PPRA YAKAMILISHA MAFUNZO YA SIKU 3 YA MFUMO WA NeST KARAGWE DC.
Leo tarehe 13/06/2025 Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA) imekamilisha Mafunzo ya siku tatu (03) ya Matumizi ya Mfumo wa Kielektroniki wa Manunuzi ya Umma (NeST) yaliyotolewa kwa Watumishi wa Idara ya Afya, Elimu Sekondari na Msingi pamoja na Watendaji Kata na Vijiji katika Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe.
Mafunzo hayo, yamefanyika katika ukumbi wa Halmashauri (Angaza) kuanzia tarehe 11 hadi 13 Juni, 2025 kwa lengo la kuwajengea uwezo watumishi kutumia mfumo kwa urahisi pamoja na kutatua changamoto walizokutana nazo wakati wa kutumia mfumo huo.
Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi wakati wa kufunga mafunzo hayo, Ndg. Tito Molel ambaye pia ni Mkuu wa Kitengo cha Manunuzi Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe amewasisitiza Watumishi hao kutumia mafunzo walioyapata kutekeleza majukumu yao ya manunuzi pamoja na kuwasilisha changamoto wamazokutana nazo ili zifanyiwe kazi.
Naye, Mkufunzi kutoka Ofisi ya PPRA Kanda ya Ziwa Ndg. Mahobe Singu amesema kuwa ni vizuri kuwa na mpango wa manunuzi kabla ya kufanya manunuzi ili uweze kukuongoza wakati wa mchakato.
" Ukiwa na Mpango wa manunuzi utarahisisha mchakato pia utaepukana na migogoro inayoweza kutokea baina yako na mzabuni hususani kwenye vigezo vya bidhaa husika, ni vizuri kuainisha vigezo sahihi vya bidhaa unayotaka" Alisema Ndg. Singu.
Aidha, NeST (National e-Procurement System of Tanzania ) ni mfumo wa kielektroniki unaorahisisha usajili wa kielektroniki wa zabuni , usimamizi wa mikataba na malipo ya kielektroniki.
KARAGWE KAGERA TANZANIA
Anuani ya posta: BOX 20 KARAGWE
Simu: 028-2227148
Simu ya mkononi: 028-2227148
Barua pepe: ded@karagwedc.go.tz ded.karagwedc@kagera.go.tz
Copyright©2017 karagwedc. All rights reserved.