX 20 KARAGWE

    Simu: 028-2227148

    Simu ya mkononi: 0754653409

    Barua pepe: ded@karagwedc.go.tz ded.karagwedc@kagera.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright©2017 karagwedc. All rights reserved.