• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
KARAGWE DISTRICT COUNCIL
KARAGWE DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KARAGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na dira
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
        • Sekondari
        • Msingi
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Mazingira na Taka ngumu
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Ufugaji na Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Inayokuja
    • Iliyotekelezwa
    • Inayoendelea
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Taarifa
    • Sheria
    • Mpango mkakati
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha

Wilaya ya Karagwe Yaitikia Agizo la Makamu wa Rais Juu ya Utunzaji wa Mazingira.

Imewekwa: January 4th, 2018

Wilaya ya Karagwe Yaitikia Agizo la Makamu wa Rais Juu Ya Utunzaji wa Mazingira.

Na Innocent E. Mwalo, KARAGWE

Katika kuitikia kwa vitendo agizo lililotolewa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Samia Suluhu Hassan  Desemba 22, 2017 mjini Dodoma wakati alipozindua Kampeni kabambe ya kuufanya mkoa huo kuwa wa kijani, Wilaya ya Karagwe imetekeleza kwa vitendo agizo hilo kwa kushiriki kikamilifu katika upandaji wa miti takribani 350 katika viunga vya mji wa Kayanga.

Tukio hilo la kihistoria lilifanyika mnamo tarehe 30 Desemba, 2017 ambapo kikundi kiitwacho Karagwe Great Mind alimaarufu kama (Timu Ten Ten) wakishirikiana na Idara ya Mazingira na Taka Ngumu ya Halmashauri ya Wilaya Karagwe kwa pamoja waliweza kuandaa hafla hiyo ya upandaji wa miti takribani 350 zoezi lililoenda sambamba na kufanya usafi katika Kituo cha Afya cha Kayanga.

Mgeni rasmi katika Hafla hiyo alitarajiwa kuwa Mh. Godfrey Mheluka ambaye hata hivyo kutokana na kuwa nje ya wilaya kwa shughuli za kikazi hakuweza kushiriki zoezi hilo kazi iliyofanywa kwa niaba yake na Katibu Tawala wa Wilaya Mh. Innocent Nsena ambaye alikuwa ameongozana takribani na wajumbe wote wa Kamati ya Ulinzi na Usalama wa Wilaya.

Katika maeneo yote ambapo upandaji wa miti ulifanyika wananchi katika Taasisi na maeneo hayo walikabidhiwa kwa maandishi kutunza miti hiyo kwenye maeneo hayo.

Mapema akimkaribisha mgeni rasmi katika kushiriki katika zoezi hilo, Mlezi wa kikundi hicho cha Karagwe Great Mind ndugu Karrim Amri aliwashukuru wananchi walioshiriki katika zoezi hilo ikiwa ni ishara ya kuunga mkono kampeni hiyo.

“Mh. Mgeni rasmi kikundi chetu kina wananchama 26 ambapo kinajihusisha na shughuli mbalimbali za kijamii ikiwemo utunzaji wa mazingira na katika kuonesha hilo tumeamua kuunga mkono jitihada za Makamu wa Rais mama Samia Suluhu Hassan alizozifanya hivi karibuni katika zoezi la upandaji wa miti”, alisema ndugu Karrim.

“Pamoja na kwamba kikundi chetu ni kichanga lakini tumeweza kutumia kiasi cha Tsh.350,000 katika zoezi hili na kwa kweli tunaomba ofisi ya Mkuu wa Wilaya na Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya zinatupa sana ushirikiano lakini bado tunayo changamoto ya kukosa ofisi”, alisisitiza ndugu Karrim.

Kwa upande wake Mgeni rasmi, Katibu Tawala Wilaya Mh. Innocent Nsena pamoja na kusoma hotuba iliyoandaliwa na Mkuu wa Wilaya aliwashukuru wanakikundi hicho na kuwaahidi kwamba wilaya inatambua mchango mkubwa wanautoa kwa jamii na akawahakikishia kwamba daima wilaya itaendelea kuwathamini kwa mchango wa hali na mali wanaoutoa.

“Ofisi ya Mkuu wa Wilaya inatambua kwamba pamoja na kikundi chenu kuwa bado ni kichanga lakini mmekwisha shiriki kwa hali na mali kwa mambo kadhaa ya kijamii na kwa kweli mnastahili pongezi na niwahakikishie kuwa ofisi yetu ipo tayari kwa chochote mtakachohitaji kutoka katika ofisi zetu”, alisema Mh. Nsena.

Matangazo

  • MATOKEO DARASA LA SABA 2022 December 01, 2022
  • WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA SEKONDARI 2023 December 14, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI July 09, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI February 21, 2022
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • ZAWADI

    September 26, 2022
  • WAJERUMANI WASAINI KITABU KWA DED

    September 26, 2022
  • KARAGWE YAPOKEA WAJERUMANI

    September 25, 2022
  • KAMATI YA FEDHA MAFUNZONI

    September 16, 2022
  • Angalia zote

Video

BARAZA LA MADIWANI LAWASIMAMISHA WATUMISHI
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • History
  • Dira na Dhamira
  • Fomu za mbalimbali
  • NEEMA INAKUJA KWA WAKULIMA
  • FEDHA ZILIZOPOKELEWA KWA AJILI YA MFUKO WA JIMBO

Viunganishi vihusishi

  • NECTA
  • UTUMISHI
  • TOVUTI YA TAIFA
  • TAMISEMI
  • FFARS
  • SALARY SLIP

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    KARAGWE KAGERA TANZANIA

    Anuani ya posta: BOX 20 KARAGWE

    Simu: 028-2227148

    Simu ya mkononi: 0754653409

    Barua pepe: ded@karagwedc.go.tz ded.karagwedc@kagera.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright©2017 karagwedc. All rights reserved.