• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
KARAGWE DISTRICT COUNCIL
KARAGWE DISTRICT COUNCIL

United Republic of Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KARAGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na dira
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
        • Sekondari
        • Msingi
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Mazingira na Taka ngumu
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Ufugaji na Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Inayokuja
    • Iliyotekelezwa
    • Inayoendelea
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Taarifa
    • Sheria
    • Mpango mkakati
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha

WILAYA YA KARAGWE YAZINDUA KIPINDI CHA PILI CHA TASAF AWAMU YA TATU.

Imewekwa: August 11th, 2021

Na Innocent E. Mwalo.

Mkuu wa Wilaya ya Karagwe Bi. Julieth Binyura, mnamo 10/08/2021, amezindua kikao kazi cha kujenga uelewa kuhusu kipindi cha pili cha awamu ya tatu ya mpango wa Kunusuru Kaya Maskini nchini Tanzanaia (TASAF).

Akizungumza na wawezeshaji waliofika ili kupata mafunzo hayo, Mh. Binyura alisema kuwa madhumuni ya mpango wa kipindi cha pili ni kuwezesha kaya za walengwa kutumia fursa za kuongeza kipato, kuboresha huduma za jamii na kiuchumi, na kuwezesha katika maendeleo ya watoto ambao ni raslmali watu.

Mh. Binyura ameishukuru Serikali ya awamu ya sita na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hasan kwa kuendelea kuuboresha mpango huu wa TASAF na kuona tija ya kuzisaidia kaya hizo maskini ili ziweze kunufaika.

Aidha amewataka wawezeshaji kuzingatia mafunzo watakayopatiwa na wataalamu na kwamba wazingatie na kuhakikisha mpango unawafikia walengwa pindi watakapokuwa uko vijijini na wafuate miongozo iliyowekwa na kuwa makini.

“Nitoe rai kwenu wote kuzingatia mafunzo haya na kuhakikisha mnatekeleza mpango kazi huu mtakapokuwa huko vijijini basi mkazingazitie miongozo mliyopewa na kuhakikisha walengwa wote wananufaika na mpango huu”alisema Mh. Binyura.

Akisoma hotuba mbele ya Washiriki wa Mafunzo hayo Afisa Mwezeshaji kutoka wa TASAF Makao Makuu, ndugu Ahmed Mafiu,  amesema kuwa kipindi cha awamu ya tatu ya mfuko wa maendeleo ya jamii (TASAFIII) kinatekelezwa katika Halmashauri zote 184 za Tanzania Bara na Wilaya zote za Zanzibar..

Aidha ameongeza kuwa kipindi cha pili cha awamu ya tatu TASAF kitafika kaya milioni moja laki nne na nusu zenye jumla ya watu zaidi ya million saba nchi nzima.

“Mkazo mkubwa katika kipindi hiki cha pili umewekwa katika kuwezesha kaya zitakazoandikishwa kwenye mpango kufanya kazi ili kuongeza kipato”alisema Mafiu.

Mafiu alisema kuwa kipindi hiki cha pili kitahakikisha kwamba huduma za jamii zinaongezwa na kuboreshwa ili kutoa huduma na kuendeleza rasilmali Watoto hususani katika upatikanaji wa Elimu na Afya.

Akitaja walengwa wa awamu hii ya pili, Mafiu amesema kuwa ni kaya zinazoishi katika hali duni kwenye Vijiji,Mitaa na, Shehia na kwamba wanufaika ndani ya kaya ni Watoto wenye umri chini ya miaka mitano wanaohudhuria kliniki,wanafunzi wa shule za awali,shule za msingi na shule za sekondari,mama wajawazito na mwanakaya mwenye ulemavu.

“Niseme tu kwamba mpango huu unatoa ruzuku za aina mbili,ruzuku ya msingi na ruzuku ya masharti kwa wale ambao wanatakiwa kwenda shuleni na Watoto wanaohudhuria kliniki”alisema Mafiu.

Hata hivyo Lwanda alisema kuwa kuna ajira mpya ambazo pia zitaweza kuwanufaisha mwanakaya mmoja ambaye ataonekana kuwa na uwezo wa kufanya kazi.

Mafiu amemshukuru Mkurugenzi Mtendaji, Michael Nzyungu kwa kutoa wawewzeshaji wengi na hasa ngazi ya kata ili kuja kushiriki mpango kazi huo.

Naye Mratibu wa TASAF Wilaya ya Karagwe Edius Rwangoga ameshukuru wataalamu hao kwa kuweza kuiweka Wilaya ya Karagwe katika mpango huu kwa awamu nyingine tena na kuwaweka watu wenye ulemavu katika mpango huo.

Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO YA ASILIMI 10 October 04, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI KADA YA DEREVA II NA WAANDISHI WAENDESHA OFISI II September 30, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI WASAIDIZI KUMBUKUMBU DARAJA LA II NA MTENDAJI WA KIJIJI WA III October 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI February 21, 2022
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KAMATI YA LISHE YAKETI KUJADILI UTEKELEZAJI WA AFUA ZA LISHE, KIPINDI CHA ROBO YA TATU 2024/2025.

    April 22, 2025
  • KUELEKEA MSIMU WA KAHAWA 2025/2026: MAAFISA UGANI KARAGWE DC WAPEWA MAFUNZO ILI KUWASAIDIA WANANCHI KUONGEZA THAMANI YA ZAO HILO.

    April 11, 2025
  • WALENGWA WA TASAF KARAGWE DC WANUFAIKA NA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA KIFEDHA WALIZOANZISHA.

    March 17, 2025
  • DC LAIZER AWATAKA WANAWAKE WA KARAGWE KUJIIMARISHA KIUCHUMI.

    March 08, 2025
  • Angalia zote

Video

SHIRIKI UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 KARAGWE TUMEJIPANGA
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • History
  • Dira na Dhamira
  • Fomu za mbalimbali
  • NEEMA INAKUJA KWA WAKULIMA
  • FEDHA ZILIZOPOKELEWA KWA AJILI YA MFUKO WA JIMBO

Viunganishi vihusishi

  • NECTA
  • UTUMISHI
  • TOVUTI YA TAIFA
  • TAMISEMI
  • FFARS
  • SALARY SLIP

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    KARAGWE KAGERA TANZANIA

    Anuani ya posta: BOX 20 KARAGWE

    Simu: 028-2227148

    Simu ya mkononi: 028-2227148

    Barua pepe: ded@karagwedc.go.tz ded.karagwedc@kagera.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright©2017 karagwedc. All rights reserved.