• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
KARAGWE DISTRICT COUNCIL
KARAGWE DISTRICT COUNCIL

United Republic of Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KARAGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na dira
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
        • Sekondari
        • Msingi
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Mazingira na Taka ngumu
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Ufugaji na Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Inayokuja
    • Iliyotekelezwa
    • Inayoendelea
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Taarifa
    • Sheria
    • Mpango mkakati
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha

HALMASHAURI YA WILAYA YA KARAGWE YAUNDA JUKWAA LA MKAKATI WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA.

Imewekwa: August 12th, 2021

Na Innocent E. Mwalo.

Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe imeunda Jukwaa la Mkakati Wa Usimamizi Wa Mazao Baada ya Kuvuna ikiwa ni kuitikia wito wa Wizara ya Kilimo kupitia mwongozo uliotolewa mwaka 2019 juu ya umuhimu wa majukwaa haya yatakayowezesha kupunguza upungufu wa mazao baada ya shughuli za uvunaji.

Semina ya uundwaji wa jukwaaa hilo ilifanyika hivi karibuni wilayani Karagwe ambapo wawezeshaji kutoka wizara ya Kilimo wakiongozwa na Bi. Daphosa Jerome ambaye ni Afisa Kilimo Msaidizi Mkuu kutoka Wizara ya Kilimo.

‘’Dhima ya jukwaa hili ni kuboresha usimamizi wa mazao baada ya kuvuna kwa kuhakisha uwepo wa mbinu na teknolojia za kupunguza upotevu nakuongeza thamani ya mazao baada ya kuvuna, kutoa motisha kwa uwekezaji katika mifumo ya masoko, pamoja na kuboresha uwezo nauratibu wa mkakati’’, alisisitiza Bi Daphosa.

Bi. Daphosa alielezea umuhimu wa jukwaa hilo kutokana na takwimu kuonesha kuwa pamoja na ukweli kamba Tanzania ina uwezo wa kuzalisha chakula kukidhi mahitaji ya taifa kwa asilimia 100, inakadiriwa kuwa asilimia 30 mpaka 40 ya kiasi hicho cha nafaka kunachovunwa hupotea bila kutumiwa na walaji kwa hiyo malengo ya jukwaa hilo ni pamoja na kujenga uelewa kwa wadau kuhusu usimamizi wa mazao baada ya kuvuna, kuimarisha uwezo wa taasisi za usimamizi wa mazao baada ya kuvuna pamoja kukusanya takwimu na taarifa za upotevu wa mazao baada ya kuvuna.

Naye Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe ambaye ndiye aliyekuwa mgeni rasmi katika shughuli hizo, ndugu Jackson Mwakisu aliishukuru Wizara ya Kilimo kupitia Idara yake ya Usalama wa Chakula kwa kuwa na mkakati huu wa uuundaji wa majukwaa haya ya kuahasisha kuepuka upotevu wa mazao baada ya kuvuna huku akiuelezea mkakati huo kama njia ya kuimarisha kipato cha mkulima baada ya kuvuna kutokana na hatua zitakazochukuliwa na wakulima ili kuepusha upotevu wa mazao baada ya kuvunwa.

Kwa kuzingatia mwongozo uliotolewa na Wizara ya Kilimo, Afisa kutoka katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kagera, ndugu Isaya Tendega alisimamia zoezi la uundaji wa jukwaa hilo ambapo wajumbe wa mkutano huo walimchagua Sostenes Ponsian kuwa Mwenyekiti wa Jukwaa hilo huku Atosha Magande akichaguliwa kuwa Makamu Mwenyekiti na Avit Theofil akichaguliwa kuwa Katibu.

Mwingine akiyechaguliwa alikuwa ni Clara Timothy ambaye alichaguliwa kuwa katibu msaidizi na hivyo basi viongozi hawa wataungana na timu tendaji itayoundwa na wataalam kutoka katika Halmashauri ya Wilaya na kwa mujibu wa mwongozo wa uundaji wa baraza hili pia wajumbe walichagua wawakilishi kutoka makundi ya wakulima ambao waliochaguliwa walikuwa ni pamoja na Anatory Chikalughai, Obed Vincent na Ernestuina Shaban na kwa upande wa asasi zisizokuwa za kiserikali wajumbe waliwachagua Innocent Kokutona na Baltazar Lutataza kuwa wajumbe wa jukwaa hilo.

Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO YA ASILIMI 10 October 04, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI KADA YA DEREVA II NA WAANDISHI WAENDESHA OFISI II September 30, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI WASAIDIZI KUMBUKUMBU DARAJA LA II NA MTENDAJI WA KIJIJI WA III October 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI February 21, 2022
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KAMATI YA LISHE YAKETI KUJADILI UTEKELEZAJI WA AFUA ZA LISHE, KIPINDI CHA ROBO YA TATU 2024/2025.

    April 22, 2025
  • KUELEKEA MSIMU WA KAHAWA 2025/2026: MAAFISA UGANI KARAGWE DC WAPEWA MAFUNZO ILI KUWASAIDIA WANANCHI KUONGEZA THAMANI YA ZAO HILO.

    April 11, 2025
  • WALENGWA WA TASAF KARAGWE DC WANUFAIKA NA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA KIFEDHA WALIZOANZISHA.

    March 17, 2025
  • DC LAIZER AWATAKA WANAWAKE WA KARAGWE KUJIIMARISHA KIUCHUMI.

    March 08, 2025
  • Angalia zote

Video

SHIRIKI UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 KARAGWE TUMEJIPANGA
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • History
  • Dira na Dhamira
  • Fomu za mbalimbali
  • NEEMA INAKUJA KWA WAKULIMA
  • FEDHA ZILIZOPOKELEWA KWA AJILI YA MFUKO WA JIMBO

Viunganishi vihusishi

  • NECTA
  • UTUMISHI
  • TOVUTI YA TAIFA
  • TAMISEMI
  • FFARS
  • SALARY SLIP

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    KARAGWE KAGERA TANZANIA

    Anuani ya posta: BOX 20 KARAGWE

    Simu: 028-2227148

    Simu ya mkononi: 028-2227148

    Barua pepe: ded@karagwedc.go.tz ded.karagwedc@kagera.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright©2017 karagwedc. All rights reserved.