• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
KARAGWE DISTRICT COUNCIL
KARAGWE DISTRICT COUNCIL

United Republic of Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KARAGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na dira
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
        • Sekondari
        • Msingi
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Mazingira na Taka ngumu
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Ufugaji na Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Inayokuja
    • Iliyotekelezwa
    • Inayoendelea
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Taarifa
    • Sheria
    • Mpango mkakati
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha

MPANGO WA TASAF AWAMU YA TATU, SEHEMU YA PILI, WAANZA KWA KISHINDO WILAYANI KARAGWE.

Imewekwa: February 18th, 2021

Na Innocent E. Mwalo.

Ikiwa ni Mpango wa Tatu, Sehemu ya Pili  ya Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini, (TASAF), uliozinduliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk John Pombe Magufuli,  Julai 17,2020, utekelezwaji wa mradi huu wilayani Karagwe unatajwa kuwa umefanyika kwa mafanikio makubwa ambapo hadi sasa umefikia dirisha la tatu tangu shughuli za mradi huu zilipoanza wakati huo.

Takwimu zilizotolewa mnamo tarehe 19/02/202 na Mratibu wa Mradi huu wilayani hapa, bwana Edius Rwangonga, zilionesha kuwa jumla ya shillingi 444,864,000 zimepokelewa na zinatajiwa kuhawilishwa kwa wanufaika wapatao 8,195 kwa dirisha la tatu linalofanyika mwezi Februari 2021 ikiwa orodha ya walengwa waliohakikiwa katika Mpango wa Tasafi Awamu ya Tatu, sehemu ya pili ya kuanza kwa zoezi la kuhawilishwa kwa fedha hizo.

Kwa upande mwingine bwana Rwangoga alibainisha kwamba mradi huu wa TASAF Awamu ya Tatu, Sehemu ya Pili utakuwa na tofauti na kidogo na ile ilitekelezwa katika Awamu za Kwanza na za Pili kutokana na ukweli kwamba utekelezaji wa Awamu ya Tatu sehemu ya Pili umejikita na kusisitizwa kwa walengwa kuwekeza katika miradi midogomigo na ya kati ili iweze kuwasaidia kujipatia mahitaji yao muhimu.

‘Katika TASAF Awamu ya Tatu, sehemu ya pili ruzuku zitakazotolewa zitajikita zaidi katika miradi ya maedeleo katika sekta za elimu, afya na hasa upatikanaji wa Bima ya Afya ya CHFili kuwa na uhakika wa huduma ya afya  na miundombinu’’, alisisitiza bwana Rwangoga.


Nao wanufaika wa mpango huu wa TASAF awamu ya Tatu, Sehemu ya Pili, kwa upnade mmoja walielezea kufurahishwa kwao na ruzuku hiyo inayotolewa na serikali ambapo waleelezea jinsi watakavyonuifa na ruzuku hiyo.

Mlengwa mmoja aliyejitambulisha kwa majina Levina Murashani kutoka Kayanga alisema yeye kama mama ambaye ana watoto watatu, ruzuku hiyo imemsaidia katika matumizi ya watoto haswa mahitaji ya shule ambapo alitoa ushuhuda kuwa kupitia ruzuku ya fedha hiyo ya TASAF imeweza kumsaidia kumudu kusomesha mtoto wake hadi kufikia elimu ya chuo Kikuu.

Mlengwa mwingine, bwana Mpembelege Zemambo wa kijiji cha Bugene alikiri kunufaika na mradi huu ambapo alibainisha kuwa mbali na kupata mahitaji ya watoto ameweza kuanzisha mradi wa ufugaji kuku ambao humsaidia kujipatia mahitaji mengine mengine ya kifamilia.

Kwa upande wake Bi. Amida Mjagala ambaye ni Afisa Mhawilishaji wa fedha hizo za ruzuku za TASAF mbali na kukiri kuwepo kwa changamoto kwa kiasi fulani kwa baadhi ya walengwa  kuzitumia fedha hizo kwa malengo yaliyokusudiwa, alieleza kwamba kwa kiasi kikubwa walengwa wengi wamekuwa wakitumia ruzuku hiyo vizuri huku akibanisha ya mafano wa kuwa na walengwa katika eneo lake walioweza kujenga nyumba za mabati na hivyo kuondokana na adha ya kunyeshewa na mvua kwani hapo awalin walikuwa wanaishi kwenye nyumba zilizoezekwa na nyasi.

Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO YA ASILIMI 10 October 04, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI KADA YA DEREVA II NA WAANDISHI WAENDESHA OFISI II September 30, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI WASAIDIZI KUMBUKUMBU DARAJA LA II NA MTENDAJI WA KIJIJI WA III October 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI February 21, 2022
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KAMATI YA LISHE YAKETI KUJADILI UTEKELEZAJI WA AFUA ZA LISHE, KIPINDI CHA ROBO YA TATU 2024/2025.

    April 22, 2025
  • KUELEKEA MSIMU WA KAHAWA 2025/2026: MAAFISA UGANI KARAGWE DC WAPEWA MAFUNZO ILI KUWASAIDIA WANANCHI KUONGEZA THAMANI YA ZAO HILO.

    April 11, 2025
  • WALENGWA WA TASAF KARAGWE DC WANUFAIKA NA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA KIFEDHA WALIZOANZISHA.

    March 17, 2025
  • DC LAIZER AWATAKA WANAWAKE WA KARAGWE KUJIIMARISHA KIUCHUMI.

    March 08, 2025
  • Angalia zote

Video

SHIRIKI UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 KARAGWE TUMEJIPANGA
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • History
  • Dira na Dhamira
  • Fomu za mbalimbali
  • NEEMA INAKUJA KWA WAKULIMA
  • FEDHA ZILIZOPOKELEWA KWA AJILI YA MFUKO WA JIMBO

Viunganishi vihusishi

  • NECTA
  • UTUMISHI
  • TOVUTI YA TAIFA
  • TAMISEMI
  • FFARS
  • SALARY SLIP

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    KARAGWE KAGERA TANZANIA

    Anuani ya posta: BOX 20 KARAGWE

    Simu: 028-2227148

    Simu ya mkononi: 028-2227148

    Barua pepe: ded@karagwedc.go.tz ded.karagwedc@kagera.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright©2017 karagwedc. All rights reserved.