• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
KARAGWE DISTRICT COUNCIL
KARAGWE DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KARAGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na dira
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
        • Sekondari
        • Msingi
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Mazingira na Taka ngumu
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Ufugaji na Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Inayokuja
    • Iliyotekelezwa
    • Inayoendelea
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Taarifa
    • Sheria
    • Mpango mkakati
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha

Mradi wa CHSSP Watambulishwa Wilayani Karagwe

Imewekwa: July 22nd, 2017

Mradi wa CHSSP watambulishwa Wilayani Karagwe

Na Innocent  E. Mwalo, KARAGWE

Community Health  and Social Welfare Strengthening Program (CHSSP) ikiwa ni  Program ya Uimarishaji Mifumo ya Afya na Ustawi wa Jamii  kwa kushirikiana na taasisi iitwayo  John Snow  inc (JSI) ambayo  makao yake katika kanda ya Ziwa yapo jijini Mwanza mnamo siku ya Jumamosi ya tarehe 22 Julai,  2017 ilifanya mkutano wa utambulisho katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya Karagwe lengo likiwa ni kuutambulisha mradi huu wa ushirikiano kati ya serikali ya Tanzania kupitia Wizara, Taasisi na Halmashauri na wadau mbalimbali ambapo muda wake wa utekelezaji ni kuanzia Novemba 2014 – Oktoba 2019.

Mradi huu wa CHSSP unaofadhiliwa na PEPFAR kupitia shirika la USAID huku utekelezaji wake ikifanywa kupitia mashirika mawili yaani JSI (Taasisi ya Utafiti na mafunzo) na World Education Inc. unatarajia kuzifikia takribani Halmashauri 84 kwa muda huo wa miaka mitano ya utekelezaji.

Lengo kuu la Mradi huu ni kuwezesha upatikanaji wa huduma bora za Afya ya jamii na ustawi wa jamii kwa makundi maalum na ya kipaumbele huku malengo mahususi yakiwa ni kuwezesha upatikanaji wa watoa huduma waliobora wa afya ya jamii na ustawi wa jamii pamoja na kuimarisha/kuwezesha utaratibu wa miundo, mifumo na ushirikishwaji wa asasi za kiraia katika kutoa huduma za afya ya jamii na ustawi wa jamii.

Katika lengo la kuwezesha upatikanaji wa watoa huduma waliobora wa afya ya jamii na ustawi wa jamii mikakati ya mradi huu ni kuhakikisha kuwa miongozo mbalimbali inahuishwa na kusambazwa kwa wadau ili kuweza kuchangia kuwafikia watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi, vijana wa kike walio katika balehe na WAVIU.

Mkakati mwingine ni uimarishaji na kupanua nguvu kazi ya ustawi wa jamii mpaka katika ngazi ya kijamii.

Katika ngazi ya Halmashauri ya Wilaya, kamati zitakazoundwa zitasaidia kusimamia na kuwezesha kuundwa kwa kamati za kata, kufanya usimamizi saidizi katika ngazi za chini na kutoa ripoti ya utekelezaji wa shughuli zilizopangwa huku kamati za kata zikitakiwa kufundisha  na kutoa ushauri kwa kamati za vijiji na kutos ripoti ya utekelezaji wa shughuli kwenye kamati ya Halmashauri.

Kwa upande wa Kamati za vijiji, Timu itaratibu shughuli zote za VVU na UKIMWI katika kijiji na mtaa ikiwa pia na kutoa ripoti ya utekelezaji kwenye kamati ya kata.

Kwenye maeneo ambayo Program hii imeshatekelezwa mpaka sasa mafanikio kadhaa yameshafikiwa mpaka sasa ikiwemo kuleta mahusiano mazuri ya kikazi na serikali, Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Tume ya Kudhibiti UKIMWI na Ofisi ya Raisi, TAMISEMI

Pia imeweza kufundisha wafanyakazi wa afya 219, kuwezesha mapitio ya mwongozo wa Kamati za UKIMWI na kuinua/kufufua mifumo ya kijamii katika serikali za mitaa.

Katika hatua ya kuelekea kuanza kutekelezwa kwa mpango huu, Bi. Edina Kabyazi, Afisa Maendeleo ya Jamii Wilaya Karagwe aliteuliwa kuwa mratibu wa “Focal person” huku Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Karagwe ndugu Godwin Moses Kitonka na mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya Karagwe Mh. Wallace Murokozi Mashanda wakisaini Mktaba wa Makuliano ya kufanya kazi (MoU) na Mradi huu wa CHSS.

 

Matangazo

  • MATOKEO DARASA LA SABA 2022 December 01, 2022
  • WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA SEKONDARI 2023 December 14, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI July 09, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI February 21, 2022
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • ZAWADI

    September 26, 2022
  • WAJERUMANI WASAINI KITABU KWA DED

    September 26, 2022
  • KARAGWE YAPOKEA WAJERUMANI

    September 25, 2022
  • KAMATI YA FEDHA MAFUNZONI

    September 16, 2022
  • Angalia zote

Video

BARAZA LA MADIWANI LAWASIMAMISHA WATUMISHI
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • History
  • Dira na Dhamira
  • Fomu za mbalimbali
  • NEEMA INAKUJA KWA WAKULIMA
  • FEDHA ZILIZOPOKELEWA KWA AJILI YA MFUKO WA JIMBO

Viunganishi vihusishi

  • NECTA
  • UTUMISHI
  • TOVUTI YA TAIFA
  • TAMISEMI
  • FFARS
  • SALARY SLIP

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    KARAGWE KAGERA TANZANIA

    Anuani ya posta: BOX 20 KARAGWE

    Simu: 028-2227148

    Simu ya mkononi: 0754653409

    Barua pepe: ded@karagwedc.go.tz ded.karagwedc@kagera.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright©2017 karagwedc. All rights reserved.