• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
KARAGWE DISTRICT COUNCIL
KARAGWE DISTRICT COUNCIL

United Republic of Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KARAGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na dira
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
        • Sekondari
        • Msingi
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Mazingira na Taka ngumu
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Ufugaji na Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Inayokuja
    • Iliyotekelezwa
    • Inayoendelea
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Taarifa
    • Sheria
    • Mpango mkakati
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha

WANAWAKE 187 WA JUMUIYA YA KIISLAM YA WILAYA YA KARAGWE WAPATIWA MAFUNZO YA UJASIRIAMALI

Imewekwa: November 18th, 2024

WANAWAKE 187 WA JUMUIYA YA KIISLAM YA WILAYA YA KARAGWE WAPATIWA MAFUNZO YA UJASIRIAMALI

Wanawake 187 wa Jumuiya ya Kiislam Wilaya ya Karagwe wamepatiwa mafunzo ya ujasiriamali ili kuwawezesha kuzalisha kwa faida na kunufaika fursa ya Mikopo ya  asilimia 10 inayotolewa na Halmashauri. Mafunzo haya yamefanyika Jumapili tarehe 17/11/2024 na yaliandaliwa na Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe kwa ushirikiano na Idara ya Maendeleo ya Jamii pamoja na idara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji.

Akizungumza wakati wa Mafunzo hayo, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe Bi. Happiness Msanga amesema kuwa Mafunzo hayo yanalenga kuwainua Wanawake kiuchumi kwa kuwajengea uwezo wa kutambua fursa za biashara zilizopo maeneo yao na kuzitumia ipasavyo katika kukuza mitaji yao sambamba na kuwaeleza namna ya kuongeza mitaji kupitia Mikopo ya asilimia 10 inayotolewa kwenye Halmashauri kwa ajili ya Vikundi vya Wanawake,Vijana na Watu wenye Ulemavu.

“Zamani wanawake tulizoea kuhudumiwa lakini kwa sasa mazingira yamebadilika  hivyo tunawajibu wa kuanza kujishughulisha 

Ili tusaidiane majukumu kwenye familia kwa kufanya hivyo hata matukio ya ukatili yanaweza kupungua kwasababu mengine yanatokana na utegemezi uliopitiliza na ukosefu wa fedha. Niwasihi kina mama wenzangu tutumie mafunzo haya kutambua fursa zilizopo na kuzitumia kujitengeneza ili tuweze kunufaika na mikopo ya Mama Samia ambayo inatolewa na Halmashauri” Alisema Bi.Happiness

Aidha, Bi. Happiness amewataka wanawake hao kuwa vinara wa kuhubiri amani na utulivu  kipindi hiki ambacho tuelekea  Uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika Novemba 27, 2024. Pia  amewasisitiza kuudhuria kampeni pindi zitakapoanza ili waweze kusikiliza sera na kushiriki kikamilifu katika Uchaguzi utakaowapatia Viongozi watakaowaongoza ipasavyo.

Naye, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wanawake wa Kiislam Wilaya ya Karagwe Bi. Hidaya Kamuzora akizungumza kwa niaba ya Wanawake amemshukuru Mkurugenzi na Uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe kwa kutambua umuhimu wa elimu ya ujasiriamali kwao na kuwapatia mafunzo hayo ambayo yatawawezesha kuinuka kiuchumi na kuwafanya wawe na nidhamu ya pesa za biashara hali ambayo itawapunguzia utegemezi na kuleta maendeleo kwenye jamii.

Mafunzo yaliyotolewa kwa Wanawake hao ni maana halisi ya Ujasiriamali, Sifa za Mjasiriamali, Jinsi ya kutambua fursa za ujasiriamali, Namna ya kukuza mtaji na kuweka akiba, Mbinu za kibiashara pamoja na jinsi ya kutengeneza vikundi na  namna ya kuomba mikopo ya Halmashauri.

Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO YA ASILIMI 10 October 04, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI KADA YA DEREVA II NA WAANDISHI WAENDESHA OFISI II September 30, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI WASAIDIZI KUMBUKUMBU DARAJA LA II NA MTENDAJI WA KIJIJI WA III October 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI February 21, 2022
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KAMATI YA LISHE YAKETI KUJADILI UTEKELEZAJI WA AFUA ZA LISHE, KIPINDI CHA ROBO YA TATU 2024/2025.

    April 22, 2025
  • KUELEKEA MSIMU WA KAHAWA 2025/2026: MAAFISA UGANI KARAGWE DC WAPEWA MAFUNZO ILI KUWASAIDIA WANANCHI KUONGEZA THAMANI YA ZAO HILO.

    April 11, 2025
  • WALENGWA WA TASAF KARAGWE DC WANUFAIKA NA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA KIFEDHA WALIZOANZISHA.

    March 17, 2025
  • DC LAIZER AWATAKA WANAWAKE WA KARAGWE KUJIIMARISHA KIUCHUMI.

    March 08, 2025
  • Angalia zote

Video

SHIRIKI UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 KARAGWE TUMEJIPANGA
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • History
  • Dira na Dhamira
  • Fomu za mbalimbali
  • NEEMA INAKUJA KWA WAKULIMA
  • FEDHA ZILIZOPOKELEWA KWA AJILI YA MFUKO WA JIMBO

Viunganishi vihusishi

  • NECTA
  • UTUMISHI
  • TOVUTI YA TAIFA
  • TAMISEMI
  • FFARS
  • SALARY SLIP

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    KARAGWE KAGERA TANZANIA

    Anuani ya posta: BOX 20 KARAGWE

    Simu: 028-2227148

    Simu ya mkononi: 028-2227148

    Barua pepe: ded@karagwedc.go.tz ded.karagwedc@kagera.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright©2017 karagwedc. All rights reserved.