• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
KARAGWE DISTRICT COUNCIL
KARAGWE DISTRICT COUNCIL

United Republic of Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KARAGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na dira
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
        • Sekondari
        • Msingi
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Mazingira na Taka ngumu
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Ufugaji na Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Inayokuja
    • Iliyotekelezwa
    • Inayoendelea
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Taarifa
    • Sheria
    • Mpango mkakati
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha

KARAGWE DC YAADHIMISHA SIKU YA LISHE KITAIFA

Imewekwa: October 31st, 2024

KARAGWE DC YAADHIMISHA SIKU YA LISHE KITAIFA

Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe leo tarehe 30 Oktoba 2024 imeadhimisha siku ya Lishe Kitaifa katika viwanja vya Zahanati ya Kijiji Kiruruma kata ya Kiruruma. Maadhimisho haya yanaadhimishiwa kila mwaka tarehe 30 ya mwezi Oktoba, yakisindikizwa na kauli mbiu mbalimbali zenye kubeba ujumbe wa Lishe na ulaji wa mlo kamili ili kuepukana na udumavu katika jamii.

Kwa mwaka huu 2024, Maadhimisho ya siku ya Lishe kitaifa yamebeba kauli mbiu isemayo “Mchongo ni Afya yako, zingatia unachokula” ikiwa na lengo la kutoa elimu ya lishe kwa jamii kwa kuzingatia mapendekezo ya mwongozo wa kitaifa wa chakula na ulaji ili kuondoa dhana potofu na mitazamo hasi iliyopo kuhusu ulaji na ulishwaji wa watoto katika jamii. Maadhimisho hayo, yamembata na Utoaji wa huduma mbalimbali za Afya kama vile upimaji wa wingi wa damu kwa watoto, Presha kwa Wajawazito, ulinganisho wa Urefu na Uzito pamoja na utoaji wa elimu ya mlo kamili .

Akizungumza kwenye maadhimisho hayo, Makamo Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe na Diwani wa kata ya Chanika, Mhe: Longino Wilbard  ametaka wananchi kuhakikisha wanazingatia wanacho kula na wajihusishe na shughuli za kilimo ambazo zitawawezesha kupata aina mbalimbali za vyakula ikiwemo matunda na mbogamboga, pamoja na kuzingatia maelekezo yote wanapewa na wataalamu wa Afya na Lishe .

“Niwaombe kina mama muhakikishe kwenye mashamba yenu mmepanda vyakula na matunda ambavyo  ni rahisi kupatikana kwenye mazingira yetu kwa kufanya hvyo mtaweza kupata mlo kamili  kwa urahisi, vibaki vile  ambavyo ni vikubwa  ambavyo vitalazimu kununua kama vile nyama, samaki na vingine ambavyo ni vigumu kupata kwenye mazingira yetu”. Alisema Mhe: Longino.

Naye, Ndugu Claudia Nkuba ambaye ni Kaimu Mratibu wa Lishe wa Wilaya wakati akiwasilisha risala iliyoandaliwa kwa ajili ya maadhimisho hayo, ameishukuru Serikali kwa kutambua umuhimu wa Lishe kwa wananchi na kuiadhimisha Siku ya Lishe kitaifa ili kuhimiza ulaji na kuzingatia mtindo bora wa maisha hususani ulaji wa vyakula mchanganyiko, kuepukana na matumizi ya pombe, tumbaku na bidhaa zake, pia ameongeza kuwa Serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali inatekeleza mwongozo wa kitaifa wa utoaji wa huduma ya chakula na lishe shuleni.

Kwa upande wake, Paskazia John mkazi Kiruruma ameshukuru kwa elimu aliyoipata na ameahidi kuwa balozi mzuri wa Lishe kijijini hapo na ameomba elimu hiyo itolewe mara kwa mara ili wananchi wasichukulie poa swala la lishe ambalo linaathari nyingi kiuchumi na kijamii.

Aidha, Mheshimiwa Longino ametumia maadhimisho hayo kuwasisitiza wananchi kushiriki uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika Novemba 27, 2024 pamoja na kuwakumbusha wazazi wajibu wao wa kuwapeleka watoto shuleni na kuwalea hayo kwenye misingi bora na maadili.

Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO YA ASILIMI 10 October 04, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI KADA YA DEREVA II NA WAANDISHI WAENDESHA OFISI II September 30, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI WASAIDIZI KUMBUKUMBU DARAJA LA II NA MTENDAJI WA KIJIJI WA III October 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI February 21, 2022
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KAMATI YA LISHE YAKETI KUJADILI UTEKELEZAJI WA AFUA ZA LISHE, KIPINDI CHA ROBO YA TATU 2024/2025.

    April 22, 2025
  • KUELEKEA MSIMU WA KAHAWA 2025/2026: MAAFISA UGANI KARAGWE DC WAPEWA MAFUNZO ILI KUWASAIDIA WANANCHI KUONGEZA THAMANI YA ZAO HILO.

    April 11, 2025
  • WALENGWA WA TASAF KARAGWE DC WANUFAIKA NA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA KIFEDHA WALIZOANZISHA.

    March 17, 2025
  • DC LAIZER AWATAKA WANAWAKE WA KARAGWE KUJIIMARISHA KIUCHUMI.

    March 08, 2025
  • Angalia zote

Video

SHIRIKI UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 KARAGWE TUMEJIPANGA
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • History
  • Dira na Dhamira
  • Fomu za mbalimbali
  • NEEMA INAKUJA KWA WAKULIMA
  • FEDHA ZILIZOPOKELEWA KWA AJILI YA MFUKO WA JIMBO

Viunganishi vihusishi

  • NECTA
  • UTUMISHI
  • TOVUTI YA TAIFA
  • TAMISEMI
  • FFARS
  • SALARY SLIP

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    KARAGWE KAGERA TANZANIA

    Anuani ya posta: BOX 20 KARAGWE

    Simu: 028-2227148

    Simu ya mkononi: 028-2227148

    Barua pepe: ded@karagwedc.go.tz ded.karagwedc@kagera.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright©2017 karagwedc. All rights reserved.