• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
KARAGWE DISTRICT COUNCIL
KARAGWE DISTRICT COUNCIL

United Republic of Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KARAGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na dira
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
        • Sekondari
        • Msingi
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Mazingira na Taka ngumu
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Ufugaji na Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Inayokuja
    • Iliyotekelezwa
    • Inayoendelea
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Taarifa
    • Sheria
    • Mpango mkakati
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha

KAMBI YA SIKU 5 YA MADKTARI BINGWA WA MAMA SAMIA YAHUDUMIA WAGONJWA 508 KARAGWE DC

Imewekwa: November 10th, 2024

KAMBI YA SIKU 5 YA MADKTARI BINGWA WA MAMA SAMIA YAHUDUMIA WAGONJWA 508 KARAGWE DC

Kambi ya Siku 5 Madaktari Bingwa wa Mama Samia katika Hospitali ya Wilaya ya  Karagwe (Nyakanongo) imehudumia wagonjwa 508.Kambi hiyo ilianza  Novemba 4 hadi 9, 2024 ikiwa na madktari bingwa 7 kutoka Hospitali za Rufaa Mikoa mbalimbali Nchini kama vile  Hospitali ya Bugando, Temeke , Songea, Muhimbili nakadhalika.Huduma zilitolewa ni Magonjwa ya Wanawake, Upasuaji, Meno, Magonjwa ya watoto, na Magonjwa ya ndani kama vile kisukari.

Hayo yameelezwa na Kiongozi wa msafara wa Madaktari Bingwa Dr. Edgar Ndaboine ambaye ni Daktari wa Magonjwa ya Wanawake wakati wakiagana na Madaktari wa Wilaya ya Karagwe Dr.Ndaboine ameupongeza Uongozi wa Wilaya ya Karagwe kwa kufikisha ujumbe wa ujio wa madaktari hao kwasababu muitikio umekua mkubwa na utayari wa wagonjwa katika pokea matibabu na ushauri waliopewa na wataalamu hao.

“Kwa siku tano zilizohudumu hapa Hospitali ya Wilaya tumehudumia wagonjwa 508 na kufanya upasuaji kwa watu zaidi ya 18 pamoja na kutoa Rufaa kwa wagonjwa wa kansa kwenda hospitali ya Bugando kwa matibabu zaidi. Tunaamini ujio wetu umewasaidia wananchi kupunguza gharama za matibabu pamoja na umbali wa kufuata huduma za kibingwa” alisema Dr.Ndaboine

Naye, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe Bi. Happiness Msanga amewashukuru Madaktari hao kwa kuhudumia wananchi wa Karagwe na kuwaomba kuitikia wito endapo watahitajika tena kwa mara nyingine baada ya menejimenti kujadili ni namna gani wataweza kuwaalika tena lengo likiwa ni kuwahudumia wananchi pamoja na kuwapunguzia gharama. Pia amewapongeza kwa kuwaongezea ujuzi watumishi wa Hospitali ya Wilaya kupitia mafunzo waliokuwa wakiwapatia na anaamini watayatumia vizuri mafunzo hayo.

Kwa upande wake, Mganga mfawidhi wa Hospitali ya Wilaya Dr. Karim Abdallah amewashukuru Madaktari bingwa kwa kuwaongezea ujuzi kupitia mafunzo waliokuwa wakiwapa kila asubuhi pamoja na wakati wa utoaji huduma. Pia ameongeza kuwa, ujio wa Madktari hao umeendelea kuitangaza Hospitali ya Nyakanongo kwa Wananchi ambao pengine hawakujua kama huduma hizo zinatolewa hapo kwani Hospitali hiyo bado ni mpya ina miaka minne tu tangu ianzishwe.

Kambi ya Madaktari Bingwa wa Mama Samia kwa Wilaya ya Karagwe imehudumia Wagonjwa 508 kwa mchanganuo  ufuatao, Magonjwa ya ndani 250, Magonjwa ya Wanawake 123, Magonjwa yanayohusisha upasuaji 48, Magonjwa ya watoto 44 na Meno 43.

Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO YA ASILIMI 10 October 04, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI KADA YA DEREVA II NA WAANDISHI WAENDESHA OFISI II September 30, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI WASAIDIZI KUMBUKUMBU DARAJA LA II NA MTENDAJI WA KIJIJI WA III October 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI February 21, 2022
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KAMATI YA LISHE YAKETI KUJADILI UTEKELEZAJI WA AFUA ZA LISHE, KIPINDI CHA ROBO YA TATU 2024/2025.

    April 22, 2025
  • KUELEKEA MSIMU WA KAHAWA 2025/2026: MAAFISA UGANI KARAGWE DC WAPEWA MAFUNZO ILI KUWASAIDIA WANANCHI KUONGEZA THAMANI YA ZAO HILO.

    April 11, 2025
  • WALENGWA WA TASAF KARAGWE DC WANUFAIKA NA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA KIFEDHA WALIZOANZISHA.

    March 17, 2025
  • DC LAIZER AWATAKA WANAWAKE WA KARAGWE KUJIIMARISHA KIUCHUMI.

    March 08, 2025
  • Angalia zote

Video

SHIRIKI UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 KARAGWE TUMEJIPANGA
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • History
  • Dira na Dhamira
  • Fomu za mbalimbali
  • NEEMA INAKUJA KWA WAKULIMA
  • FEDHA ZILIZOPOKELEWA KWA AJILI YA MFUKO WA JIMBO

Viunganishi vihusishi

  • NECTA
  • UTUMISHI
  • TOVUTI YA TAIFA
  • TAMISEMI
  • FFARS
  • SALARY SLIP

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    KARAGWE KAGERA TANZANIA

    Anuani ya posta: BOX 20 KARAGWE

    Simu: 028-2227148

    Simu ya mkononi: 028-2227148

    Barua pepe: ded@karagwedc.go.tz ded.karagwedc@kagera.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright©2017 karagwedc. All rights reserved.