• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
KARAGWE DISTRICT COUNCIL
KARAGWE DISTRICT COUNCIL

United Republic of Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KARAGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na dira
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
        • Sekondari
        • Msingi
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Mazingira na Taka ngumu
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Ufugaji na Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Inayokuja
    • Iliyotekelezwa
    • Inayoendelea
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Taarifa
    • Sheria
    • Mpango mkakati
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha

BARAZA LA MADIWANI WAJA NA MPANGO MKAKATI WAKUHAMASISHA WANANCHI KULIMA MAZAO YA UKAME

Imewekwa: November 13th, 2024

BARAZA LA MADIWANI WAJA NA MPANGO MKAKATI WAKUHAMASISHA WANANCHI KULIMA MAZAO YA UKAME

Mkutano wa Baraza la Madiwani robo ya kwanza la mwaka 2024/2025 (Mwezi Julai hadi Septemba) katika Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe uliofanyika Novemba 12 na 13, 2024 limeweka mpango mkakati wa kuhamasisha Wananchi kulima mazao yanayostahimili ukame ili kupambana njaa itakayosababishwa na mabadiliko ya hali ya hewa ikiwemo ukosefu wa mvua za kutosha kipindi cha Vuli.

Akifungua mkutano huo, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe na Diwani wa Kata ya Nyaishozi Mhe. Wallace Mashanda amezungumzia uhaba wa mvua Wilaya ya Karagwe kwa mwaka huu, ambapo kupitia mkutano huo wa siku mbili Baraza la Madiwani limeazimia kushirikisha viongozi wote ndani ya Wilaya wakiwemo Viongozi  wa dini, Mashirika na Watendaji wa Serikali kuweka mikakati ya kuweka mkazo kwa wananchi kulima mazao yanayostahimili ukame kama vile mihogo na viazi, Pamoja na kuwakumbusha wazazi wenye watoto wanaosoma kuandaa mazao ya chakula mapema kwaajili ya wanafunzi ili mwaka wa masomo utakapoanza watoto waweze kupata chakula shuleni.

Akitoa maelekezo ya Serikali katika mkutano huo, Mkuu wa Wilaya ya Karagwe Mhe. julius Kalanga Laizer amewaomba Waheshimiwa Madiwani, Wadau wa Serikali na Wananchi kuhakikisha Ulinzi na Usalama wa Wilaya unazingatiwa kwa asilimia mia hasa kipindi cha Uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika Novemba 27,2024. Pia alitumia nafasi hiyo kutoa wito kwa Wananchi kuacha kukata miti kwa ajili ya mkaa ikibidi Wilaya itafute namna ya kupunguza vibali vya kukata miti ili kuepukana na ukame.Alizungumzia pia kuhusiana na mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na Halmashauri kwa wananchi ambapo aliutaka Uogozi wa Halmashauri kutoa mafunzo kwa viongozi hususani madiwani ili waweze kufikisha ujumbe sahihi wa mikopo hiyo na kumbushia wadeni kulipa madeni yao ili wengine waweze kukopa.

Naye, Waziri wa Ujenzi na Mbunge wa Jimbo La Karagwe Mhe.Innocent Bashungwa wakati akitoa salamu kwenye mkutano huo, Amesema kuwa Serikali inatarajia kuleta kivuko kwenye Ziwa Burigi ili kurahisisha usafiri kwa wakazi wa kijiji cha Ruhita, Mililo na Kigasha ambapo kwa miaka mingi wamekua wakipata changamoto ya usafiri ambapo iliwalazimu kutumia boti ambazo zinahatarisha usalama wao na mali zao. Pia amewapongeza Madiwani kwa kazi nzuri wanazofanya kwenye kata zao na kutumia nafasi zao kuwaelimisha Wananchi waachane na imani potofu.

Aidha, Waheshimiwa Madiwani wa Kata zote 23 za Wilaya ya Karagwe walipata nafasi ya kuwasilisha taarifa za Kata zao kuanzia Julai hadi Septemba kwa mwaka 2024, Pamoja na kuwasilisha taarifa za Kamati za kudumu za Halmashauri. Wakizungumza kwa nyakati tofauti za uwasilishaji wa taarifa hizo Madiwani walisema kuna uhaba wa mvua jambo ambalo liliwekewa azimio la kupanda mazao yanayostahimili Changamoto nyingine  zilizowasilishwa na Waheshimiwa Madiwani  ni kuhusu makusanyo ya Mapato kwenye vizuizi na uchache wa watumishi baadhi ya maeneo.

Kwa Upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Ya Karagwe Bi.Happiness Msanga wakati akijibu maswali ya papo kwa papo na hoja zilizowasilishwa kwenye taarifa za Kata za Madiwani amesema kuwa Makusanyo ya vizuizi vya Wilaya ya Karagwe wakusanywe kulingana na eneo la utawala na alisisitiza makusanyo yoyote ya kwenye Kata yanatakiwa kupelekwa benki kabla ya kupangiwa matumizi. Kuhusu Uhaba wa Watumishi, Mkurugenzi amesema kuwa, Halmashauri itazingatia msawazo wa watumishi waliopo na kuendelea kuomba Watumishi Serikalini Pia alitoa wito kwa Waheshimiwa Madiwani kuwahamasisha Wananchi kujenga nyumba bora ya kupangisha ili Watumishi wanapopangiwa maeneo hayo waweze kupata makazi.

Aidha, Mkutano huo ulitoa nafasi kwa Mashirika ya Umma kuwasilisha taarifa za utelekelezaji wa miradi yao kulingana na bajeti na kutoa majibu ya hoja ambazo zimeibuliwa na Waheshimiwa Madiwani wakati wa uwasilishwaji wa taarifa za kila Kata. Wakala wa Barabara za Mijini na Vijijini (TARURA) ni moja ya Shirika la Umma lililowasilisha taarifa yake na kujibu hoja zilizoibuliwa kuhusiana na barabara mbalimbali Wilayani humo ikiwemo Bukangaro. Mkurugenzi wa TARURA wilaya ya Karagwe aliwaomba Waheshimiwa Madiwani kuwasilisha changamoto na barabara zitakazopewa kipaumbele kabla ya bajeti ya mwaka mpya itakayopangwa Disemba 2024.

Hata hivyo, Mkutano huo ulipata ugeni kutoka Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma ambao walifanya mafunzo mafupi kwa ajili ya kukumbushia Sheria na Maadili kwa Viongozi na Watumishi wa Umma.

Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO YA ASILIMI 10 October 04, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI KADA YA DEREVA II NA WAANDISHI WAENDESHA OFISI II September 30, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI WASAIDIZI KUMBUKUMBU DARAJA LA II NA MTENDAJI WA KIJIJI WA III October 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI February 21, 2022
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KAMATI YA LISHE YAKETI KUJADILI UTEKELEZAJI WA AFUA ZA LISHE, KIPINDI CHA ROBO YA TATU 2024/2025.

    April 22, 2025
  • KUELEKEA MSIMU WA KAHAWA 2025/2026: MAAFISA UGANI KARAGWE DC WAPEWA MAFUNZO ILI KUWASAIDIA WANANCHI KUONGEZA THAMANI YA ZAO HILO.

    April 11, 2025
  • WALENGWA WA TASAF KARAGWE DC WANUFAIKA NA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA KIFEDHA WALIZOANZISHA.

    March 17, 2025
  • DC LAIZER AWATAKA WANAWAKE WA KARAGWE KUJIIMARISHA KIUCHUMI.

    March 08, 2025
  • Angalia zote

Video

SHIRIKI UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 KARAGWE TUMEJIPANGA
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • History
  • Dira na Dhamira
  • Fomu za mbalimbali
  • NEEMA INAKUJA KWA WAKULIMA
  • FEDHA ZILIZOPOKELEWA KWA AJILI YA MFUKO WA JIMBO

Viunganishi vihusishi

  • NECTA
  • UTUMISHI
  • TOVUTI YA TAIFA
  • TAMISEMI
  • FFARS
  • SALARY SLIP

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    KARAGWE KAGERA TANZANIA

    Anuani ya posta: BOX 20 KARAGWE

    Simu: 028-2227148

    Simu ya mkononi: 028-2227148

    Barua pepe: ded@karagwedc.go.tz ded.karagwedc@kagera.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright©2017 karagwedc. All rights reserved.