• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
KARAGWE DISTRICT COUNCIL
KARAGWE DISTRICT COUNCIL

United Republic of Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KARAGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na dira
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
        • Sekondari
        • Msingi
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Mazingira na Taka ngumu
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Ufugaji na Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Inayokuja
    • Iliyotekelezwa
    • Inayoendelea
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Taarifa
    • Sheria
    • Mpango mkakati
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha

BARAZA LA MADIWANI ‘LACHORA’ DIRA MPYA YA MAENDELEO KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA KARAGWE.

Imewekwa: January 29th, 2021

Na Innocent E. Mwalo.

Kikao cha Baraza la Madiwani kilifanyika hivi karibuni kwa muda kwa siku mbili, kikiwa pia ni kikao cha kwanza cha kazi tangu kuchaguliwa kwa Baraza jipya mnamo Novemba 2020, kimeazimia kwa kauli moja kuongezwaa kwa bidii na kubuniwa kwa mikakati mipya yenye lengo la kuongeza tija na kurahisha shughuli za maendeleo kwa wananchi wilayani hapa.

Awali katika hotuba yake ya ufunguzi, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya, Mh.Wallace Mashanda, pamoja na kupongeza juhudi za menejimenti na uongozzi mzima wa wilaya hii katika suala nzima la ufaulu kwa shule za msingi na sekondari; huku akirejea matokea ya kidato cha nne kwa mwaka 2020 ambapo wilaya ya Karagwe imeshika nafasi ya tatu kati ya Halmashauri nane za mkoa wa Kagera, Mh. Mashanda alitoa maagizo anuai kwa wananchi na maenejimenti ya Halmashauri ya wilaya kuhakikisha wanafunzi wote waliofaulu na kuchaguliwa kujiunga kidato cha kwanza kwa mwaka 2021 wanaripoti shuleni mara moja. Agizo hili liilitokana na takwimu zilizoonesha kusuasua kuripoti kwa wanafunzi hao katika shule mbalimbali za serikali katika Halmashauri ya wilaya hii.

Aidha, katika kuliwekea mkazo suala la uimarishaji wa elimu wilayani hapa, Mh. Mashanda alitoa maagizo mengine kwa shule zote za msingi na sekondari wilayani hapa kuhakiksha kuwa wanafunzi wote wa shule hizo wanapata uji/chakula shuleni.

Agizo jingine la Mh. Mshanda lilikuwa ni juu ya upatikanaji wa takwimu sahihi za wananfunzi wanaokaa chini ili kuweza kuweka mkakati maalum wa kuhakikisha kuwa hakuna mwanafunzi anayekaa chini.

Maagizo mengine yaliyopewa uzito katika hotuba ya Mh. Mashanda ilikuwa ni suala la maafisa ugani kubadilika hasa kwenye suala la usimamizi wa shughuli za kilimo kwa wakulima, pamoja na lile la kuhakisha suala la upimaji wa ardhi na makazi ya watu mijini na vijijini linawekwa kwenye mpango wa bajeti ili watu waweze kupata makazi bora pamoja na kuepuka migogoro ya ardhi inayoikumba wilaya hii kwa sasa.

Hali kadhalika, taarifa ya serikali iliyotolewa na Mkuu wa Wilaya ya Karagwe, Mh. Godfrey Mheluka, ilijulisha na kuwaagiza wananchi wote kuchukua tahadhali zote muhimu kama vile kunawa mikono kwa maji tiririka, kutumia vitakasa mikono pamoja na kuepuka mikusanyiko isiyo ya lazima kufuatia kuepuka kwa dalili za ugonjwa wa homa kali ya ‘’praenomina’’ ikiwa ni pamoja na homa kali, uchovu na kikohozi kikavu.

Kwa upande mwingine, Mhe. Mheluka alitoa taarifa kwa wananchi kupitia kikao hicho juu ya kuzuka kwa ugonjwa wa mafua ya nguruwe na ambapo katika jitihada za kuzuia maambukizi hayo kuenea, amepiga marufuku kwa muda, ulaji na usafirishaji wa nyama za nguruwe.

Aidha katika kujibu maswali yaliyoibuliwa na wajumbe wa kikao hicho ambao ni madiwani kutoka katika kata mbalimbali za wilaya, Mh. Mheluka aliagiza na kutoa ratiba ya siku tatu kwa ofisi yake kukutana na taasisi mbalimbali za serikali zilizopo wilayani hapa kwa ajili ya kushughulikia kero za maji, barabara, bei ya zao la kahawa, vitambulisho vya taifa pamoja na mambo mengine ambayo yaliibuliwa na kikwazo hiki kama masuala yanayokwaza juhudi za ustawi watu wa Karagwe.

Msisitizo mwingine uliotolewa na kikao hicho ulikuwa ni maazimio yaliyotokana na uwasilishwaji wa taarifa za wenyeviti wa Kamati tatu za kudumu za Halmashauri ya Wilaya yaani; Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango chini ya Mwenyekiti wake Mh. Wallace Mashanda, Kamati ya Elimu, Afya na Maji chini ya uenyekiti wa Mh. Charles Beichumila, na ile ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira inayoongozwa na Mh. Valence Kasumuni.

Kwa ujumla kikao hicho ambacho pia kilikuwa ni kikao cha robo ya pili kwa mwaka 2020/2021 kiliagiza na kuelekeza mambo kadhaa wa kadhaa kwa Idara za Fedha, Elimu, Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Usafi na Mazingira ili kuboresha ustawi wa wananchi wa Wilaya ya Karagwe ikiwemo lile la Halmashauri kuongeza wigo wa kukusanya mapato kutoka vyanzo mbalimbali.

Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO YA ASILIMI 10 October 04, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI KADA YA DEREVA II NA WAANDISHI WAENDESHA OFISI II September 30, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI WASAIDIZI KUMBUKUMBU DARAJA LA II NA MTENDAJI WA KIJIJI WA III October 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI February 21, 2022
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KAMATI YA LISHE YAKETI KUJADILI UTEKELEZAJI WA AFUA ZA LISHE, KIPINDI CHA ROBO YA TATU 2024/2025.

    April 22, 2025
  • KUELEKEA MSIMU WA KAHAWA 2025/2026: MAAFISA UGANI KARAGWE DC WAPEWA MAFUNZO ILI KUWASAIDIA WANANCHI KUONGEZA THAMANI YA ZAO HILO.

    April 11, 2025
  • WALENGWA WA TASAF KARAGWE DC WANUFAIKA NA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA KIFEDHA WALIZOANZISHA.

    March 17, 2025
  • DC LAIZER AWATAKA WANAWAKE WA KARAGWE KUJIIMARISHA KIUCHUMI.

    March 08, 2025
  • Angalia zote

Video

SHIRIKI UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 KARAGWE TUMEJIPANGA
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • History
  • Dira na Dhamira
  • Fomu za mbalimbali
  • NEEMA INAKUJA KWA WAKULIMA
  • FEDHA ZILIZOPOKELEWA KWA AJILI YA MFUKO WA JIMBO

Viunganishi vihusishi

  • NECTA
  • UTUMISHI
  • TOVUTI YA TAIFA
  • TAMISEMI
  • FFARS
  • SALARY SLIP

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    KARAGWE KAGERA TANZANIA

    Anuani ya posta: BOX 20 KARAGWE

    Simu: 028-2227148

    Simu ya mkononi: 028-2227148

    Barua pepe: ded@karagwedc.go.tz ded.karagwedc@kagera.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright©2017 karagwedc. All rights reserved.