• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
KARAGWE DISTRICT COUNCIL
KARAGWE DISTRICT COUNCIL

United Republic of Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KARAGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na dira
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
        • Sekondari
        • Msingi
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Mazingira na Taka ngumu
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Ufugaji na Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Inayokuja
    • Iliyotekelezwa
    • Inayoendelea
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Taarifa
    • Sheria
    • Mpango mkakati
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha

YALIYOJIRI KATIKA SIKU YA KWANZA YA KIKAO CHA BARAZA LA MADIWANI.

Imewekwa: May 17th, 2018

YALIYOJIRI KIKAO CHA BARAZA LA MADIWANI

Na Innocent E. Mwalo, KARAGWE

Baraza la Madiwani Wilayani hapa, linaendelea na kikao chake cha kawaida kwa robo ya tatu ya mwaka wa Fedha 2017/2018, kikao ambacho kinafanyikia katika ukumbi wa Angaza uliopo mjini Kayanga huku kikitarajiwa kudumu kwa takribani  wa siku mbili kikiangazia masuala kadhaa wa kadhaa yahusuyo ustawi wa watu wa Karagwe.

Katika siku ya kwanza masuala kadhaa yaliyadiliwa ambapo hapo awali, Mwenyekiti wa Baraza la Madiwani, Mh. Wallace Mashanda, katika ufunguzi wa Baraza hilo, aliipongeza Timu ya Menejimenti chini ya Uongozi wa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashahuri, Mh.Godwin Kitonka kwa kupata hati safi huku akibainisha ya kwamba jambo hilo limefanikiwa kutokana na ushirikiano mkubwa uliofanywa kati ya timu ya menejimenti na Baraza la Madiwani kwa ujumla kupitia kamati zake za kudumu.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri, Mh. Kitonka mapema akimkaribisha Mwenyekiti wa Halmashauri, aliwaeleza wajumbe wa kikao hicho na wageni waalika pamoja na mambo mengine juu ya kufanya tahadhali ya kuzuia ugonjwa wa Ebola ambao umezuka katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, DRC na kwa mujibu wa taatifa za vyombo vya habari inasemekana ugonjwa huo ulikwisha ua takribani watu 21 huko DRC.

“Ugonjwa huu una dalili nyingi lakini zilizo kubwa ni kwamba mgonjwa hupata homa kali ghafla na pia mgonjwa huharisha na kutapika sana”, alisisitiza Mh. Kitonka.

Katika hatua nyingine, kikao hicho kwa kauli moja kilitoa tamko la kudhibiti moto kutokana na musimu wa kiangazi kukaribia huku kwa mara nyingine kikao hicho kikitoa maagizo kwa wananchi kuanza maandalizi ya awali ya kilimo cha mazao ya biashara.

Jambo jingine ambalo lilijitokeza kwenye kikao hicho lilikuwa ni suala la  simu akaunti ambao ni  mfumo wa kielekroniki utakaotumiwa katika kufanya malipo kwa wakulima wa zao la kahawa ambapo Mratibu wa Mfumo huu kutoka Chama cha Ushirika cha Karagwe, KDCU, Casius Rugemarila aliweza kuwaelezea wajumbe wa kikao hicho juu ya mfumo huo.

Nao wajumbe wa kikao hicho, pamoja na kuunga mkono mfumo huo kuwa mzuri, wito ulitolewa kwa KDCU kuendelea kutafari juu ya kuendelea pia na mfumo wa malipo ya wa papo kwa papo kwani kwa hali halisi sio wakulima wote wanaweza kutumia simu katika shughuli za malipo hayo. Na katika suala hili ilisisitizwa ya kwamba, Halmashauri inao wajibu wa kusimamia kilimo cha kahawa ikiwemo kuratibu uanzishwaji wa vyama vya ushirika.

Katika kujadili taarifa za Mabaraza ya Kata, WDC, wajumbe waliibua masuala kadhaa ambayo ni changamoto kwenye maeneo yao ikiwemo suala la upungufu wa watumishi katika kada za afya na utawala. Ilifafanuliwa ya kwamba kwa sasa serikali imetangaza takribani nafasi 6,000 kwa watumishi wa kada ya afya na mara watakapoajiriwa watumishi hao kipaumbele cha maeneo ambapo kuna upungufu wa watoa huduma hao kitazingatiwa.

Jambo jingine lililojadiliwa kwa msisitizo lilikuwa ni suala la gugu karoti ambao ni mmea unaotajwa kuharibu sana mazao ambapo iliagizwa ya kwamba wananchi wachukue tahadhali ya kung’oa na kuchoma moto gugu hilo pindi mmea unapoonekana kuathiriwa na gugu hilo ili mmea huo usiendelea kuleta madhara kwa mimea mingine iliyo karibu nao.

Aidha masuala mengine yaliyopewa nafasi ya kujadiliwa ilikuwa ni suala la utambuzi wa wazee kwa ajili ya matibabu, agizo kwa wananchi wote juu ya ujenzi na matumizi bora ya ardhi ili kuepuka kukumbana na faini zitakazotozwa kwa wale watakaokaidi agizo hilo.

Katika kikao hicho wajumbe kwa kauli moja waliiomba Wakala wa Barabara, Mjini na Vijijini, TARURA kurejesha miundombinu ya barabara iliyoharibiwa vibaya kutokana na mvua kwenye maeneo yao.

Katika kuhitimisha kikao kwa siku ya kwanza Mh. Wallace Mashanda alitoa wito kwa waheshimiwa madiwani kuwasilisha kwake maandiko kama wakifanikiwa kuandika juu ya namna yeyote ile ya kuboresha ustawi wa wananchi wa Karagwe.

 

Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO YA ASILIMI 10 October 04, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI KADA YA DEREVA II NA WAANDISHI WAENDESHA OFISI II September 30, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI WASAIDIZI KUMBUKUMBU DARAJA LA II NA MTENDAJI WA KIJIJI WA III October 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI February 21, 2022
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KAMATI YA LISHE YAKETI KUJADILI UTEKELEZAJI WA AFUA ZA LISHE, KIPINDI CHA ROBO YA TATU 2024/2025.

    April 22, 2025
  • KUELEKEA MSIMU WA KAHAWA 2025/2026: MAAFISA UGANI KARAGWE DC WAPEWA MAFUNZO ILI KUWASAIDIA WANANCHI KUONGEZA THAMANI YA ZAO HILO.

    April 11, 2025
  • WALENGWA WA TASAF KARAGWE DC WANUFAIKA NA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA KIFEDHA WALIZOANZISHA.

    March 17, 2025
  • DC LAIZER AWATAKA WANAWAKE WA KARAGWE KUJIIMARISHA KIUCHUMI.

    March 08, 2025
  • Angalia zote

Video

SHIRIKI UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 KARAGWE TUMEJIPANGA
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • History
  • Dira na Dhamira
  • Fomu za mbalimbali
  • NEEMA INAKUJA KWA WAKULIMA
  • FEDHA ZILIZOPOKELEWA KWA AJILI YA MFUKO WA JIMBO

Viunganishi vihusishi

  • NECTA
  • UTUMISHI
  • TOVUTI YA TAIFA
  • TAMISEMI
  • FFARS
  • SALARY SLIP

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    KARAGWE KAGERA TANZANIA

    Anuani ya posta: BOX 20 KARAGWE

    Simu: 028-2227148

    Simu ya mkononi: 028-2227148

    Barua pepe: ded@karagwedc.go.tz ded.karagwedc@kagera.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright©2017 karagwedc. All rights reserved.