• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
KARAGWE DISTRICT COUNCIL
KARAGWE DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KARAGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na dira
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
        • Sekondari
        • Msingi
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Mazingira na Taka ngumu
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Ufugaji na Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Inayokuja
    • Iliyotekelezwa
    • Inayoendelea
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Taarifa
    • Sheria
    • Mpango mkakati
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha

Ufugaji wa nyuki

KITENGO CHA UFUGAJI NYUKI

Ufugaji  nyuki ni kati ya kazi za kiuchumi zinazofanywa na watu wa Wilaya ya Karagwe.  Kazi ya ufugaji Nyuki hufanywa na watu binafsi, vikundi vya kijamii (CBO’s),  taasisi (NGO,s) na taasisi za umma kama vile mashule.  Mpaka sasa kuna idadi ya wafugaji nyuki na  vikundi 258, idadi ya mizinga ya kisasa 3,551, mizinga ya kienyeji 5,592, jumla  ya mizinga yote 7,143, kiasi cha asali kinachotegemewa kuvunwa ni Kg 91,430, na  kiasi cha nta ni Kg 18,286U

wekezaji katika Sekta ya Nyuki 

  • Halamshauri  ya wilaya imetengeneza jumla ya mizinga 1000 kwa mwaka 2015/16 yenye thamani ya Tsh 70,000,000 ambayo itagawiwa  kwa vikundi 40 vya wanawake na vijana.  Aidha kwa mwaka wa fedha  2016/17  zimetengwa Tsh. 60,000,000 kwa shughuli hiyo    
  • Kupitia  miradi ya ruzuku ya maendeleo, kikundi cha Mabadiliko Vijana Kishoju kimewezeshwa kutengeneza mizinga  ya kisasa. Jumla ya    mizinga 100 aina ya  TTBH (Tanzania Transitional Bee Hives). Pia banda   moja la kuhifahi mizinga hiyo limetengenezwa na tayari nyuki  wameingia kwenye baadhi ya mizinga.    

Changamoto zinazoikabili Sekta ya Ufugaji wa Nyuki    

  • Uharibifu wa mazingira: kazi za  binadamu hasa uchomaji moto ovyo,  ukataji  miti ovyo, ufugaji wa mifugo hasa matumizi ya dawa za kuua  kupe, na kazi nyinginezo zimechangia katika  kupunguza makundi ya nyuki.     
  • Mwamko ndogo wa jamii: bado  jamii kubwa haina mwamuko wa kutosha  katika sekta hii.    
  • Matatizo ya soko huria: Kila mara imekua ni vigumu kupata takwimu     za  kutosha kutokana na wafugaji wengi kuuza mazao ya nyuki kwa wanunuzi wanaotoka ndani na nje ya nchi  bila ofisi kupata takwimu  hizo.   

Mkakati wa kuendeleza sekta ya ufugaji wa nyuki.    

  • Mkakati ni  Halmashauri kuendelea kushirikiana na sekta mbalimbali ili kuboresha ufugaji nyuki na utunzaji wa  mazingira, kuendelea kutoa elimu kwa wananchi juu  ya faida za ufugaji nyuki, na kuboresha utendaji  wa Kitengo cha Nyuki ikiwa ni pamoja na kuandaa maandiko  ya miradi kwa kutafuta uwekezaji zaidi katika  sekta hii.  






TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA MAJUKUMU YA SEKTA YA UFUGAJI NYUKI KWA MWAKA 2016/2017

 

Madhumuni ya Ufugaji Nyuki

Kwa mujibu wa Sera ya Taifa ya Ufugaji Nyuki ya mwaka 1998, Sheria ya Ufugaji Nyuki Namba 15 ya mwaka 2002 na Kanuni zake za mwaka 2005, ufugaji nyuki una malengo makuu matatu ambayo ni:

  1. Kuhakikisha kuwa nyuki wanahifadhiwa kwa misingi endelevu kwa faida ya kizazi kilichopo na kizazi kijacho.
  2. Kuinua uchumi wa wafugaji nyuki kupitia kuinua viwango vya ubora na wingi wa asali, nta, na mazao mengine ya nyuki na kuboresha soko la mazao hayo.
  3. Kuboresha na kukuza wingi wa mahusiano baina ya nyuki, viumbe wengine na mazingira (Bio-diversity = Bioanuwai) ili kuongeza ubora wa mazao ya kilimo na mimea ya asili.

Ili kuweza kutekeleza malengo tajwa hapo juu, Kitengo cha Ufugaji Nyuki kimefanya yafuatayo kwa mwaka 2016/2017.

A: Kazi zilizofanyika kwa kipindi tajwa ni kama ifuatavyo

Kutoa ushauri wa kitaalamu kwa wananchi waliofika ofisini: Jumla ya wanachi 28 walifika ofisini kwa vipidi tofauti kuomba ushauri wa njia bora za ufugaji nyuki. Ushauri uliotelewa ni pamoja na njia bora za utengenezaji, uambikaji na utundikaji wa mizinga, jinsi ya kutengeneza mizinga ya kisasa (modern bee hives), jinsi ya kuboresha mizinga ya asili ili kulinda ubora wa mazao yanayovunwa, habari ya masoko kwa mazao ya nyuki  na utunzaji wa mazingira kwa ujumla.

Kuendesha mafunzo ya ufugaji nyuki na utunzaji wa mazingira kwa njia ya redio:  Jumla ya vipindi 43 vya utunzaji wa mazingira kupitia upandaji wa miti, utunzaji wa vyanzo vya maji na ufugaji nyuki kupitia Redio FADECO vilienda hewani. Vipindi hivi vilirushwa kila siku ya jumatatu ya wiki kuanzia saa 3.00 – 4.00 asubuhi. Vipindi hivi havilipiwi na Halmashauri gharama yoyote bali ni mchango wa redio katika kuielimisha jamii na kuongeza hamasa ya ufugaji nyuki na utunzaji wa mazingira.

Kuhusu ufugaji wa nyuki, vipindi hivi viliielimisha jamii juu ya mada zifuatazo:

  1. Matatizo yanayojitokeza katika uzalishaji wa asali na nta bora – matatizo yanayohusu ubora wa maeneo ya ufugaji nyuki, matatizo yanayohusu uelewa sahihi usiowatoshelezea wadau wa ufugaji nyuki, matatizo yanayohusu mbinu za uvunaji na uchakataji, matatizo yanayohusu vifaa vya kuhifadhia mazao ya nyuki na matatizo yanayohusu usafirishaji wa mazao ya nyuki.
  2. Uzalishaji bora wa mazao ya nyuki- ubora wa maeneo ya kufugia nyuki, huduma bora za ugani ninazotolewa na kitengo cha nyuki, maandalizi ya mizinga ya nyuki, njia sahihi za upatikanaji wa makundi ya nyuki, afya na ustawi wa makundi ya nyuki, njia sahihi za uvunaji wa mazao ya nyuki, njia sahihi za ufungashaji wa mazao ya nyuki, uhifadhi na usafirishaji wa mazao ya nyuki, na masoko ya mazao ya nyuki.
  3. Viwango vya ubora wa asali na nta.
  4. Uchukuaji wa sampuli ya asali na uchunguzi katika maabara ili kulinda afya za watumiaji wa mazao ya nyuki.
  5. Uthibitisho wa asali mahuluku (organic honey) na vipengele muhimu vya mfumo wa uthibitisho wa asali mahuluku
  6.   Muundo na tabia ya asali na nta – muundo wa asali, tabia ya asali na tabia ya nta ya nyuki,

Mafunzo haya yalikuwa na madhumini yafuatayo kwa jamii:

  • Kuhakikisha uwepo wa ufugaji wa nyuki endelevu kwa kuwaelimisha wananchi kutumia njia bora na za kisasa katika kufuga nyuki,
  • Kuboresha uzalishaji na ubora wa mazao ya nyuki kama vile asali na nta kwa wafugaji wa karagwe,
  •  Kupunguza uharibifu wa mazingira na uboreshaji wa kipato na lishe kutokana na ufugaji wa nyuki, na
  • Kuongeza ubora wa mazao ya kilimo hasa kahawa na mimea mingine kutokana na huduma za uchavushaji zinazofanywa na nyuki.

Kutembelea wafugaji nyuki vijijini na kuwaelimisha juu ya ufugaji bora: Vikundi vya wafugaji nyuki na wafugaji binafsi waliko maeneo mbalimbali ya Karagwe walitembelewa kwa lengo la kuwaelemisha na kuwashauri juu ya upunguzaji wa changamoto walizonazo.

 

Maeneo ya ufugaji nyuki Karagwe

Nyuki wanafugwa kwenye kata zote 23 za wilaya ya Karagwe lakini maeneo yanayofuga zaidi nyuki ni pamoja na;

Kata ya Bweranyange kwenye vijiji vya Muguruka na Chamchuzi

Kata ya Nyakasimbi kwenye vijiji vya Muungano na Chanyamisa

Kata ya Rugu kwenye vijiji vya Ruhita, Misha na Rugu

Kata ya Kihanga kwenye vijiji vya Kihanga, Katanda na Mulamba

Kata ya chanika kwenye vijiji vya Mchuba, Chanika na Runyaga na Ruzinga

Kata ya Nyakahanga kwenye vijiji vya Nyakahanga, Rwandalo, Omurusimbi na Bisheshe

Kata ya Rugera kwenye vijiji vya Rugera, Omukakajiji na Nyarugando

Kata ya Nyaishozi kwenye vijiji vya Rukale na Nyakayanja na

Kata ya Igurwa kwenye kijiji cha Kigarama.

Maeneo tajwa hapo huu yametembelewa zaidi kutokana na hatuwa waliokwisha fikia kwenye swala zima la ufugaji nyuki, ingawa pia na maeneo mengine ya Halmashauri yalitembelewa ili kuongeza hamasa ya ufugaji yuki.























Baadhi ya mizinga ya kisasa iliyotolewa kwa vikundi vya vijana na wanawake na ile ya kienyeji waliyonayo


 

 

 


Ukusanyaji wa takwimu: Takwimu zilizokusanywa hadi mwishoni mwa mwaka 2016/2017 ni kama ifuatavyo kwenye jedwari hapa chini:

Idadi ya mizinga yenye nyuki

Idadi ya mizinga isiyo na nyuki

Jumla ya mizinga yote

mizinga ya kisasa
mizinga ya asili
mizinga ya kisasa
mizinga ya asili
mizinga ya kisasa
mizinga ya asili

1755

5981

882

2685

2637

8666

Takwimu hizo zinaonyesha kuwa kuna jumla ya makundi ya nyuki 7,736 yenye uwezo wa kuzalisha kiasi cha Kilogramu za asali 77,360 (kwa wastani wa kila mzinga Kg 10 za asali) na Kg 15,472 (kwa wastani wa kila mzinga Kg 2 za nta). Changamoto kubwa iliyopo ni kudhibiti njia za usafirishaji wa mazao haya hasa kwenda nje ya nchi na ukweli wa wafugaji kueleza kiasi hasa wanachovuna. Hili linasababisha kutopata takwimu za kutosha za mazao yanayovunmwa na kuuzwa. Kwa takwimu za mizinga na makundi ya nyuki kwa kila kata angalia kiambatanisho A.

Soko la mazao ya nyuki:

Kwa sasa wanunuzi wakuu wa mazao ya nyuki Karagwe ni CHEMA- Omurushaka na shirika la OLAM. Wanunuzi wengine ni warejareja kwenye masoko ya Kayanga, Omurushaka, Chanyamisa na miji mingine midogo midogo iliyoko Karagwe. Kutokana na kuhitajika kwa asali hasa kwa ajili ya chakula na dawa hakuna mfugaji nyuki anayezalisha asali akakosa soko. Hii inaonyesha kuwa soko la ndani bado lipo na wafugaji tunawahimiza wazalishe zaidi ili tukuze soko la ndani na pia la nje ya Wilaya.

Makampuni makubwa ya ununuzi wa asali yaliyoko kwenye mikoa mingine hasa miko ya kati yamekuwa na ugumu wa kuja kununua asali kwenye wilaya za huku pembezoni kutokana na uzalisha mdogo wa mazao ya nyuki uliopo na umbali pia. Nawashauri vikundi vya nyuki na wafugaji wetu kununua vigungashio na kuuza asali zao moja kwa moja kwa mlaji wa ndani na nje ya wilaya badara ya kusubiri makampuni kutoka nje ya wilaya.

Taasisi za MAVUNO na FADECO nazo ziko kwenye maandalizi ya kuanza kununua, kufungasha na kuuza mazao ya nyuki.
























Baadhi ya picha za mazao ya nyuki yanayochakatwa na Taasisi ya OLAM



Ushirikiano na taasisi nyingine: Kitengo kimeendelea kushirikiana na taasisi nyingine katika kuendeleza ufugaji wa nyuki kwa lengo la kupunguza umaskini na kutunza mazingira. Taasisi tunazofanya kazi nazo  ni pamoja na CHEMA, ELCT, MAVUNO, World Vision, Redio FADECO na OLAM.

  • Taasisi hizi tunashirikiana nazo kwenye kutoa mafunzo mbalimabli yahusuyo ufugaji bora wa nyuki na utunzaji wa mazingira kwa ujumla. Baadhi ya taasisi zimesaidia kufanya uwekezaji kwa kutengeneza mizinga ya kisasa na kuigawa kwa wanachi kwa lengo la kuendeleza swala zima la ufugaji nyuki. Mfano wa taasisi hizo ni CHEMA, MAVUNO na ADP Rugu na ADP Bushangalo.
  • Taasisi ya MAVUNO imetengeneza mizinga 90 ya biashara (commecial bee hives)  na lengo ni kutengeneza mizinga 300. Mizinga hii itatolewa  kwa wafugaji nyuki walioko kwenye kata za Chonyonyo na Ihanda. Pia MAVUNO  tayari imejenga Kiwanda kidogo kwa ajili ya kuchakata na kufungasha mazao ya nyuki na hii itasaidia kuboresha soko la mazao ya nyuki.
















  • Baadhi ya mizinga ya ngazi iliyotengenezwa na taasisi ya MAVUNO


     
  •  
  •  










B: Changamoto

Uharibifu wa mazingira: kazi za binadamu hasa uchomaji moto ovyo, ukataji miti ovyo, matumizi ya dawa za kilimo (herbicides), ufugaji wa mifugo hasa matumizi ya dawa za kuua kupe (acaricides), na kazi nyinginezo zimechangia katika kupunguza makundi ya nyuki.

Ukosefu wa mvua za uhakika kwa kipindi kirefu: kutokana na tatizo la ukame lililoikumba Wilaya ya Karagwe na maeneo mengine hasa kwenye nusu ya kwanza ya mwaka 2016/017, makundi ya nyuki yalikuwa haba na kuchangia mizinga mingi kukosa makundi ya nyuki kwa mda mrefu. Hili lilisababisha baadhi ya mizinga kuanza kuharibika na baadhi ya vikundi kuanza kusambaratika kutokana na kukata tamaa.

Mwamuko ndogo wa jamii: bado jamii kubwa haina mwamuko wa kutosha katika sekta hii kutokana na asili ya watu wa Karagwe ukilinganisha na makabila mengine hapa nchini. Hili limesababisha ukuaji mdogo wa sekta hii kwa wilaya ya Karagwe pamoja na juhudi zinazoendelea kufanyika za uhamasishaji zinazofanywa na Halmashauri na mashirika binafsi.

 

Matatizo ya soko huria: Kila mara imekuwa ni vigumu kupata takwimu za kutosha hasa za mazao ya nyuki kutokana na wafugaji wengi kuuza mazao ya nyuki kwa wanunuzi wanaotoka ndani na nje ya nchi bila kupita ofisini kwetu.

C: Mkakati wa kuendeleza sekta ya ufugaji wa nyuki na kupunguza changamoto

Mkakati wa Kitengo cha Nyuki ni pamoja na;

  1. kuendelea kushirikiana na sekta rafiki kwenye kuwekeza na kutunza miradi ya Ufugaji Nyuki na utunzaji wa mazingira,
  2. kuendelea kutoa elimu kwa wananchi kwa njia ya redio, semina na kuwatembelea vijijini juu ya faida za ufugaji nyuki kwa uchumi wao, kwa jamii na kwa mazingira,
  3. kuboresha hali ya soko la mazao ya nyuki ndani na nje ya wilaya,
  4. kusimamia miradi iliyokwisha anzishwa na kuhakikisha inapata makundi ya nyuki kwa kusambaza mizinga kwenye maeneo mbalimbali, na
  5. kuendelea kuandaa maandiko ya miradi kwa kutafuta uwekezaji zaidi katika sekta hii.

D: Taarifa ya mizinga 1000 ya mikopo kwa vikundi vya wanawake na vijana:

Jumla ya vikundi 28 vya wanawake na vijana vilipewa mkopo wa mizinga 1000 ya kisasa (top Bar Hives). Hadi mwishoni mwa mwaka 2016/017 mizinga 563 sawa na asilimia 56.3 ya mizinga yote imepata makundi ya nyuki na mizinga na 437 sawa na asilimia 43.7 haijapata makundi ya nyuki. Vikundi vingine zaidi ya nusu ya mizinga waliopewa imepata makundi ya nyuki na vingine ni chini ya nusu. Orodha ya vikundi na mizinga walionayo imeambatanishwa kama ‘kiambatanisho B’.

Sababu za  matokeo tajwa hapo juu:

  1. Ukame wa mda mrefu ulisababisha mizinga mingi kukosa makundi ya nyuki kwa mda mrefu wa kusababisha baadhi ya wanavikundi kukata tamaa na kujiondoa ndani ya mradi. Hili limesababisha vikundi vingi kufanya kazi chini ya kiwango.
  2. baadhi ya vikundi kusikiliza na kutekeleza ushauri wa kitaalamu wa jinsi ya kupata makundi ya nyuki kwa urahisi. Mfano, ilitakiwa mizinga kufanyiwa usafi wa mara kwa mara ili kuzuia panya, mijusi, buibui na visumbufu vingine vya nyuki visiingie ndani ya mizinga ili kuwezesha nyuki kuingia kwa urahisi.
  3. Kusambaza mizinga kwenye maeneo mbalimbali kwa ajili ya kudaka makundi ya nyuki kwani nyuki husafiri kutoka eneo moja kwenda jingine kupita njia tofauti. Waliotekeleza hili wamefanikiwa kupata makundi ya nyuki kwa urahisi.
  4. Kufanya usafi wa maeneo yenye mizinga hasa kwa lengo la kupambana na sisimizi na siafu wanaosababisha makundi ya nyuki kuhama mara baada ya kuingia kwenye mizinga. Waliotekeleza hilo wameendea kuwa na makundi ya nyuki kwenye mizinga yao.
  5. Mizinga ilitakiwa kufanyiwa uambikaji wa mara kwa mara kwa lengo la kulua makundi ya nyuki ili waweze kuingia kwa urahisi. Waliotekeleza hili wamefanikiwa kupata makundi ya nyuki kwa urahisi.

Thamani ya mradi:

Jumla ya Tsh. 62,188,000/= zilitumika kununua mizinga 1,000 ambapo bei ya kila mzinga ilikuwa Tsh. 62,118/=. Riba ya asilimia 14 ilitakiwa kulipwa na mtaji (principal) na hivo jumla ya Tsh. 70,894,320/= zinatakiwa kulipwa na mradi (wanavikundi). Mkopo huu unatakiwa kuanza kulipwa baada ya mwaka mmoja ambao umeisha june 2016 na ni matumaini kuwa baadhi ya vikundi wataanza kurejesha.

Naomba kuwasilisha.

Rajabu Khasimu

K.NY. MKURUGENZI MTENDAJI,

HALMASHAURI YA WILAYA,

KARAGWE.


Kiambatanisho B

Taarifa ya maendeleo ya Vikundi vya vijana na wanawake vilivyokopeshwa mizinga hadi mwezi Juni 2017  


Na.
Jina la kikundi
Namba ya usajiri
Kata 
Kijiji
Jumla ya mizinga 
mizinga yenye nyuki
mizinga isiyo na nyuki
1
UKIWACHO
KDC/CD/CBO/033
Chonyonyo
chonyonyo

25

18

7

2
Twejune
KDC/CD/CBO/082
Nyakahanga
Nyakahanga

25

11

14

3
Nguvu Kazi
KDC/CD/CBO/120
Rugera
Nyarugando

50

38

12

4
Bora Imani
KDC/CD/CBO/173
Igurwa
Kigarama

50

27

23

5
Kimiza Pamoja Group
KDC/CD/CBO/154
Kihanga
Kishoju

50

36

14

6
UMAM
Reg: 233215
Chanika
Mchuba

50

47

3

7
KIWAWAVIKA
KDC/CD/CBO/150
Kituntu
Katwe

50

24

26

8
Umoja Rugera
KDC/CD/CBO/143
Rugera
Rugera

50

4

46

9
KIWAKAKA
KDC/CD/CBO/230
Kihanga
katanda

50

9

41

10
Umoja ni mali
KDC/CD/CBO/428
Igurwa
Bwera

50

30

20

11
Juhudi group
KDC/CD/CBO/420
Chonyonyo
Chonyonyo

50

40

10

12
Faraja
KDC/CD/CBO/136
Nyakahanga
Rwandalo

25

20

5

13
Tuinuane
KDC/CD/CBO/128
Rugu
Rugu

25

16

9

14
Tweyememu
KDC/CD/CBO/275
Kihanga
Nyarwele

25

11

14

15
Mavuno
KDC/CD/CBO/043
Nyakasimbi
Muungano

25

21

4

16
Tuyatunze mazingira
KDC/CD/CBO/696
Ihanda
Ihanda

25

21

4

17
Tuinuane
KDC/CD/CBO/478
Bweranyange
Muguluka

25

22

3

18
Wapendanao
KDC/CD/CBO/190
Ihembe
Ihembe

25

23

2

19
Wanambingu
KDC/CD/CBO/705
Kayanga
Kayanga

25

6

19

20
Tuinuane Rwambaizi
KDC/CD/CBO/189
Kanoni
Rwambaizi

50

13

37

21
Tupendane Kanoni
KDC/CD/CBO/479
Kanoni
Kanoni

50

8

42

22
Rugabo ELCT group
KDC/CD/CBO/510
Rugu
Misha

25

14

11

23
Furaha group
KDC/CD/CBO/288
Kituntu
Kinyinya

25

23

2

24
Mchaka Mchaka
KDC/CD/CBO/703
Nyaishozi
Nyaishozi

25

17

8

25
Umoja Wajasiliamali
KDC/CD/CBO/608
Kayanga
Kayanga

25

5

20

26
Muungano
KDC/CD/CBO/795
Kanoni
Rwambaizi

25

21

4

27
Hosiana A. group
KDC/CD/CBO/850
Ndama
Nyabwegira

25

8

17

28
Mshikamano Group
KDC/CD/CBO/856
Nyaishozi
Nyakayanja

50

30

20


jumla ya mizinga yote



1000

563

437



Kiambatanisho A

Takwimu za mizinga ya nyuki kwa kila kata




S/NO:

Jina la kata

Idadi ya mizinga yenye nyuki

Idadi ya mizinga isiyo na nyuki

Jumla ya mizinga yote

 
mizinga ya kisasa
mizinga ya asili
mizinga ya kisasa
mizinga ya asili
mizinga ya kisasa
mizinga ya asili

1

Nyaishozi

133

123

42

82

175

205

2

Ihembe

54

198

36

132

90

330

3

Nyakasimbi

39

228

12

93

51

321

4

Rugu

52

268

79

370

131

638

5

Nyakabanga

43

52

14

36

57

88

6

Nyakakika

0

22

0

8

0

30

7

Bweranyange

68

2,796

57

789

125

3585

8

Kibondo

5

26

0

28

5

54

9

Nyabiyonza

7

303

3

239

10

542

10

Kiruruma

81

70

26

22

107

92

11

Kamagambo

90

136

20

30

110

166

12

Chonyonyo

74

159

58

51

132

210

13

Ihanda

123

54

24

11

147

65

14

Nyakahanga

89

272

56

166

145

438

15

Bugene

21

55

3

13

24

68

16

Kayanga

96

59

47

14

143

73

17

Rugera

41

338

62

69

103

407

18

Kihanga

352

318

137

112

489

430

19

Kituntu

52

71

35

22

87

93

20

Ndama

23

10

15

78

38

88

21

Chanika

183

269

33

82

216

351

22

Kanoni

63

46

83

44

146

90

23

Igurwa

66

108

40

194

106

302


jumla

1755

5981

882

2685

2637

8666













Matangazo

  • MATOKEO DARASA LA SABA 2022 December 01, 2022
  • WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA SEKONDARI 2023 December 14, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI July 09, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI February 21, 2022
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • ZAWADI

    September 26, 2022
  • WAJERUMANI WASAINI KITABU KWA DED

    September 26, 2022
  • KARAGWE YAPOKEA WAJERUMANI

    September 25, 2022
  • KAMATI YA FEDHA MAFUNZONI

    September 16, 2022
  • Angalia zote

Video

BARAZA LA MADIWANI LAWASIMAMISHA WATUMISHI
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • History
  • Dira na Dhamira
  • Fomu za mbalimbali
  • NEEMA INAKUJA KWA WAKULIMA
  • FEDHA ZILIZOPOKELEWA KWA AJILI YA MFUKO WA JIMBO

Viunganishi vihusishi

  • NECTA
  • UTUMISHI
  • TOVUTI YA TAIFA
  • TAMISEMI
  • FFARS
  • SALARY SLIP

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    KARAGWE KAGERA TANZANIA

    Anuani ya posta: BOX 20 KARAGWE

    Simu: 028-2227148

    Simu ya mkononi: 0754653409

    Barua pepe: ded@karagwedc.go.tz ded.karagwedc@kagera.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright©2017 karagwedc. All rights reserved.