• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
KARAGWE DISTRICT COUNCIL
KARAGWE DISTRICT COUNCIL

United Republic of Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KARAGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na dira
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
        • Sekondari
        • Msingi
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Mazingira na Taka ngumu
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Ufugaji na Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Inayokuja
    • Iliyotekelezwa
    • Inayoendelea
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Taarifa
    • Sheria
    • Mpango mkakati
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha

‘’Tutachukua Hatua kwa Watendaji Watakaoshindwa Kusimamia Ajenda ya Lishe Wilayani Karagwe’’ - Kitonka.

Imewekwa: June 4th, 2021

Na Innocent E. Mwalo.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe, ndugu Godwin Kitonka, kwa mara nyingine, amewaagiza watendaji wa vijiji na kata wilayani hapa kulifanya suala la lishe kuwa ni moja ya vipeumbele katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku na kuwaonya wale watakaolega katika kutekeleza agizo hilo la serikali ya kwamba serikali haitasita kuchukua hatua dhidi yao kwa mujibu wa sheria.

Ndugu Kitonka alitoa maelekezo haya kwa watendaji wa kata wilayani hapa katika kikao cha tathmini ya mkataba wa lishe kilichofanyika katika ukumbi Angaza ambayo kikao hicho kiliwahusisha watendaji hao wa kata na baadhi ya wataalam kutoka katika Idara mbalimbali za Halmashauri ya wilaya.

‘’Naomba kuwaeleza kupitia kikao hiki kuwa suala la lishe katika vijiji na kata zenu sio la hiari tena, ninyi watendaji wa kata nendeni mkavisimamie kata zenu na vijiji vilivyopo katika maeneo yenu, ili kwa mwezi mmoja toka tarehe ya kikao hiki, kila kijiji na kata kikafufue au kuunda upya (kama hamna) kamati za lishe kwenye ngazi hizo za kata na vijiji’’, alisema Kitonka.

Kitonka alisisitiza,’’ Lakini sio tu mkafufue nakuunda kamati hizo, bali nendeni mkahakikishe orodha ya wajumbe wa kamati hizo za lishe zinabandikwa kwenye mbazo za matangazo kwa kila kijijii na kata ili wananchi kwenye maeneo hayo wapate kuwatambua wajumbe hao’’.

Ndugu Kitonka alienda mbali na kuwaagiza watendaji wa kata kuhakikisha katika kila kata na vijiji kunakuwa na majalada yenye mihtasari ya vikao vya lishe na katika mikutano mikuu ya vijiji pamoja na ile ya kamati za maendeleo ya kata (KAMAKA) agenda ya lishe iwe ni suala la kudumu.

‘’Kwa kuwa suala la utapiamlo ni kubwa sana katika mkoa wa Kagera, kwa mara nyingine natoa maagizo kwa watendaji wa vijiji na kata pamoja na wale watumishi wanaohusika na huduma ya afya ya kwamba ili suala la udumavu liweze kukomeshwa  wilayani hapa, hatuna budi kufanya pia ufuatiliaji kwa akina mama wajawazito ili kurekebisha kasoro hizo kabla ya watoto kuzaliwa’’, alisema ndugu Kitonka.

Katika hatua nyingine ndugu Kitonka aliwaeleza washiriki wa kikao hicho juu ya dhamira ya serikali katika Halmashauri ya wilaya hii katika kulithamini suala la lishe ambapo kwa kuanzia kwa mwaka wa fedha 2021/2022, Halmashuri ya wilaya imetenga bajeti ya kiasi cha shilingi milioni 83 kwa ajili ya kutekeleza shughuli zinazohusiana na masuala ya lishe.

Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO YA ASILIMI 10 October 04, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI KADA YA DEREVA II NA WAANDISHI WAENDESHA OFISI II September 30, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI WASAIDIZI KUMBUKUMBU DARAJA LA II NA MTENDAJI WA KIJIJI WA III October 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI February 21, 2022
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KAMATI YA LISHE YAKETI KUJADILI UTEKELEZAJI WA AFUA ZA LISHE, KIPINDI CHA ROBO YA TATU 2024/2025.

    April 22, 2025
  • KUELEKEA MSIMU WA KAHAWA 2025/2026: MAAFISA UGANI KARAGWE DC WAPEWA MAFUNZO ILI KUWASAIDIA WANANCHI KUONGEZA THAMANI YA ZAO HILO.

    April 11, 2025
  • WALENGWA WA TASAF KARAGWE DC WANUFAIKA NA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA KIFEDHA WALIZOANZISHA.

    March 17, 2025
  • DC LAIZER AWATAKA WANAWAKE WA KARAGWE KUJIIMARISHA KIUCHUMI.

    March 08, 2025
  • Angalia zote

Video

SHIRIKI UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 KARAGWE TUMEJIPANGA
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • History
  • Dira na Dhamira
  • Fomu za mbalimbali
  • NEEMA INAKUJA KWA WAKULIMA
  • FEDHA ZILIZOPOKELEWA KWA AJILI YA MFUKO WA JIMBO

Viunganishi vihusishi

  • NECTA
  • UTUMISHI
  • TOVUTI YA TAIFA
  • TAMISEMI
  • FFARS
  • SALARY SLIP

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    KARAGWE KAGERA TANZANIA

    Anuani ya posta: BOX 20 KARAGWE

    Simu: 028-2227148

    Simu ya mkononi: 028-2227148

    Barua pepe: ded@karagwedc.go.tz ded.karagwedc@kagera.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright©2017 karagwedc. All rights reserved.