• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
KARAGWE DISTRICT COUNCIL
KARAGWE DISTRICT COUNCIL

United Republic of Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KARAGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na dira
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
        • Sekondari
        • Msingi
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Mazingira na Taka ngumu
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Ufugaji na Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Inayokuja
    • Iliyotekelezwa
    • Inayoendelea
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Taarifa
    • Sheria
    • Mpango mkakati
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha

DC LAIZER AONGOZA USAFI NA BONANZA MAIDHIMISHO YA MIAKA 63 YA UHURU

Imewekwa: December 9th, 2024

DC LAIZER AONGOZA USAFI NA BONANZA MAIDHIMISHO YA MIAKA 63 YA UHURU

Mkuu wa Wilaya ya Karagwe Mhe; Julius Kalanga Laizer ameongoza zoezi la kufanya usafi mazingira na bonanza katika kuadhimisha miaka 63 ya uhuru wa Tanzania leo tarehe 09 Desemba 2024.

Maadhimisho hayo ya miaka 63 Wilaya ya Karagwe yalianza kwa kufanya usafi wa mazingira sehemu mbalimbali za mji wa Kayanga uliongozwa na Mkuu wa Wilaya pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe Bi; Happiness J. Msanga kwa kushirikiana na Watumishi wote na Wananchi wa Wilaya ya Karagwe kwa maeneo ya Stendi ya mabasi Kayanga, Soko la Kayanga  na Ofisi ya Kata ya Kayanga.

Baada ya zoezi la usafi Mhe.Laizer aliongoza Watumishi na Wananchi kuelekea uwanja wa Bashungwa kwa ajili ya Bonanza la michezo ambalo lilihusisha michezo mbalimbali kama vile mpira wa pete  na Mpira wa Miguu ambapo timu ya  ulinzi na usalama ilishindana na  watumishi Halmashauri. Pia kulikua na zoezi la kuendesha baiskeli kuzunguka uwanja huo zote hizi zikiwa ni shamrashamra za kusherekea miaka 63 ya uhuru tangu Tanzania ilipotangazwa rasmi kuwa huru mwaka 1961 na aliyekua Rais wa kwanza wa Tanzania Hayati Julius Kambarage Nyerere.

Aidha, Mhe.Laizer amesema kuwa Wananchi wa Wilaya ya Karagwe wanaungana na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu Hassan na Watanzania wote nchini kuenzi na kuadhimisha Miaka 63 ya Uhuru kwa Amani, Mshikamano na Ushirikiano uliyobeba kauli mbiu isemayo “Uongozi madhubuti na Ushirikishwaji wa Wananchi ni Msingi wa Maendeleo yetu”.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe Bi.Hapiness Msanga amewapongeza Watumishi na Wananchi wote waliojitokeza kushiriki maadhimisho hayo kikamilifu na kwa mshikamano kama ilivyoelekezwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan

Hata hivyo, Maaadhimisho haya hufanyika kila mwaka tarehe 09 Desemba kulingana na maelekezo yanayotolewa na Rais ambapo kwa mwaka huu Mhe. waziri Mkuu Kassim Majaliwa alisema kuwa  Rais ameelekeza Maadhimisho haya yafanyike katika ngazi ya mikoa  na Wilaya  kwa kufanya shughuli za kijamii ikiwemo upandaji miti, usafi wa mazingira katika maeneo ya kijamii kama vile kwenye Masoko, Hospitali, pamoja na mashindano ya michezo mbalimbali, makongamano na midahalo ya kujadili maendeleo endelevu ambayo nchi yetu imefikia katika kipindi cha miaka 63 ya Uhuru.

Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO YA ASILIMI 10 October 04, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI KADA YA DEREVA II NA WAANDISHI WAENDESHA OFISI II September 30, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI WASAIDIZI KUMBUKUMBU DARAJA LA II NA MTENDAJI WA KIJIJI WA III October 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI February 21, 2022
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KAMATI YA LISHE YAKETI KUJADILI UTEKELEZAJI WA AFUA ZA LISHE, KIPINDI CHA ROBO YA TATU 2024/2025.

    April 22, 2025
  • KUELEKEA MSIMU WA KAHAWA 2025/2026: MAAFISA UGANI KARAGWE DC WAPEWA MAFUNZO ILI KUWASAIDIA WANANCHI KUONGEZA THAMANI YA ZAO HILO.

    April 11, 2025
  • WALENGWA WA TASAF KARAGWE DC WANUFAIKA NA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA KIFEDHA WALIZOANZISHA.

    March 17, 2025
  • DC LAIZER AWATAKA WANAWAKE WA KARAGWE KUJIIMARISHA KIUCHUMI.

    March 08, 2025
  • Angalia zote

Video

SHIRIKI UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 KARAGWE TUMEJIPANGA
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • History
  • Dira na Dhamira
  • Fomu za mbalimbali
  • NEEMA INAKUJA KWA WAKULIMA
  • FEDHA ZILIZOPOKELEWA KWA AJILI YA MFUKO WA JIMBO

Viunganishi vihusishi

  • NECTA
  • UTUMISHI
  • TOVUTI YA TAIFA
  • TAMISEMI
  • FFARS
  • SALARY SLIP

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    KARAGWE KAGERA TANZANIA

    Anuani ya posta: BOX 20 KARAGWE

    Simu: 028-2227148

    Simu ya mkononi: 028-2227148

    Barua pepe: ded@karagwedc.go.tz ded.karagwedc@kagera.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright©2017 karagwedc. All rights reserved.