• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
KARAGWE DISTRICT COUNCIL
KARAGWE DISTRICT COUNCIL

United Republic of Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KARAGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na dira
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
        • Sekondari
        • Msingi
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Mazingira na Taka ngumu
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Ufugaji na Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Inayokuja
    • Iliyotekelezwa
    • Inayoendelea
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Taarifa
    • Sheria
    • Mpango mkakati
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha

DC LAIZER AMALIZA MGOGORO WA ARDHI ULIODUMU KWA MIAKA 10

Imewekwa: July 23rd, 2025

DC LAIZER AMALIZA MGOGORO WA ARDHI ULIODUMU KWA MIAKA 10

Mkuu wa Wilaya ya Karagwe Mhe: Julius Kalanga Laizer mapema leo Julai 23, 2025 amefanya mkutano wa hadhara na wananchi wa maeneo ya Kijiji cha Igurwa na Kata ya Igurwa na kutatua mgogoro wa Ardhi uliodumu eneo hilo kwa takribani miaka 10 sasa suluhu yake imepatikana.

Mgogoro huo umemalizika kwa maridhiano ya pande zote mbili kati ya serikali ya kijiji na Bwana Salvatory kalabamu ambapo Mkuu wa Wilaya ametoa maelekezo kwa Wataalamu wa ardhi kupima na kuweka mipaka katika maeneo waliokubaliana kumpatia bwana kalabamu na Serikali ya Kijiji.

 Aidha Mh. Laizer amewahakikishia wananchi hao kutokuwa na wasiwasi na kwamba serikali ya Wilaya ya Karagwe imeamua kutumia falsafa ya "Maridhiano" (Reconciliations), ili kumaliza mgogoro huo baina ya pande mbili na kurejesha hali ya amani katika eneo hilo.

Akisoma maridhiano hayo Afisa Ardhi Wilaya ya Karagwe Ndg: Alex Japhet Mpunji amesema Machi 25, 2024 kulifanyika kikao cha maridhiano kilichoongozwa na mkuu wa Wilaya  na April 2024, walitembelea eneo la mgogoro na kubaini Bwana Kalabamu Salvatory   anamiliki eneo lenye ekari  351.61 badala ya ekari 80 ambayo alinunua kutoka kwa wananchi wa serikali ya kijiji hicho.

Pia timu ya wataalam ilibaini anamiliki ardhi ya sehemu ya uchimbaji wa madini yenye ekari 9.5 na aliamuliwa kubaki na ekari 9.5 kama mkataba unavyoonyesha badala 16.5 kama alivokuwa ameonyesha kwenye madai yake ambapo pia kikao cha maridhiano kiliamua kumpatia ekari 50 kutoka kwenye serikali ya kijiji badala ya ekari 80 kama alivokuwa anadai.

Kwa upande wake Salvatory kalabamu ambaye aliwahi kuwa diwani wa Kata ya Igurwa amemshukuru mkuu wa Wilaya kwa kukubali kusuruhisha mgogoro huo wa muda mrefu, ambapo aliamua kusitisha kesi mahakamani ili kupata suruhisho kutoka kwake na serikali ya Kijiji.

Naye Kamanda wa TAKUKURU Wilaya ya Karagwe Ndg: Victor Lesuya, amesema Dira ya TAKUKURU ni kutokomeza vitendo vya rushwa na kusema katika mgogoro huo, isingekuwa busara ya Mkuu wa Wilaya ya kutumia maridhiano basi watu wote wangekuwa katika mikono ya takukuru kwa uchunguzi na hatua zaidi zingechukuliwa kwakuwa Mgogoro ulikuwa unaeleza ekari 80 baada ya kupimwa zikakutwa 361 na Takukuru ikibaini hivyo inakuwa na makosa ya matumizi mabaya ya madaraka, nyaraka za kugushi na kuwasilisha nyaraka za uwongo ili kummilikisha mtu mwingine pamoja na kosa la ukwepaji kodi (utakatishaji).

Ameongeza kuwa Ardhi haiuzwi kiholela hivyo kila mmoja anapaswa kufuata utaratibu ili kupatikana kwa kodi ya serikali.

Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO YA ASILIMI 10 October 04, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI KADA YA DEREVA II NA WAANDISHI WAENDESHA OFISI II September 30, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI WASAIDIZI KUMBUKUMBU DARAJA LA II NA MTENDAJI WA KIJIJI WA III October 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI February 21, 2022
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • DC LAIZER AMALIZA MGOGORO WA ARDHI ULIODUMU KWA MIAKA 10

    July 23, 2025
  • WATHIBITI UBORA WA SHULE, MAAFISA OFISI YA ELIMU MSINGI NA SEKONDARI KARAGWE DC WANOLEWA MFUMO WA SQAS.

    July 10, 2025
  • MASHIRIKA YASIYOKUWA YAKISERIKALI KARAGWE DC YAASWA KUDUMISHA USHIRIKIANO ENDELEVU NA SERIKALI ILI KULETA MATOKEO CHANYA KWA WANANCHI.

    July 01, 2025
  • HATI SAFI ISIWE BANGO LA KUTUPUMZISHA TUJITUME ZAIDI KUIDUMISHA - RC MWASSA.

    June 17, 2025
  • Angalia zote

Video

SHIRIKI UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 KARAGWE TUMEJIPANGA
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • History
  • Dira na Dhamira
  • Fomu za mbalimbali
  • NEEMA INAKUJA KWA WAKULIMA
  • FEDHA ZILIZOPOKELEWA KWA AJILI YA MFUKO WA JIMBO

Viunganishi vihusishi

  • NECTA
  • UTUMISHI
  • TOVUTI YA TAIFA
  • TAMISEMI
  • FFARS
  • SALARY SLIP

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    KARAGWE KAGERA TANZANIA

    Anuani ya posta: BOX 20 KARAGWE

    Simu: 028-2227148

    Simu ya mkononi: 028-2227148

    Barua pepe: ded@karagwedc.go.tz ded.karagwedc@kagera.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright©2017 karagwedc. All rights reserved.