• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
KARAGWE DISTRICT COUNCIL
KARAGWE DISTRICT COUNCIL

United Republic of Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KARAGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na dira
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
        • Sekondari
        • Msingi
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Mazingira na Taka ngumu
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Ufugaji na Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Inayokuja
    • Iliyotekelezwa
    • Inayoendelea
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Taarifa
    • Sheria
    • Mpango mkakati
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha

WAZIRI JAFFO AIFAGILIA WILAYA YA KARAGWE, AMWAGA NEEMA TENA

Imewekwa: January 6th, 2021

Na Innocent Mwalo.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mh. Suleimani Jaffo (Mb), mnamo 06/01/2021 alifanya ziara ya kikazi Wilayani Karagwe iliyolenga kukagua na kuangalia maendeleo ya miradi mbalimbali inayotekelezwa wilayani hapa, ambapo pamoja na mambo mengine ameoneshwa kuridhishwa na kufurahishwa sana na utekelezwaji na utunzwaji wa miradi hiyo.

Baadhi ya miradi ambayo Mh. Waziri Jaffo aliitembelea ni pamoja na ujenzi wa vyumba 3 vya madarasa na matundu 6 ya vyoo katika Shule ya Msingi Ihembe ambapo mradi huu umekamilika kwa gharama za shilingi 66, 600,000.00 ikiwa ni fedha iliyotolewa kwa ufadhili wa serikali kupitia Programu ya Lipa Kulingana na matokeo  (EP4R).

Huku akioneshwa kuridhishwa sana na utekelezaji na utunzwaji wa mradi huu ambao ulizinduliwa nae mnamo mwaka 2018, Mh. Waziri Jaffo aliupongeza uongozi wa shule hiyo na ule wa Wilaya ya Karagwe kwa ujumla kwa kutekeleza na kutunza miradi mbalimbali mara inapokamilika wilayani hapa.

Zaidi alioneshwa kuvutiwa na ujenzi wa maktaba unaoendelea katika shule ya msingi Ihembe, mradi ambao unafadhiliwa na baadhi ya wananchi wa kijiji hicho ambapo Mh. Waziri Jaffo aliahidi kwa uongozi wa Wilaya ya Karagwe na kwa wananchi waliokuwa wamekusanyika kumsikiliza katika viwanja vya shule ya Msingi Ihembe ya kwamba ofisi yake inakusudia kuangalia namna ya kusaidia ujenzi wa maktaba hiyo pamoja na baadhi ya miradi ya shule za msingi na sekondari iliyoombwa kwa nyakati tofauti na mbunge wa Jimbo la Karagwe ambae pia ni Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mh. Innocent Lugha Bashungwa.

Katika hatua nyingine Mh. Jaffo aliutembelea mradi wa ujenzi wa Hospitali ya Wilaya, uliopo eneo la Nyakanongo, mradi ambao umekamilika kwa zaidi ya asilimia 98, huku ukigharimu kiasi cha shilingi blioni moja na milioni mia nane ikiwa ni fedha kutoka serikali kuu na kiasi kingine cha shilingi 161, 477, 869.00 ikiwa ni fedha iliyochangiwa na Halmashauri ya Wilaya ambapo licha ya kupongeza jitihada za uongozi wa wilaya hii, Mh. Waziri Jaffo alitoa agizo kwa Halmashauri ya Wilaya kuendelea kutenga kutoka katika mapato ya ndani, fedha kwa ajili ya ukamilishwaji wa maeneo muhimu ambayo hayakamilika.

Aidha, katika hatua nyingine Mh. Waziri Jaffo, ameahidi kwamba ofisi yake itatoa kiasi cha shilingi bilioni moja ambapo kiasi cha shilingi milioni mia tano (500,000,000.00/=) itatumika kwa ajili ya ujenzi wa wodi ya wanaume na kiasi kingine kinachobaki kitatumika kwa ajili ya ununuzi wa vifaa tiba ili kukidhi mahitaji ya hospitali.

Ziara ya Mh. Jaffo, kwa mara nyingine ilitoa agizo kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Karagwe, Mh. Godwin Kitonka na Timu ya Menejimenti kuongeza kasi ya ukusanyaji wa mapato licha ya kupongeza hatua iliyofikiwa ya kukusanya mapato hayo zaidi ya asilimia 49 mpaka sasa.

Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO YA ASILIMI 10 October 04, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI KADA YA DEREVA II NA WAANDISHI WAENDESHA OFISI II September 30, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI WASAIDIZI KUMBUKUMBU DARAJA LA II NA MTENDAJI WA KIJIJI WA III October 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI February 21, 2022
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KAMATI YA LISHE YAKETI KUJADILI UTEKELEZAJI WA AFUA ZA LISHE, KIPINDI CHA ROBO YA TATU 2024/2025.

    April 22, 2025
  • KUELEKEA MSIMU WA KAHAWA 2025/2026: MAAFISA UGANI KARAGWE DC WAPEWA MAFUNZO ILI KUWASAIDIA WANANCHI KUONGEZA THAMANI YA ZAO HILO.

    April 11, 2025
  • WALENGWA WA TASAF KARAGWE DC WANUFAIKA NA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA KIFEDHA WALIZOANZISHA.

    March 17, 2025
  • DC LAIZER AWATAKA WANAWAKE WA KARAGWE KUJIIMARISHA KIUCHUMI.

    March 08, 2025
  • Angalia zote

Video

SHIRIKI UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 KARAGWE TUMEJIPANGA
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • History
  • Dira na Dhamira
  • Fomu za mbalimbali
  • NEEMA INAKUJA KWA WAKULIMA
  • FEDHA ZILIZOPOKELEWA KWA AJILI YA MFUKO WA JIMBO

Viunganishi vihusishi

  • NECTA
  • UTUMISHI
  • TOVUTI YA TAIFA
  • TAMISEMI
  • FFARS
  • SALARY SLIP

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    KARAGWE KAGERA TANZANIA

    Anuani ya posta: BOX 20 KARAGWE

    Simu: 028-2227148

    Simu ya mkononi: 028-2227148

    Barua pepe: ded@karagwedc.go.tz ded.karagwedc@kagera.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright©2017 karagwedc. All rights reserved.