• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
KARAGWE DISTRICT COUNCIL
KARAGWE DISTRICT COUNCIL

United Republic of Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KARAGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na dira
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
        • Sekondari
        • Msingi
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Mazingira na Taka ngumu
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Ufugaji na Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Inayokuja
    • Iliyotekelezwa
    • Inayoendelea
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Taarifa
    • Sheria
    • Mpango mkakati
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha

YALIYOJIRI MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI APRILI 28-29, 2021.

Imewekwa: April 30th, 2021

Na Innocent E. Mwalo.

Baraza la Madiwani la Halmashauri ya wilaya, kupitia Mkutano wake wa robo ya tatu iliyoanzia Januari mpaka Machi, 2021, uliofanyika katika Ukumbi wa Vijana Rafiki wa Angaza mnamo Aprili 28/29, umeagiza na kushauri mambo kadhaa yanapaswa kutekelezwa katika Halmashauri hii ili kuongeza tija ya kuwahudumia wananchi wa Karagwe.

Katika hotuba yake ya ufunguzi,  Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya, Mh. Wallace Mashanda, licha ya kupongeza jitihada zilizofikiwa na Halmashauri katika suala nzima la ukusanyaji wa mapato ya ndani ambapo hadi kufikia robo tatu ya mwaka wa fedha 2020/2021,  mwezi Machi, Halmashauri ya Wilaya imeshakusanya mapato hadi kufikia asilimia 88.

Mh. Mashanda aliiasa menejimenti kutokubweteka na mafanikio  hayo na alitoa angalizo la kwamba pamoja na mafanikio yaliyofikiwa katika kukusanya mapato,  huenda Halmashauri haikukadiria ipasavyo kutokana na wingi wa vyanzo vya mapato ya ndani katika Halmashauri  hii.

Aidha kupitia mkutano huo, Mh. Mashanda aliwajulisha wananchi wa Karagwe ya kwamba kwa kipindi cha kuanzia Julai 2020 mpaka Machi 2021 tayari Halmashauri ya Wilaya imepokea kiasi cha takribani bilioni 4.12 ikiwa ni fedha kutoka serikali kuu na wafadhili mbalimbali kwa ajili ya kufadhili shughuli mbalimbali ikiwemo Elimu bure na chakulani mashuleni, fedha za mradi wa TASAF, maboma ya shule ya msingi na miradi mingine zaidi ya 20 ya maendeleo.

Mkutano huu uliotawaliwa na mjadala mkali kutoka kwa wajumbe wa baraza la madiwani hasa katika utelezaji wa maazimio ya mkutano uliopita ambao ulifanyika mwezi Januari mwaka huu.

Katika mkutano huu, wajumbe kwa mara nyingine tena, baada ya hoja iliyoibuliwa na Mh. Maginus Cheusi ambaye ni Diwani wa Kata ya Kibondo,  waliazimia juu ya kuhamasishwa kwa akina mama wajawazito ili waweze kuwa na bima ya afya itakayowawezesha kuwa na uhahika wa matibabu ikilinganishwa na ilivyo sasa ambapo wanawake wengi wanapata vikwazo wakati wa kujifungua  kutokana na tatizo la ukosefu wa fedha za kulipia huduma hizo kwa malipo ya tele kwa tele.

Katika hatua nyingine waheshimiwa  madiwani kupitia baraza hili waliagiza kutokujitokeza tena kwenye taarifa zinazowasilishwa na kamati za maendeleo ya kata juu ya ukosefu wa uji na chakula cha mchana mashuleni  kutokana na wilaya hii kuelekea kwenye  msimu wa mavuno ambapo hakutakuwa na kisingizio cha ukosefuwa mahindi yakuchangia  huduma hiyo muhimu kwa  wanafunzi hao.

Aidha ili kuipa uzito agenda ya lishe na afya kwa ujumla wajumbe waliendelea kusikitishwa na ongezeko wa watoto wenye utapiamlo na kuagiza takwimu za kliniki kwa watoto wa umri wa chini ya miaka mitano kuwasilishwa katika kila kikao cha kijiji, kamati za maendeleo ya kata pamoja na mikutano mingine inayofanyika katika ngazi ya wilaya ikiwemo mkutano wa baraza la madiwani ili kuipa nguvu ajenda hiyo muhimu kupitia vikao vya maamuzi.

Kupitia mkutano huu wajumbe walienda kusisitiza juu ya kutekelezwa kwa maazimio kadhaa  ya mkutano uliopita ambapo  pamoja na mambo mengine baraza liliazmia kuwa vituo vya kutolea huduma ya afya yaani zahanati,  vituo vya afya na hospitali kutoa huduma za afya kwa masaa yote 24 bila kuwepo na kisingizio chochote. 

Katika hatua nyingine wajumbe walionekana kutolikuridhishwa na namna menejimenti ilivyotekeleza azimio la kuhamasisha jamii juu ya kujiunga na bima ya afya iliyoboreshwa ambapo wajumbe waliazimia uboreshwaji wa huduma hiyo kwenye ngazi ya kata na vijiji. 

Mjadala mwingine mkali katika mkutano huu, ulihusu marejesho ya mikopo ambayo hutolewa kwa vikundi vya wanawake, vijana na wenye ulemavu  ambapo madiwani waliendelea  kushikilia azimio lao lilipitishwa kwenye mkutano wa baraza la Januari 2021  ambapo iliazimiwa kuwa kata  zenye madeni madeni makubwa ya mikopo ya kuanzia milioni kumi ambayo haijareshwa,   ikiwemo kata ya Kayanga  ambayo  inadaiwa jumla ya milioni  47 kutokupewa tena mikopo hiyo.

Katika hatua nyingine mkutano wa baraza la madiwani uliipokea na kuipongeza timu ya Nyaishozi FM ya wilayani hapa ambayo imefuzu kuingia ligi ngazi ya daraja la pili kwenye mashindano yaliyofanyikia   mkoani Lindi ambapo mabingwa hawa ni wawakilishi pekee wa mkoa wa Kagera.

Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO YA ASILIMI 10 October 04, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI KADA YA DEREVA II NA WAANDISHI WAENDESHA OFISI II September 30, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI WASAIDIZI KUMBUKUMBU DARAJA LA II NA MTENDAJI WA KIJIJI WA III October 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI February 21, 2022
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KAMATI YA LISHE YAKETI KUJADILI UTEKELEZAJI WA AFUA ZA LISHE, KIPINDI CHA ROBO YA TATU 2024/2025.

    April 22, 2025
  • KUELEKEA MSIMU WA KAHAWA 2025/2026: MAAFISA UGANI KARAGWE DC WAPEWA MAFUNZO ILI KUWASAIDIA WANANCHI KUONGEZA THAMANI YA ZAO HILO.

    April 11, 2025
  • WALENGWA WA TASAF KARAGWE DC WANUFAIKA NA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA KIFEDHA WALIZOANZISHA.

    March 17, 2025
  • DC LAIZER AWATAKA WANAWAKE WA KARAGWE KUJIIMARISHA KIUCHUMI.

    March 08, 2025
  • Angalia zote

Video

SHIRIKI UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 KARAGWE TUMEJIPANGA
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • History
  • Dira na Dhamira
  • Fomu za mbalimbali
  • NEEMA INAKUJA KWA WAKULIMA
  • FEDHA ZILIZOPOKELEWA KWA AJILI YA MFUKO WA JIMBO

Viunganishi vihusishi

  • NECTA
  • UTUMISHI
  • TOVUTI YA TAIFA
  • TAMISEMI
  • FFARS
  • SALARY SLIP

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    KARAGWE KAGERA TANZANIA

    Anuani ya posta: BOX 20 KARAGWE

    Simu: 028-2227148

    Simu ya mkononi: 028-2227148

    Barua pepe: ded@karagwedc.go.tz ded.karagwedc@kagera.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright©2017 karagwedc. All rights reserved.