• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
KARAGWE DISTRICT COUNCIL
KARAGWE DISTRICT COUNCIL

United Republic of Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KARAGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na dira
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
        • Sekondari
        • Msingi
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Mazingira na Taka ngumu
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Ufugaji na Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Inayokuja
    • Iliyotekelezwa
    • Inayoendelea
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Taarifa
    • Sheria
    • Mpango mkakati
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha

MKOPO WA SHILINGI 138,000,000/= WATOLEWA KWA VIKUNDI 42 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU, KWA KIPINDI CHA JANUARI – MACHI, 2021WILAYANI KARAGWE.

Imewekwa: April 16th, 2021

Na Innocent E. Mwalo.

Katika kutekeleza agizo la Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Sheria ya Fedha namba 4 iliyotungwa na Bunge hilo mwaka 2018 ambayo inayozitaka Halmashauri zote nchini kuhakikisha zinatenga asilimia 10 ya mapato yake ya ndani ya kila mwezi kwa ajili ya mfuko wa wanawake, vijana na watu wenye ulemavu,  Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe kwa kipindi cha Januari – Machi, 2021 imetenga na kutoa kiasi cha shilingi 138,000,000/= ikiwa ni mkopo kwa vikundi 42 vya wanawake, vijana na wenye ulemavu.

Hafla ya makabidhiano ya fedha hizo ilifanyika katika Ukumbi wa Vijana Rafiki wa Angaza, mnamo Aprili 18, 2021, ambapo viongozi waandamizi wa Halmashauri na Wilaya akiwemo Mkuu wa Wilaya ya Karagwe, Mh. Godfrey Mheluka, Katibu Tawala Wilaya, Mh. Innocent Nsena, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya, Mh. Wallace Mashanda na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ndugu Godwin Kitonka, kwa nyakati tofauti walitoa maelekezo muhimu kwa wanavikundi hao waliopokea mkopo huo.

Mh. Mheluka pamoja na mambo mengine, aliwahimiza na kuwaagiza wanufaika wa mkopo huo kuhakikisha mkopo huo walioupata unatumika kwa malengo yaliyopangwa na kukusudiwa ambapo kila kikundi kiliaswa kuzingatia kanuni na taratibu walizojiwekea bila kutawaliawa na ubinafsi.

‘’Kumewekuwa na changamoto mbalimbali za urejeshaji wa mikopo hii hasa kwa kundi la vijana licha ya kwamba mikopo hii inatolewa bila riba yeyote lakini baadhi ya vijana wanaonekana kutokuwa waaminifu,  hivyo mitumie hafla hii kuwaagiza ninyi mnaopewa mkopo huu leo kuhakikisha marejesho ya mkopo huu yanafanyika kila mwezi kwa mujibu wa mkataba wenu kwani kipindi cha miezi mitatu mnachopewa kama kipindi cha neema kinatosha sana kujipanga kwa ajili ya kuanza kufanya marejesho ya mikopo hii kuanzia Agosti 2021, na mtapaswa kumaliza marejesho hayo mwezi Aprili, 2022’’, alisisitiza Mh. Mheluka.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya, Mh. Kitonka, alitoa wito kwa kundi la watu wenye ulemavu kuchangamkia fursa ya kuomba mikopo hiyo ambapo aliwaambia watu wenye ulemavu ya kwamba serikali imelegeza masharti ya ukopaji kwa kundi hilo ambapo kwa sasa hata mtu mmoja anaweza kuomba mkopo huo pale anapokosa  watu wa kuunda nao kundi hilo  kwa ajili ya kupata mkopo hiyo.

Naye Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii, Edina Kabyazi aliviagiza vikundi hivyo kuhakikisha kuwa vinawasilisha taarifa ya maendeleo ya kikundi inayoonyesha mafanikio na changamoto  za kikundi.

Kwa upande mwingine chombo hiki lilitembela na kuangazia miradi mbalimbali iliyokwisha kupewa mikopo na Halmashauri ya Wilaya hii kwa vipindi tofauti na mradi mmojawapo uliotembelewa ulikuwa ni ‘Yes Group’ uliopo eneo la Kayanga ambao mwaka 2020 ulipewa mkopo wa kiasi cha shilingi milioni saba na ukafanikiwa kujenga kiwanda cha kuchakata alizeti kwa ajili ya kutengeneza mafuta ya kupikia.

Tangu mwaka 2015/2016 mpaka hivi leo, Halmashauri ya Wilaya imechangia kiasi cha Tshs. 715,244,385/= kwenye mfuko wa wanawake, vijana na watu wenye ulemavu huku kiasi cha Tshs. 1,466,488,000/= kikiwa kimekopeshwa kwa vikundi vya wanawake, vijana na wenye ulemavu vipatavyo 570 na wanufaika 9,643.

Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO YA ASILIMI 10 October 04, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI KADA YA DEREVA II NA WAANDISHI WAENDESHA OFISI II September 30, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI WASAIDIZI KUMBUKUMBU DARAJA LA II NA MTENDAJI WA KIJIJI WA III October 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI February 21, 2022
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KAMATI YA LISHE YAKETI KUJADILI UTEKELEZAJI WA AFUA ZA LISHE, KIPINDI CHA ROBO YA TATU 2024/2025.

    April 22, 2025
  • KUELEKEA MSIMU WA KAHAWA 2025/2026: MAAFISA UGANI KARAGWE DC WAPEWA MAFUNZO ILI KUWASAIDIA WANANCHI KUONGEZA THAMANI YA ZAO HILO.

    April 11, 2025
  • WALENGWA WA TASAF KARAGWE DC WANUFAIKA NA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA KIFEDHA WALIZOANZISHA.

    March 17, 2025
  • DC LAIZER AWATAKA WANAWAKE WA KARAGWE KUJIIMARISHA KIUCHUMI.

    March 08, 2025
  • Angalia zote

Video

SHIRIKI UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 KARAGWE TUMEJIPANGA
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • History
  • Dira na Dhamira
  • Fomu za mbalimbali
  • NEEMA INAKUJA KWA WAKULIMA
  • FEDHA ZILIZOPOKELEWA KWA AJILI YA MFUKO WA JIMBO

Viunganishi vihusishi

  • NECTA
  • UTUMISHI
  • TOVUTI YA TAIFA
  • TAMISEMI
  • FFARS
  • SALARY SLIP

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    KARAGWE KAGERA TANZANIA

    Anuani ya posta: BOX 20 KARAGWE

    Simu: 028-2227148

    Simu ya mkononi: 028-2227148

    Barua pepe: ded@karagwedc.go.tz ded.karagwedc@kagera.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright©2017 karagwedc. All rights reserved.