• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
KARAGWE DISTRICT COUNCIL
KARAGWE DISTRICT COUNCIL

United Republic of Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KARAGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na dira
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
        • Sekondari
        • Msingi
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Mazingira na Taka ngumu
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Ufugaji na Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Inayokuja
    • Iliyotekelezwa
    • Inayoendelea
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Taarifa
    • Sheria
    • Mpango mkakati
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha

WATUMISHI KARAGWE DC WAMSHUKURU DED KWA KUWEZESHA MAFUNZO YA AFYA YA AKILI.

Imewekwa: September 19th, 2025

WATUMISHI KARAGWE DC WAMSHUKURU DED KWA KUWEZESHA MAFUNZO YA AFYA YA AKILI.

Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe wamemshukuru Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo Bi.Happiness Msanga kwa kuwezesha Mafunzo ya Afya ya Akili  kwa Watumishi ambayo yamewasaidia kuboresha afya zao za akili pamoja kuwapa uwezo kukabiliana na changamoto zao kwa utashi bila kuleta madhara.

 Mafunzo haya yamefanyika  kwa siku tano mfululizo  kuanzia Septemba 14 hadi 18, 2025 kwenye Tarafa zote 5 za Wilaya ya Karagwe ambazo ni Bugene, Nyakakika, Nyaishozi, Kituntu na Nyabiyonza kuhakikisha Watumishi wote 2700 wa Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe  wanapata Elimu hiyo iliyowasilishwa na Mkufunzi  wa Afya ya akili kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili Dkt.Garvin Kweka.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti  tofauti za Mafunzo, Watumishi hao wamemshukuru Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Karagwe Bi.Happiness Msanga kuhakikisha  elimu hiyo inawafikia Watumishi wengi hadi waliopo vijiji vya mbali na makao makuu wanaamini elimu waliyopata itawasaidia kuweka usawa kwenye kazi  na maisha yao (work & life balance).

Akizungumza kwa niaba ya Watumishi waliohudhuria mafunzo hayo katika Tarafa ya Bugene, Mtendaji wa kijiji cha Nyarugando Bw. Athanas Mapombe amesema mafunzo  hayo yatamsaidia kujenga mahusiano mazuri kazini ikiwemo kusaidiana endapo ataona dalili za uwepo wa tatizo la afya ya akili kwa mtumishi mwenzie  pia ameomba , kuwepo na semina kama hizo kila inapotokea fursa ili kujengeana uwezo zaidi katika mazingira ya kazi.

Naye, Mwalimu Grace Shibundulila wa shule ya msingi Bujara aliyehudhuria mafunzo hayo Tarafa ya Nyaishozi amesema mafunzo haya yatamsaidia kwenye kufanya maamuzi sahihi anapokua na msongo wa mawazo na kuweka usawa kwenye kutekeleza majukumu yake ya kazini na nyumbani.

Aidha, Mafunzo hayo yalitolewa pia kwa Vyombo vya Usalama Wilaya ya Karagwe, Wanafunzi wa Kidato cha Sita Shule ya Sekondari Bugene pamoja na Wananchi wa Wilaya ya Karagwe ambao Walikutana kwenye Ukumbi wa chuo cha VETA Wilayani humo.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI September 19, 2025
  • TANGAZO KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA KARAGWE September 02, 2025
  • TANGAZO LA KITWA KWENYE USAILI WA MAHOJIANO September 17, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO YA ASILIMI 10 October 04, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • DED MSANGA AKAGUA NA KUTEMBELEA MIRADI MBALIMBALI YA MAENDELEO

    September 29, 2025
  • WATUMISHI KARAGWE DC WAMSHUKURU DED KWA KUWEZESHA MAFUNZO YA AFYA YA AKILI.

    September 19, 2025
  • UFAULU WA ASILIMIA 100 WAWAPELEKA WALIMU WA KIDATO CHA TANO NA SITA HIFADHI YA TAIFA YA NGORONGORO.

    August 11, 2025
  • DC LAIZER AMALIZA MGOGORO WA ARDHI ULIODUMU KWA MIAKA 10

    July 23, 2025
  • Angalia zote

Video

ZIARA YA WALIMU KATIKA HIFADHI YA TAIFA NGORONGORO
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • History
  • Dira na Dhamira
  • Fomu za mbalimbali
  • NEEMA INAKUJA KWA WAKULIMA
  • FEDHA ZILIZOPOKELEWA KWA AJILI YA MFUKO WA JIMBO

Viunganishi vihusishi

  • NECTA
  • UTUMISHI
  • TOVUTI YA TAIFA
  • TAMISEMI
  • FFARS
  • SALARY SLIP

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    KARAGWE KAGERA TANZANIA

    Anuani ya posta: BOX 20 KARAGWE

    Simu: 028-2227148

    Simu ya mkononi: 028-2227148

    Barua pepe: ded@karagwedc.go.tz ded.karagwedc@kagera.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright©2017 karagwedc. All rights reserved.