• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
KARAGWE DISTRICT COUNCIL
KARAGWE DISTRICT COUNCIL

United Republic of Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KARAGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na dira
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
        • Sekondari
        • Msingi
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Mazingira na Taka ngumu
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Ufugaji na Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Inayokuja
    • Iliyotekelezwa
    • Inayoendelea
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Taarifa
    • Sheria
    • Mpango mkakati
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha

Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika

Idara ya Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika inaundwa na sehemu tatu (3) ambazo ni:-

  •  Kilimo
  •  Umwagiliaji
  • Ushirika

MAELEZO YA JUMLA KUHUSU SEKTA YA KILIMO WILAYANI KARAGWE.

Kilimo ni mojawapo ya shughuli za kiuchumi  inayochangia  wastani  asilimia 70 ya pato la Halmashauri. Kaya zinazoshiriki katika shughuli za kilimo ni 61,351 kati ya kaya zote 72,178 za wilaya ya Karagwe. Eneo linalofaa kwa kilimo ni hekta 108,000 kati ya hekta 4,500,000 ya eneo lote la wilaya. Eneo linalofaa kwa kilimo cha Umwagiliaji ni hekta 9,920. Pia idara inashirikiana na wadau mbalimbali waliopo wilayani katika kuendeleza sekta ya kilimo. 

Baadhi ya wadau hao wa Kilimo ni K.V.T.C, MAVUNO, CHEMA, WORLD VISION, MATUNDA MEMA, BISHESHE WINW, KARAGWE ESTATE, RADIO KARAGWE, RADIO FADECO, LUKALE WINE, KDCU, KADERES NA OLAM.

 

 LENGO LA IDARA.

Lengo ni kuongeza uzalishaji wa mazao mbalimbali ya biashara na chakula ili kuongeza kipato cha mkulima na kupunguza umasikini.

Idara ya Kilimo, Ushirika na Umwagiliaji inashughulikia masuala ya; Afya za mimea, Ushauri na mafunzo, Uzalishaji wa mazao mbalimbali, Usalama wa mazao ya chakula, lishe na biashara, Biashara ya mazao, Kusimamia vikundi  mbalimbali vya uzalishaji na mikopo kupitia SACCOS.

 

MAJUKUMU YA IDARA

  • SERA, SHERIA NA PROGRAMU ZA KILIMO
  • Kuainisha sera na sheria ndogo kuhusu uendelezaji wa mazao
  • Kuandaa sera za matumizi ya ardhi
  • Kuandaa sheria ndogo za hifadhi ya mazingira
  • Kuandaa programu za uendelezaji mazao
  • MAFUNZO
  • Kuendesha mafunzo kwa wazalishaji na wakaguzi wa mbegu
  • Kuendesha mafunzo kwa wasambazaji pembejeo
  • Kutoa mafunzo ya lishe kwa wakulima
  • Kuelimisha wakulima juu ya matumizi bora ya udongo na maji
  • Kutoa taaluma za uzalishaji wa mboga, matunda, maua na viungo.
  • Kuendesha mafunzo ya wataalamu wa kilimo
  • Kuwafundisha wakulima kutengeneza na kufanya matengenezo ya zana za kilimo
  • Kuandaa mafunzo/ maonesho ya matumizi ya zana za kilimo
  • Kuwafundisha wakulima juu ya ujenzi wa vihenge bora
  • Kuwafundisha wakulima mbinu bora za kilimo, matumizi bora ya mbolea na madawa na pembejeo za kilimo.
  • Kushirikiana na mafundi sanifu katika kufundisha wakulima uendeshaji skimu za Umwagiliaji.
  • Kuandaa programu za mafunzo kwa wakulima kutumia zana za kilimo
  • KUONGEZA UZALISHAJI WA MAZAO MBALIMBALI
  • Kuhamasisha uzalishaji mazao mapya
  • Kusimamia udhibiti wa kuingiza visumbufu vipya vya mazao na mimea
  • Kusimamia udhibiti wa visumbufu vya mazao na mimea
  • Kusimamia/ Kuedeleza uzalishaji wa mbegu bora
  • Kuandaa, kutayarisha na kusambaza mbegu bora
  • Kuhamasisha uanzishaji wa vikundi vya wakulima/wamwagiliaji
  • Kushiriki katika kufundisha wakulima juu ya matumizi bora ya zana za kilimo
  • Kutoa ushauri wa kilimo mseto
  • Kutoa ushauri kwa wakulima kuhusu matumizi bora ya zana za kilimo kwa vitendo
  • Kuhamasisha uzalishaji wa mazao ya bustani
  • UKUSANYAJI , UANDAAJI NA UTUNZAJI WA TAKWIMU NA TAARIFA  MBALIMBALI ZA KILIMO
  • Kutunza benki ya takwimu zinazohusu udongo
  • Kukusanya na kutunza takwimu za bei ya mazao kwa wiki,  mwezi na robo mwaka
  • Kukusanya takwimu za ukusanyaji wa mazao katika masoko, kila wiki na mwezi
  • Kukusanya na kutunza  takwimu  za miradi ya Umwagiliaji
  • Kukusanya takwimu za mvua
  • Kukusanya takwimu za mahitaji, upatikanaji, matumizi, akiba na bei za pembejeo na kuzitoa kwa waagizaji na wawekezaji katika pembejeo.
  • Kukusanya na kutunza takwimu za zana za kilimo
  • Kuandaa/kuandika taarifa za utekelezaji kwa sekta ndogo ya mazao.
  • TAFITI NA TATHIMINI
  • Kutathimini na kusavei maeneo ya vyanzo vya maji
  • Kupima uotaji wa mbegu na kusimamia taratibu za ukaguzi
  • Kufanya ukaguzi wa ubora wa matumizi ya pembejeo na zana
  • Kufanya ukaguzi wa mbegu mpya, kwa kushirikia na utafiti wa mbegu kabla ya kupitishwa.
  • Kufanya utafiti mdogo mdogo wa mazao yanayofaa kulimwa katika sehemu ya kilimo cha Umwagiliaji
  • Kufanya vipimo vya ubora, unyevu unyevu na utoaji wa mbegu
  • Kuendesha na kusimamia vishamba vya majaribio vya mbegu na ukaguzi maabara ili kuondoa utata juu ya mbegu.
  • Kufanya majaribio ya magonjwa kwenye mbegu
  • Kushiriki katika savei za kilimo
  • SHUGHULI NYINGINE ZA IDARA
  • Kusoma na kutafsiri ramani
  • Kujibu maswali, hoja na ahadi za bunge
  • Kutayarisha na kuzipitia ramani za kijiji
  • Kupanga  mipango ya uzalishaji
  • Kuandaa mipango na bajeti za sekta ya mazao
  • Kusimamia/Kuhamasisha na kuhimiza uwekezaji katika sekta ya kilimo
  • Kuwatambua wasambazaji wa pembejeo
  • Kushiriki kutengeneza michoro/ ramani za Umwagiliaji.
  • Kushiki katika ujenzi wa miradi ya Umwagiliaji
  • Kufanya kazi nyingine za fani yako kama utakavyoagizwa na mkuu wako wa kazi.
    •     
  •        CHANGAMOTO ZINAZOJITOKEZA KATIKA IDARA YA KILIMO.
  • Mabadiliko ya tabia nchi.
    • Mabadiliko ya hali ya hewa yanasababisha misimu ya unyeshaji wa mvua kubadilika na hivyo kusababisha uzalishaji mashambani kuwa wa kubahatisha.
  • Magonjwa ya mimea kama vile ugonjwa wa Unyanjano, Ugonjwa wa batobato kali n.k
  • Wakulima kutokuwa na desturi ya kuhifadhi chakula kinachokaa kwa muda mrefu.
  • Wakulima kutokutumia teknolojia za kisasa ikiwemo matumizi ya mbegu bora.
  • Wakulima kutozingatia matumizi ya kanuni bora za kilimo
  • Migogoro ya wakulima na wafugaji
  •        MIKAKATI YA KUJITOSHELEZA KWA CHAKULA


    • Kusimamia utekelezaji wa sheria  ya ugonjwa wa mnyauko wa migomba.
    • Kuhimiza kilimo cha mazao yanayostahimili ukame ambayo ni viazi vitamu, mihogo, viazi mviringo, mtama, kuongeza uzalishaji wa mahindi.
    • Halmashauri imeweka mkakati wa kusisitiza matumizi na utunzaji bora wa chakula ili kukabili ipasavyo  upungufu wa chakula unaoweza kujitokeza
    • Idara imeandaa mikakati ya kilimo cha mahindi, maharage, kahawa na alizeti ili kuinua kipato cha mkulima.
      • Shughuli zinazotekelezwa chini ya mnyororo wa thamani.
    • Uundwaji wa vikundi vitatu  vya mashamba darasa vya mnyororo wa thamani
    • Uanzishwaji wa Vitalu 3 vya miche ya kahawa.
    • Utoaji wa mafunzo kwa wakulima katika vijiji vyote 3 na jumla ya wakulima 300 wamepata mafunzo hayo.
    • Ziara za mafunzo kwa wakulima katika chuo cha utafiti MARUKU kuhusiana na uzalishaji bora wa zao la kahawa zimefanyika.
       

TAARIFA YA MWAKA 2016/2017 IDARA YA KILIMO, UMWAGILIAJI NA USHIRIKA

Husika na somo tajwa hapo juu.

Ifuatayo ni taarifa ya Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika kwa mwaka 2016/2017.

  • Utangulizi
  • Idara ya kilimo ni moja ya Idara zilizo chini ya Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe ambayo inafanya kazi zake kwa mujibu wa sheria, taratibu na kanuni za nchi. Idara ya kilimo ina vitengo vikuu vitatu ambavyo ni Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika.
  • Watumishi waliopo na mgawanyo wake
  • Idara ina jumla ya watumishi 62, ambao wamegawanyika katika vitengo vyote vitatu;
  • Kitengo cha kilimo kina watumishi 56 kati ya  110 wanaohitajika
  • Kitengo cha Umwagiliaji kina watumishi 4 kati ya 6  wanaohitaji
  • Kitengo cha Ushirika kina watumishi 2 kati ya 6 wanaohitajika
  • Hata hivyo Halmashauri iliomba kwenye bajeti ya 2017/2018 kuongezewa watumishi 25 kwa ajili kuziba baadhi ya nafasi.
  • Kitengo cha Kilimo na Umwagiliaji.
  • Miradi ya maendeleo
  • Kwa mwaka wa fedha 2016/2017 Idara imetekeleza mradi mmoja tu wa Umwagiliaji wa Mwisa awamu ya pili ambao pesa zake zilipokelewa mwaka wa fedha 2015/2016.
  • Hatua za Utekelezaji wa mradi;
  • Halmashauri ya Wilaya ilifanya mchakato wa kumpata Mkandarasi ambaye ni Grinda Builders and Supplies LTD na mkandarasi alianza ujenzi tar 23 mwezi wa kwanza mwaka 2017 mpaka tar 23 mwezi wa nne kwa mujibu wa mkataba wenye kumb no.LGA/033/2016/2017/C/NT/01 wenye thamani ya Tsh 177,664,003.70/=kutokana na mvua kunyesha sana mkandarasi aliomba kuongezewa mda mpaka tar 23 mwezi wa sita 2017 ndo akakamilisha ujenzi.
  • Baada ya kuona baadhi ya kazi ambazo zipo kwenye mkataba na baada ya kufanya ukaguzi kiuhalisia(scheme audit) tulibaini baadhi ya kazi kama vipunguza kasi(drop structure) zipatazo 12 zilitolewa kulingana na geography, pia Tsh 6,000,000/= ilibaki kwenye akaunti ya kamati ya ujenzi Mwisa.
  • Hivyo hela yote ambayo imebaki ni Tsh 19,978,026.72/=. Fedha hiyo imeombewa kazi ya nyongeza ambapo kazi ilitakiwa ifanyike kwa wiki 2 kuanzia tarehe 24/06/2017 hadi 8/7/2017.
  •  Hivyo Mkandarasi amekamilisha kazi yote ya ujenzi wa mradi mpaka sasa kwa asilimia 98 kulingana na mkataba.


  • Changamoto ambazo zipo kwenye mradi wa Umwagiliaji;
  • Wamiliki wa mashamba kwenye mradi ni wananchi binafsi.
  • Ukandishaji wa mashamba sehemu ambazo miundo mbinu ya Umwagiliaji imefika na maji yanafika.
  • Mifereji mikuu na midogo haifanyiwi usafi vizuri.
  • Watu wenye mashamba kwenye mradi hawataki kulima pia hata kuwakodishia watu wengine hawataki hivyo hata kufanya usafi kwenye mitaro inakuwa shida

         Mapendekezo/ushauri;

  • Wale wenye mashamba wapewe msukumo waweze kulima mashamba yao haraka, kama hawawezi wawe tayari kuwagawia watu ambao wako tayari kulima.
  • Shughuli kuu zilizotekelezwa kwa kipindi cha mwaka 2016/2017
  • Idara kupitia maafisa Ugani wake imetoa elimu kwa wakulima kulima kwa kufuata kanuni za kilimo bora katika mazao mbalimbali.
  • Idara ilisimamia shughuli za Usambazaji wa pembejeo za ruzuku ikiwemo mbegu za mahindi pamoja na mbolea
  • Imeandaa taarifa za mwezi, robo na mwaka za ARDS (Agriculture Routine Data System) na kuziwasilisha zinakotakiwa.
  • Imeandaa taarifa za Robo na Mwaka za ASDP (Agriculture Sector Development Program).
  • Imefanya vikao vya Idara vya kila mwezi
  • Idara imehudhuria vikao vya kisheria vya Halmashauri
  • Idara pia imeshiriki ukaguzi wa miradi ya maendeleo ya Halmashauri
  • Imeshiri kugawa mbegu bora za viazi lishe kwa baadhi ya wakulima kwa ajili ya kuzalisha mbegu.
  • Idara iligawa mahindi ya msaada wakati wa janga lilotokea kutokana na ukame.
  • Idara pia imeshirikiana na wadau wa sekta binafisi katika shughuli za maendeleo ya kilimo. Sekta hizo binafisi ni kama KADERES, Mavuno, KDCU, TCRS, TIA, OLAM, World Vision n.k
  • Idara pia kupitia watalaam wake wameshiriki semina mbalimbali kama vile ARDS, ASDPII,Kahawa pamoja na mabadiliko ya tabia ya nchi.
  • Idara pia iligawa miche ya kahawa kwa baadhi ya wakulima

Kilimo cha kahawa

Kahawa ni zao kuu la kibiashara kwa wilaya ya Karagwe na ndilo linaloingizia mapato makubwa halmashauri. Mwaka huu wa fedha halmashauri iliwasaidia wakulima kuwanunulia miche ya kahawa. Lengo kuu ilikuwa ni kufidia mibuni iliyokauka na kuongeza kiasi cha mibuni. Jumla ya miche 115,000 ilinunuliliwa na kugawiwa kwa wakulima 2,300 wa Kahawa katika vijiji 36 mbalimbali hasa vile vilivyokuwa vimeathirika sana na ukame. Shughuli hiyo iligharimu jumla ya Tsh.34,500,000/=

Miche hiyo ilinunuliwa kwa vikundi vya wakulima binafsi vilivyoko hapa wilayani. Hata hivyo vikundi hivyo bado havijalipwa kiasi chochote. Halmashauri inatakiwa ivilipe vikundi hivyo kwa mchanganuo ufuatao.

  • Hekima Farmers group …………………………......Tsh.2,382,000/=
  • Uboreshaji wa zao la Kahawa Ihembe II …...Tsh.1,497,600/=
  • TWEYAMBE (Katwe)…………………………………….…Tsh.3,296,700/=
  • VIJANA KAKULAIJO (Kalupoa)………………….....Tsh.3,905,100/=
  • TACRI Kishoju………………………………………………….Tsh.3,900,000/=
  • KIKUNDI CHAA BUSTANI YA KAHAWA – BAKARUKA.…4,290.000/=
  • TWENDE NA WAKTI GROUP –ukale…………………Tsh. 569,100/=

                             JUMLA…………………………………………..Tsh.19,579.500/=

Hili ndilo deni ambalo Halmashauri inadaiwa na vikundi vya wakulima wa vitalu vya miche ya Kahawa.

Mafanikio; 

Kwa mwaka huu wa fedha tulilenga kukusanya tani 12,000 za Kahawa ya maganda na tukafanikiwa kukusanya tani 9,868 sawa na 82%. Kiasi hicho cha Kahawa kilinunuliwa na makampuni 6 binafisi yaliyoruhusiwa kununua Kahawa wilaya ya Karagwe pamoja na Chama kikuu cha Ushirika KDCU. Makampuni hayo yalinunua kati ya tani1, 200 hadi 1,600 za Kahawa ya maganda

 

 

Changamoto katika uzalishaji wa Kahawa

  • Bei kubwa ya miche ya Kahawa ambayo inamfanya mkulima ashindwe kununua na hivyo kupanda miche ambayo haikuzalishwa kitaalamu.
  • Bei ya Kahawa kutokuwa imara. Hii inatokakana na kuyumba kwa soko la Kahawa la kimataifa.

Changamoto Katika Kitengo cha Kilimo na Umwagiliaji

Katika kitengo cha kilimo na Umwagiliaji kuna changa moto mbalimbali zilizojitokeza na kusababisha baadhi ya shughuli kutokutekelezwa kikamilifu. Changamoto hizo ni:

  • Upungufu wa Maafisa Ugani wa vijiji na kata kwa ajili ya kutoa elimu kwa wakulima ili kuongeza tija katika uzalishaji.
  • Upungufu wa vyombo vya usafiri hasa pikipiki kwa Maafisa Ugani kwa ajili ya kuwafikia wakulima kwa urahisi.
  • Ukosefu wa mafuta kwa maafisa ugani walio na pikipiki kwa ajili ya kuwafikia wakulima.
  • Ukosefu wa Shajara kwa ajili ya kutunza kumbukumbu pamoja na kutolea taarifa mbalimbali.
  • Ukosefu wa fedha kwa ajili ya kuendesha Idara,Kutoa mafunzo kwa maafisa Ugani kwa ajili ya kuwajengea uwezo ili kuendana na teknolojia iliyopo pamoja na kulipa stahiki za watumishi wa Idara, zikiwamo nauli za rikizo pamoja na posho pale wanapofanya kazi za ziada.
  • Kitengo cha ushirika
  • Katika kitengo cha Ushirika kuna jumla ya vyama vya ushirika 74 kikiwemo chama kikuu cha ushirika KDCU.
  • Kuna vyama vya msingi 39
  • SACCOS 32
  • Ushirika aina nyingine ni 1.
  • Aidha katika kitengo hiki kuna shughuli mbalimbali zilizofanyika kwa kipindi cha mwaka mzima. Shughuli hizo ni:
  • Ukaguzi wa ndani kwa vyama vinne vya TUWAKA +Ltd, Karagwe watumishi, Chakanya Ltd na Chaifo Ltd.
  • Mikutano mikuu ya maksio kwa SACCOS 19
  • Mikutano mikuu ya vyama vya msingi 37 na chama cha Ushirika KDCU.
  • Mafunzo kwa vyama vya Ushirika 4 chini ya mradi wa MIVARF kupitia Banki ya Wakulima ya Ushirika.
  • Mafunzo kwa vyama vya Ushirika vya msingi 33 juu ya marekebisho ya masharti ya vyama vya msingi kwa kufuata sheria mpya no.6 ya mwaka 2013 kupitia mradi wa KDCU wa kilimo hai.
  • Uhamasishaji wa elimu ya Ushirika katika vikundi mbalimbali vya wakulima na wafugaji.
  • Kuviandikia barua vyama vilivyopendekezwa kufutwa na Mrajisi wa vyama vya Ushirika.

Changamoto katika Kitengo cha Ushirika.

Katika kitengo hiki kuna changamoto mbalimbali ambazo zimejitokeza na bado zinakikabili

  • Upungufu wa maafisa Ushirika wa kusimamia vyama vya Ushirika, kwa kuwa wilaya nzima ina maafisa Ushirika 2 tu. Lakini anayefanya kazi za Ushirika ni mmoja, mwingine anafanya kazi za TASAF.
  • Ukosefu wa fedha kwa ajili ya kusimamia shughuli za Ushirika kikamilifu.
  • Ukosefu wa vitendea kazi kwa watalaamu wa Ushirika.
  • Shughuli zinazotarajiwa kufanyika mwaka 2017/2017
  • Kuendelea kutoa elimu kwa wakulima kulima kwa kufuata kanuni za kilimo bora, ikiwamo namna ya kudhibiti magonjwa na wadudu wa mimea, kulima mazao ya kinga ya njaa.
  • Kuhamasisha kilimo cha Umwagiliaji kwenye mradi wa Mwisa
  • Kuendelea kusaidia wakulima upatikanaji wa mbegu bora kama vile miche ya kahawa, mazao ya kinga ya njaa (malando, mihogo mtama mweupe n.k)
  • Kuendelea kushirikiana na wadau mbalimbali wa sekta binafsi katika shughuli za maendeleo ya kilimo.
  • Kwa taarifa hii naomba kuwasilisha

Martine, J.L.Nsongoma

Kaimu Mkuu wa idara ya Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika

Halmashauri ya Wilaya

KARAGWE



Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO YA ASILIMI 10 October 04, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI KADA YA DEREVA II NA WAANDISHI WAENDESHA OFISI II September 30, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI WASAIDIZI KUMBUKUMBU DARAJA LA II NA MTENDAJI WA KIJIJI WA III October 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI February 21, 2022
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KAMATI YA LISHE YAKETI KUJADILI UTEKELEZAJI WA AFUA ZA LISHE, KIPINDI CHA ROBO YA TATU 2024/2025.

    April 22, 2025
  • KUELEKEA MSIMU WA KAHAWA 2025/2026: MAAFISA UGANI KARAGWE DC WAPEWA MAFUNZO ILI KUWASAIDIA WANANCHI KUONGEZA THAMANI YA ZAO HILO.

    April 11, 2025
  • WALENGWA WA TASAF KARAGWE DC WANUFAIKA NA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA KIFEDHA WALIZOANZISHA.

    March 17, 2025
  • DC LAIZER AWATAKA WANAWAKE WA KARAGWE KUJIIMARISHA KIUCHUMI.

    March 08, 2025
  • Angalia zote

Video

SHIRIKI UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 KARAGWE TUMEJIPANGA
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • History
  • Dira na Dhamira
  • Fomu za mbalimbali
  • NEEMA INAKUJA KWA WAKULIMA
  • FEDHA ZILIZOPOKELEWA KWA AJILI YA MFUKO WA JIMBO

Viunganishi vihusishi

  • NECTA
  • UTUMISHI
  • TOVUTI YA TAIFA
  • TAMISEMI
  • FFARS
  • SALARY SLIP

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    KARAGWE KAGERA TANZANIA

    Anuani ya posta: BOX 20 KARAGWE

    Simu: 028-2227148

    Simu ya mkononi: 028-2227148

    Barua pepe: ded@karagwedc.go.tz ded.karagwedc@kagera.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright©2017 karagwedc. All rights reserved.