• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
KARAGWE DISTRICT COUNCIL
KARAGWE DISTRICT COUNCIL

United Republic of Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KARAGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na dira
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
        • Sekondari
        • Msingi
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Mazingira na Taka ngumu
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Ufugaji na Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Inayokuja
    • Iliyotekelezwa
    • Inayoendelea
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Taarifa
    • Sheria
    • Mpango mkakati
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha

DC LAIZER AONGOZA BARAZA LA BIASHARA KARAGWE.

Imewekwa: November 8th, 2024

DC LAIZER AONGOZA BARAZA LA BIASHARA KARAGWE.

Mkuu wa Wilaya ya Karagwe  Mhe. Julius Kalanga Laizer ameongoza kikao cha Baraza la Wafanyabiashara wa Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe leo tarehe 7 Novemba, 2024. Baraza hilo limefanyika  katika ukumbi wa Angaza Wilayani humo na kuudhuriwa na Mashirika mbalimbali ya Umma, Taasisi za Kifedha , pamoja na Wafanyabiashara wa Wilaya ya Karagwe

Baraza hilo limelenga kusikiliza kero za Wafanyabishara na kuzipatia ufumbuzi, Kupokea mapendekezo ya nini kifanyike ili kuboresha utoaji huduma na uwekezaji katika Wilaya, pamoja na kutoa maelekezo mbalimbali ya Serikali na taratibu za Halmashauri ili kuendeleza na kudumisha mahusiano mazuri baina ya Serikali na Wafanyabiashara.

Akijibu hoja mbalimbali ziliziwasilishwa na Wafanyabiashara, ikiwemo ulipaji wa Kodi ya zuio ambapo Wafanyabiashara wamekuwa wakitakiwa kulipa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) badala ya wamiliki wa halali wa eneo la biashara, Mhe. Laizer amewataka wafanyabiashara kuhakikisha wanamikataba ya pango na kuiwasilisha mikataba hiyo kwa TRA ili kodi hizo zilipwe na wamiliki wa maeneo hayo na si mfanyabiashara.Pia ametumia baraza hilo kuwataka TRA pamoja na Halmashauri kutathimini majengo yote ya biashara ili kuweza kuwatambua wamiliki wa maeneo hayo.

Aidha, Mhe.Laizer ametoa wito kwa Wafanyabiashara kuimarisha ulinzi na usalama katika maeneo yao ya kazi ikiwemo kuhakikisha wanafunga kamera za ulinzi na kuhifadhi fedha zao kwenye Taasisi za Kifedha kama vile benki badala ya kuweka pesa nyumbani, kwasababu wanahatarisha usalama wao na mali zao.

Naye, Katibu Tawala ndugu Rasul Shandala ametumia baraza hilo kuwakumbusha wafanyabiashara wanaotumia barabara kusafirisha na kupokea mizigo kutoka sehemu mbalimbali, kuzingatia matumizi sahihi ya barabara ikiwemo viwango vya uzito wa magari vilivyowekwa ili kuepuka kuharibu miudombinu ya barabara hizo, pamoja na faini ambazo zinaweza kuwa kero kwa wamiliki wa magari ambao wakati mwingine wanakua hawajui barabara zipi wanapaswa kutumia wanapoingia Wilaya ya Karagwe.

Vilevile, Baraza hilo pia lilitoa nafasi kwa mashirika ya umma pamoja na wadau wa biashara kujibu hoja zilizowahusu ili baraza hilo liwe na tija. Baadhi ya mashirika na wadau waliopata nafasi ya kuzungumza na wafanyabiashara ni Shirika la umeme la Taifa (TANESCO), Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Benki ya NMB na TCB.

Hatahivyo, Ndg. Shandala amepongeza  Wafanyabiashara kwa kuudhuria baraza hilo na kuwashuru kwa michango yao na ushiriki wao katika shughuli mbalimbali za kijamii. Na ametumia nafasi hiyo kutangaza matokeo ya Mbio za Mwenge wa Uhuru 2024 kwa Wilaya ya Karagwe ambapo Wilaya imekua ya 6 kimkoa na ya 32 Kitaifa.

Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO YA ASILIMI 10 October 04, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI KADA YA DEREVA II NA WAANDISHI WAENDESHA OFISI II September 30, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI WASAIDIZI KUMBUKUMBU DARAJA LA II NA MTENDAJI WA KIJIJI WA III October 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI February 21, 2022
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KAMATI YA LISHE YAKETI KUJADILI UTEKELEZAJI WA AFUA ZA LISHE, KIPINDI CHA ROBO YA TATU 2024/2025.

    April 22, 2025
  • KUELEKEA MSIMU WA KAHAWA 2025/2026: MAAFISA UGANI KARAGWE DC WAPEWA MAFUNZO ILI KUWASAIDIA WANANCHI KUONGEZA THAMANI YA ZAO HILO.

    April 11, 2025
  • WALENGWA WA TASAF KARAGWE DC WANUFAIKA NA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA KIFEDHA WALIZOANZISHA.

    March 17, 2025
  • DC LAIZER AWATAKA WANAWAKE WA KARAGWE KUJIIMARISHA KIUCHUMI.

    March 08, 2025
  • Angalia zote

Video

SHIRIKI UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 KARAGWE TUMEJIPANGA
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • History
  • Dira na Dhamira
  • Fomu za mbalimbali
  • NEEMA INAKUJA KWA WAKULIMA
  • FEDHA ZILIZOPOKELEWA KWA AJILI YA MFUKO WA JIMBO

Viunganishi vihusishi

  • NECTA
  • UTUMISHI
  • TOVUTI YA TAIFA
  • TAMISEMI
  • FFARS
  • SALARY SLIP

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    KARAGWE KAGERA TANZANIA

    Anuani ya posta: BOX 20 KARAGWE

    Simu: 028-2227148

    Simu ya mkononi: 028-2227148

    Barua pepe: ded@karagwedc.go.tz ded.karagwedc@kagera.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright©2017 karagwedc. All rights reserved.