• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
KARAGWE DISTRICT COUNCIL
KARAGWE DISTRICT COUNCIL

United Republic of Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KARAGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na dira
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
        • Sekondari
        • Msingi
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Mazingira na Taka ngumu
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Ufugaji na Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Inayokuja
    • Iliyotekelezwa
    • Inayoendelea
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Taarifa
    • Sheria
    • Mpango mkakati
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha

KIKAO CHA TATHIMINI YA SHUGHULI ZA LISHE KWA ROBO YA PILI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA KARAGWE

Imewekwa: January 23rd, 2025

KIKAO CHA TATHIMINI YA SHUGHULI ZA LISHE KWA ROBO YA PILI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA KARAGWE

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe Ndg. Jackson Mwakisu leo mapema Tarehe 23/1/2025 ameongoza kikao cha tathimini ya shughuli za lishe kwa kipindi cha robo ya pili kuanzia mwezi Oktoba hadi Desemba,2024.

Aidha, Ndg; Mwakisu amewataka wajumbe hao kuendelea kutoa elimu na kila mmoja atimize wajibu wake ili kufikia malengo yaliyokusudiwa. Pia amevishukru vyombo vya habari vya kijamii kwa kuendelea kutoa elimu sahii ya lishe na mambo mengine kwa uharaka akiwaomba watumishi wa ngazi zote kuwaeleza wananchi kufuatilia elimu hizo. Hata hivyo Mwakisu amewataka wanaume kuondoa mfumo dume na kushiriki huduma za malezi kwa watoto wao na kuwasisitiza maafisa ugani kuendelee kuwahimiza wananchi kulima vyakula vya kutosha na kuchangia chakula mashuleni ili Watoto wetu waendelee kupata chakula Shuleni.

“Kwahiyo suala la lishe tunavyokaa hapa sisi, tunajadiliana mustakabali wa maendeleo ya Halmashauri yetu. Watoto wetu wa baadae waje kuwa na akili, wafanye mambo makubwa kwa ajili ya Nchi yetu”


Akisoma taarifa ya Lishe kwa robo ya pili Oktoba Desemba Afisa Lishe wa Wilaya ya Karagwe Bi. Asnath Thobias ameeleza shughuli zilizofanywa na idara hiyo kwa robo hii ya pili ikiwa ni ununuzi na Ufungaji wa Mashine 4 za kuongeza virutubishi Kwenye unga wa mahindi katika shule tatu za sekondari (Sekondari ya Ihembe, Kawela, Nyabiyonza na mdau mmoja Kata ya Nyakahanga) pia aliwasisitiza Wanaume kushiriki katika matukio mbalimbali ya Lishe katika jamii Kwani wanaume ndiyo wanao toa maamuzi ndani ya familia.


Aidha, Mganga mkuu wa Wilaya ya Karagwe Dr. Agness Mwaifuge ameishauri kamati ya lishe ya Wilaya kuendelea kutoa elimu kwenye jamii juu ya vyakula sahii ili kuondokana na magonjwa ya utapiamlo na udumavu na kama wajumbe wa kamati ya lishe wasione aibu katika kuwaelimisha wananchi ili kuwa na watoto wasio na udumavu, Wito huo ameutoa kwenye kikao cha kawaida cha robo ya pili Oktoba- Novemba 2024 kilichoketi katika ukumbi wa angaza mjini Kayanga.

Kupitia kikao hicho wajumbe wa kamati ya lishe Wilaya ya Karagwe wameeleza namna walivyotekeleza shughuli za lishe kwa kipindi hicho kupitia sekta na taasisi zao ambapo Afisa Maendeleo Ya Jamii Bi; Henrieta Wiliam alieleza kwenye kikao hicho wameendelea kuhamasisha jamii kujihusisha na kilimo ili kupata chakula Cha kutosha katika kaya na kuendelea kupata mlo Kamili na Wananchi kujishughurisha katika masuala ya kiuchumi Kwa kusajili vikundi kwaajili ya kupata mikopo ili kuimarisha uchumi ndani ya familia.

Aidha, Kaimu Afisa kilimo wa Wilaya ya Karagwe Ndg; Yustadi Dominic akiwasilisha taarifa ya idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi wameendelea kuwaelimisha wananchi Kutunza mashamba, kutengeneza bustani za mbogamboga majumban kwao ili kuongeza uzalishaji wa mbogamboga, kilimo Cha viazi Lishe, ulaji wa Samaki, na ufugaji wa wanyama hasa ngombe na mbuzi kwaajili ya unywaji wa maziwa jumla ya mabwawa 65 ya ufugaji wa Samaki ambapo Kwa kipindi Cha Oktoba Desemba kilo 265 za samaki zimevunwa ili kuongeza Lishe Bora katika jamii.


Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO YA ASILIMI 10 October 04, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI KADA YA DEREVA II NA WAANDISHI WAENDESHA OFISI II September 30, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI WASAIDIZI KUMBUKUMBU DARAJA LA II NA MTENDAJI WA KIJIJI WA III October 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI February 21, 2022
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • HATI SAFI ISIWE BANGO LA KUTUPUMZISHA TUJITUME ZAIDI KUIDUMISHA - RC MWASSA.

    June 17, 2025
  • KARAGWE DC YAADHIMISHA SIKU YA MTOTO WA AFRIKA.

    June 16, 2025
  • PPRA YAKAMILISHA MAFUNZO YA SIKU 3 YA MFUMO WA NeST KARAGWE DC.

    June 13, 2025
  • WATUMISHI WAPYA WA KADA MBALIMBALI KARAGWE DC WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI YA UTUMISHI WA UMMA.

    June 11, 2025
  • Angalia zote

Video

SHIRIKI UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 KARAGWE TUMEJIPANGA
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • History
  • Dira na Dhamira
  • Fomu za mbalimbali
  • NEEMA INAKUJA KWA WAKULIMA
  • FEDHA ZILIZOPOKELEWA KWA AJILI YA MFUKO WA JIMBO

Viunganishi vihusishi

  • NECTA
  • UTUMISHI
  • TOVUTI YA TAIFA
  • TAMISEMI
  • FFARS
  • SALARY SLIP

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    KARAGWE KAGERA TANZANIA

    Anuani ya posta: BOX 20 KARAGWE

    Simu: 028-2227148

    Simu ya mkononi: 028-2227148

    Barua pepe: ded@karagwedc.go.tz ded.karagwedc@kagera.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright©2017 karagwedc. All rights reserved.