• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
KARAGWE DISTRICT COUNCIL
KARAGWE DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KARAGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na dira
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
        • Sekondari
        • Msingi
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Mazingira na Taka ngumu
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Ufugaji na Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Inayokuja
    • Iliyotekelezwa
    • Inayoendelea
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Taarifa
    • Sheria
    • Mpango mkakati
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha

Mkuu wa Mkoa wa Kagera Afanya Ziara ya Kihistoria Wilayani Karagwe.

Imewekwa: February 6th, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Kagera Afanya Ziara ya Kihistoria Wilayani Karagwe.

Na Innocent E.Mwalo, KARAGWE.

Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mh. Meja Jenerali(Mst) Salim Kijuu amefanya ziara ya kihistoria Wilayani hapa kwa kukagua miradi ya maendeleo inayohusisha ujenzi wa Kituo cha Afya cha Kayanga, Kituo cha Afya cha Nyakayanja na Zahanati ya Kafunjo pamoja na kuhimiza shughuli za maendeleo kwenye maeneo hayo ikiwemo suala la kilimo cha kahawa, uanzishwaji wa bustani za matunda pamoja na suala la lishe ili kuepukana na suala la utapiamlo linalotajwa kuzikumba familia nyingi katika mkoa wa Kagera.

Ziara yake hiyo ilianzia katika kituo cha Afya cha Nyakayanja ambapo ujenzi wake umekamilika kwa kiasi kikubwa ambapo katika kituo hicho Mkuu wa Mkoa aliweza kupata taarifa ya ujenzi wa mradi huo ulianza mnamo mwaka 2016 ambapo mpaka sasa ujenzi wa jengo la wagonjwa wa nje iliyogharimu kiasi cha Tsh. 244,425,000.00, ujenzi wa nyumba ya watumishi uliojengwa kwa hisani ya World Vision kwa kiasi cha Tsh.70,900,000.00, ujenzi wa vyoo vya wagonjwa na kichomea taka ambapo kwa pamoja umegharimu kiasi cha Tsh. 12,055,000.00 

Mkuu wa mkoa alioneshwa kugushwa na jitihada hizo za wananchi hasa katika kuchangia miradi ya maendeleo katika maeneo hayo na kuahidi kwamba serikali itatoa kiasi cha Tsh. 400,000,000.00 ili kuunga mkono jitihada hizo.

Baada ya ukkaguzi kwenye kituo hicho, msafara ulielekea katika kituo cha Afya cha Kayanga ambacho ndio kituo kikubwa cha Afya Wilayani hapa chenye uwezo wa kuhudumia wananchi takribani 2,400 mpaka 3,500 kwa mwezi ambapo ujenzi wa miundo mbinu yake unaendelea kwa kasi kubwa.

 Awali katika  taarifa yake kwa Mkuu wa Mkoa, Kamu Mkurugenzi Mtendaji ndugu Adeodata Peter alielezea kuwa huduma katika kituo hiki imeimarika  zaidi ya mara dufu ambapo idadi ya wanawake wanaojifungulia katika kituo hiki imeongezeka kutoka wanawake 40 na 45 ambao walikuwa wanajifungulia kwenye kituo hicho hapo awali hadi kufikia wanawake 110 na 140 kwa mwezi huku vifo vya akina mama vikipungua kutoka kutoka vifo 15 hadi vifo 05 ambayo ni sawa na asilimia 69.

“Ujenzi wa miundo mbinu unaoendelea katika kituo hiki cha afya hiki unalenga kutibu changamoto zilizoonekana hapo hapo katika eneo hilo lakini pia athali za tetemeko la ardhi lililotokea katika mkoa wa Kagera mnamo 10/09/2016 na kusababisha changamoto kadhaa ikiwemo kuharibika kwa  miundombinu ya kituo hiki cha afya na makazi ya watu”, alibainisha ndugu Adeodata kupitia taarifa hiyo.

Ndugu Adeodata aliendelea kusisitiza kwamba kufuatia athari hizo za tetemiko la ardhi, Kituo hiki cha afya kilipokea kiasi cha Tsh.170,714,452.18 mnamo 16/06/2017 kutoka Mfuko wa Maafa wa Mkoa kwa ajili ya ujenzi wa wodi ya wazazi, chumba cha kuhifadhia maiti na power house ambapo kwa mujibu wa Mganga Mkuu wa Wilaya Karagwe, Dkt. Libamba Sobo fedha hizo ziliweza kupelekwa moja kwa moja katika kituo hiki cha afya kwa ajili ya kutekeleza mradi huo kwa kutumia utaratibu wa “Force Account”

Aidha taarifa hiyo iliendelea kusisitiza kwamba kutokana na ahadi iliyotolewa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Ajira, Vijana na Watu wenye Ulemavu, Mh. Jenista Mhagama (Mb) aliyoitoa mnamo 11 -13 /07/2017 wilayani hapa na mkoani Kagera kwa ujumla, kituo cha Afya cha Kayanga kimeweza kupokea takribani kiasi cha 72,989,530 ikiwa ni kutekeleza ahadi yake hiyo juu ya urejeshwaji wa miundombinu hiyo kwenye kituo cha Afya cha Kayanga.

“Sio hivyo, Halmashauri ya Wilaya Karagwe imeweza kupokea pia kiasi cha Tsh. 500,000,000 kutoka Serikali kuu chini ya mradi wa kuboresha vituo vya afya ikiwa ni kwa ajili ya ukarabati na ujenzi wa majengo wa Kituo cha Afya cha Kayanga kwa ufadhili wa Serikali ya Canada”, alisisitiza ndugu Adeodata.

Aidha taatifa hiyo iliendelea kusisitiza kwamba tayari kuna vifaa vya ujenzi vilivyopokelewa kutoka ghala la maafa mkoa ni pamoja na mabati ya kuezekea 280, matofali ya block 8,600, wire Pv 2.5 mita 400 na wire pv 1.5 mita 500.

Kutokana na michango hiyo tayari tayari ujenzi wa mradi wa wodi ya wazazi, chumba cha kuhifadhia maiti na power house ambapo ujenzi wake umekamilika kwa zaidi ya asilimia 92.3

Aidha ujenzi wa majengo mengine ambayo ni wodi ya akina mama, nyumba ya mtumishi, jengo la huduma za wagonjwa za afya ya uzazi na mtoto pamoja nahuduma za wagonjwa wa nje (OPD na RCH) na jengo la wodi ya wanawake umekamilika kwa asilimia 89.02.

“Itakumbukwa kwamba hapo awali kituo kilipokea Tshs. 743,704,057.20 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi hiyo, ambapo fedha zilizokwisha kutumika ni Tsh.591,688,477.00 na zilizobaki ni Tsh. 152,015,580.20 ambazo zinaendelea kutumika ili kukamilisha ujenzi na ukarabati wa majengo yanayokusudiwa ambayo ni wodi ya wagonjwa, jengo la upasuaji, jengo la utawala, store ya dawa na jengo la CTC ambapo ujenzi wake unatajiwa kuanza mwezi huu”, ilisisitiza taarifa hiyo

Kituo hiki cha Afya Kayanga ni kituo pekee cha Afya kilichopo ndani ya Wilaya Karagwe ambacho kilianza kutoa huduma mwaka 1961 ambapo kilipoanza muda huo ilikuwa kama sehemu tu ya kutolea huduma ya kwanza (Health post) ambapo baadae kulipandishwa hadhi na kuwa kituo cha Afya.

Mambo yalipamba moto zaidi katika zahanati ya Kafunjo ambapo umati wa wananchi ulifurika katika kumsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Kagera ambapo Mkuu wa Mkoa aliwapongeza sana wananchi wa maeneo hayo kwa kuchangia  kiasi cha Tsh.5,735,000.00 katika ujenzi wa zzahanati hiyo.

Katika hatua nyingine Mkuu wa Mkoa alitumia fursa hiyo kwenye maeneo yote aliyoyatembea kuwahimiza wanachi kushiriki katika kilimo cha kahawa na ulimaji wa bustani za matunda na zaidi zaidi alihamasisha juu ya ulaji wa chakula bora ili kuepukana na tatizo la utapiamlo linalotajwa kuundama mkoa wa Kagera.

Matangazo

  • MATOKEO DARASA LA SABA 2022 December 01, 2022
  • WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA SEKONDARI 2023 December 14, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI July 09, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI February 21, 2022
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • ZAWADI

    September 26, 2022
  • WAJERUMANI WASAINI KITABU KWA DED

    September 26, 2022
  • KARAGWE YAPOKEA WAJERUMANI

    September 25, 2022
  • KAMATI YA FEDHA MAFUNZONI

    September 16, 2022
  • Angalia zote

Video

BARAZA LA MADIWANI LAWASIMAMISHA WATUMISHI
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • History
  • Dira na Dhamira
  • Fomu za mbalimbali
  • NEEMA INAKUJA KWA WAKULIMA
  • FEDHA ZILIZOPOKELEWA KWA AJILI YA MFUKO WA JIMBO

Viunganishi vihusishi

  • NECTA
  • UTUMISHI
  • TOVUTI YA TAIFA
  • TAMISEMI
  • FFARS
  • SALARY SLIP

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    KARAGWE KAGERA TANZANIA

    Anuani ya posta: BOX 20 KARAGWE

    Simu: 028-2227148

    Simu ya mkononi: 0754653409

    Barua pepe: ded@karagwedc.go.tz ded.karagwedc@kagera.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright©2017 karagwedc. All rights reserved.