WATUMISHI WAPYA WA KADA MBALIMBALI KARAGWE DC WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI YA UTUMISHI WA UMMA.
Watumishi wapya wa Kada Mbalimbali wa Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe wamepewa mafunzo elekezi ya Utumishi wa Umma ili kuwajengea uelewa wa Sheria, Miongozo na Kanuni za Maadili ya Utumishi wa Umma.
Mafunzo hayo yaliyoandaliwa na Idara ya Utumishi kwa kushirikiana na Taasisi Mbalimbali za Umma kama vile TAKUKURU na Tume ya Utumishi wa Waalimu yametolewa mapema leo Juni 10, 2025 katika ukumbi wa Halmashauri (ANGAZA).
Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo, kaimu Mkurugenzi Mtendaji Bi. Henrietta William amewahimiza Watumishi kufuata kanuni na miongozo katika utekelezaji wa majukumu yao ili waweze kuzitumikia nafasi zao kwa amani.
" Tumepewa dhamana ya kuwatumikia Wananchi kwa nafasi mbalimbali, tukatumike vyema na kiuadilifu. Niwasihi mkaishi viapo vyenu na kufuata miongozo ya Utumishi wa Umma hata mnapokua nje ya maeneo ya kazi" Alisema Bi.Henrietta.
Naye, Afisa Utumishi na Rasilimali Watu Ndg. Hamduni Siraji amewapa miongozo ya Utumishi wa Umma ikiwemo taratibu za ruhusa na likizo, kupanda madaraja, uhamisho, kugombea nafasi kwenye siasa, kanuni na makosa kwenye utendaji.
Aidha, Watumishi hao walipata nafasi ya kuuliza maswali kuhusu sheria na miongozo mbalimbali yenye utata kwa ajili ya maelezo zaidi.
Watumishi waliopatiwa mafunzo hayo ni takribani 169 kutoka kwenye kada mbalimbali ikiwemo Afya, Elimu, Utendaji, Misitu, Maendeleo ya Jamii, Habari nakadhalika.
KARAGWE KAGERA TANZANIA
Anuani ya posta: BOX 20 KARAGWE
Simu: 028-2227148
Simu ya mkononi: 028-2227148
Barua pepe: ded@karagwedc.go.tz ded.karagwedc@kagera.go.tz
Copyright©2017 karagwedc. All rights reserved.