• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
KARAGWE DISTRICT COUNCIL
KARAGWE DISTRICT COUNCIL

United Republic of Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KARAGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na dira
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
        • Sekondari
        • Msingi
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Mazingira na Taka ngumu
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Ufugaji na Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Inayokuja
    • Iliyotekelezwa
    • Inayoendelea
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Taarifa
    • Sheria
    • Mpango mkakati
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha

WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WAENDELEA KUNUFAIKA NA MIKOPO ISIYOKUWA NA RIBA.

Imewekwa: January 11th, 2021

Na Innocent Mwalo.

Halmashauri ya Wilaya Karagwe imeendelea kutekeleza Ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) ya mwaka 2020 pamoja na  agizo la Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia na Sheria ya fedha Na.4 ya mwaka 2018 inayozitaka Halmashauri zote nchini kuhakikisha zinatenga asilimia 10 ya mapato ya ndani ikiwa ni mikopo yenye masharti nafuu na isiyo na riba kwa ajili ya mfuko wa vikundi vya wanawake,vijana na watu wenye ulemavu.

Hivi karibuni Halmashauri hii imetoa mikopo usiokuwa na riba wa jumla ya Tsh.88,000,000 kwa vikundi 31 ambavyo kati ya hivyo vikundi 24 ni vya wanawake na vikundi 7 vya vijana.

Awali katika taaarifa yake kwa mgeni rasmi ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya hii, Mh. Geofrey Mheluka, Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii katika Halmashauri hii Bi. Edina Kabyazi alimtaarifu mgeni rasmi huyo ya kwamba vikundi vilivyokuwa vinakabidhiwa mkopo ni vile ambavyo vimepewa Elimu juu ya kuhakikisha kwamba mkopo huu unatumika kwa malengo yaliyopangwa kwa kuzingatia kanuni na taratibu na bila kutawaliwa na ubinafsi wala upendeleo.

”Napenda kusisitiza vikundi vyenye miradi mingine kuhakikisha fedha zote zinaingizwa katika shughuli za miradi na si vinginevyo, na taarifa ya mapato na matumizi ifahamike kwa wanakikundi wote’’, alisisitiza Bi. Edina.

Aidha pamoja na kuainisha changamoto ya baadhi ya vikundi kutorejesha mikopo kwa mjibu wa mkataba hasa vya vijana, Bi Edina aliahidi ya kwamba Idara yake itaendelea kufanya tathmini ya kina ili vikundi vinavyokidhi vigezo viweze kukopeshwa kiasi hicho kidogo.

Kwa upande wake Mh. Mheluka alitoa rai kwa wanavikundi kuwa waaminifu katika marejesho ili vikundi vingine pia vinufaike na fursa hii Huku akiagizwa kukabidhiwa kwake kwa orodha ya wale aliowaita wadaiwa sugu.

Kwa mujibu wa taarifa ya Bi. Edina kwa mgeni rasmi, Halmashauri ya wilaya ya Karagwe imeshachangia kiasi cha Tsh. 109,448.052 sawa na asilimia 10% ya mapato halisi yaliyokusanywa kwa kipindi cha tangu Julai 2020 hadi Disemba 2020. Aidha taarifa hiyo inaonesha ya kwamba tangu mwaka 2015/2016 mpaka sasa Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe imeshachangia jumla ya Tsh 651,755,632/= kwenye mfuko wa wanawake,vijana na watu wenye ulemavu huku kiasi cha Tsh 1,331,488,000/= kikiwa kimekopeshwa kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu vipatavyo 526 vyenye wanufaika 9143.

 

 

 

 

Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO YA ASILIMI 10 October 04, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI KADA YA DEREVA II NA WAANDISHI WAENDESHA OFISI II September 30, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI WASAIDIZI KUMBUKUMBU DARAJA LA II NA MTENDAJI WA KIJIJI WA III October 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI February 21, 2022
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KAMATI YA LISHE YAKETI KUJADILI UTEKELEZAJI WA AFUA ZA LISHE, KIPINDI CHA ROBO YA TATU 2024/2025.

    April 22, 2025
  • KUELEKEA MSIMU WA KAHAWA 2025/2026: MAAFISA UGANI KARAGWE DC WAPEWA MAFUNZO ILI KUWASAIDIA WANANCHI KUONGEZA THAMANI YA ZAO HILO.

    April 11, 2025
  • WALENGWA WA TASAF KARAGWE DC WANUFAIKA NA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA KIFEDHA WALIZOANZISHA.

    March 17, 2025
  • DC LAIZER AWATAKA WANAWAKE WA KARAGWE KUJIIMARISHA KIUCHUMI.

    March 08, 2025
  • Angalia zote

Video

SHIRIKI UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 KARAGWE TUMEJIPANGA
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • History
  • Dira na Dhamira
  • Fomu za mbalimbali
  • NEEMA INAKUJA KWA WAKULIMA
  • FEDHA ZILIZOPOKELEWA KWA AJILI YA MFUKO WA JIMBO

Viunganishi vihusishi

  • NECTA
  • UTUMISHI
  • TOVUTI YA TAIFA
  • TAMISEMI
  • FFARS
  • SALARY SLIP

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    KARAGWE KAGERA TANZANIA

    Anuani ya posta: BOX 20 KARAGWE

    Simu: 028-2227148

    Simu ya mkononi: 028-2227148

    Barua pepe: ded@karagwedc.go.tz ded.karagwedc@kagera.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright©2017 karagwedc. All rights reserved.