• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
KARAGWE DISTRICT COUNCIL
KARAGWE DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KARAGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na dira
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
        • Sekondari
        • Msingi
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Mazingira na Taka ngumu
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Ufugaji na Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Inayokuja
    • Iliyotekelezwa
    • Inayoendelea
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Taarifa
    • Sheria
    • Mpango mkakati
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha

Mkurugenzi Mtendaji awasihi watendaji, watumishi kutokuwa miungu watu

Imewekwa: June 22nd, 2017

Mkurugenzi Mtendaji awasihi watendaji, watumishi kutokuwa miungu watu

Na. Innocent E. Mwalo, KARAGWE 

   Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Karagwe, Godwin Kitonka amewataka watumishi na watendaji wa Halmashauri hiyo kuacha kuwanyanyasa wananchi wanaohitaji kupata huduma kutoka kwao badala yake watumishi na watendaji hao wamepaswa kuwahumia wananchi hao kwa kufuata miongozo na taratibu nyingine za kiutumishi huku akiwasihi kujenga tabia ya kuwa wasikivu.

   Kitonka aliyasema hayo mapema tarehe 20/06/2017 alipozindua mafunzo kwa baadhi ya watendaji na watumishi waliohudhuria mafunzo haya yanayotarajiwa kudumu kwa siku mbili katika Shule ya Msingi Kambarage, tarafa ya Bugene kurudia maneno hayo tarehe 21/06/2017 kwenye tarafa ya Nyaishozi kadhalika amefanya hivyo tarehe 22/06/2017 kwenye tarafa ya Kituntu ambapo mafunzo hayo yanaendelea .

   Mafunzo haya yaliyoandaliwa mahususi kwa ajili ya  kuwajengea watendaji na watumishi uwezo wa kiuongozi katika Halmashauri hii ni moja ya mikakati ya Halmashauri ya wilaya Karagwe ya kuhakikisha viongozi hawa wanapata uelewa wa mambo kadhaa kwa ajili ya kuwahudumia wananchi.

  Kitonka alisema mafunzo haya ni muafaka kwa ajili kuwaongezea viongozi hao uwezo wa kufanya kazi ikiwa ni pamoja kuwajengea uelewa wa pamoja lengo likiwa ni kuwahudumia wananchi wanyonge.

   Mapema  katika Tarafa za Bugene na  Kituntu, akimkaribisha Mkurugenzi Mtendaji kufungua mafunzo haya Afisa Utumishi wa Wilaya, Jackson Mwakisu aliyaelezea mafunzo haya kuwa yatafanyika katika tarafa zote za wilaya hii ili kuwawezesha watendaji wa serikali  kata na vijiji kupata maarifa kwa ajili ya kuwahudumia wananchi.

  Kitonka amekuwa anatumia fursa  ya mafunzo hayo kuwaonya baadhi ya watendaji ambao sio waadilifu kuacha tabia hizo na kufanya kazi kwa uadilifu ili wananchi wanufaike na rasilimali za nchi.

  Huku akimiminia sifa kemkem Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dk. John Pombe Magufuli, Kitonka alisema watendaji hawa wanapaswa kusoma alama za nyakati kwani serikali ya awamu ya tano inataka watumishi wanaendana na kasi yake katika kuwahudumiwa wananchi wanyonge.

   “Rais wetu anafanya mambo makubwa na kwa hiyo basi ni wajibu wetu kama viongozi ambao ndio tunawaohudumia wananchi hao wanyonge katika ngazi za chini tujitahidi sana kuhakikisha tunaendana na kasi hiyo kwa kuwahudumia  na kuhakikisha  wananchi hawa wananufaika na rasilimali za nchi hii kama ambavyo Mh. Rais anataka” amenukuliwa Kitonka kwenye mafunzo hayo

  “Mnapaswa kuwa viongozi na sio watawala katika kuwahudumia wananchi wanyonge” alisisitiza Kitonka

   Mafunzo haya yanayotolewa na wakufunzi ambao ni wataalam toka  Halmashauri ya wilaya waliopewa mafunzo hapo awali na wakufunzi kutoka chuo cha Utumishi wa Umma, Singida yanapaswa kuendelea kwenye tarafa nyingine za wilaya kama vile Kituntu tarehe 22/06/2017 na 23/06/2017 huku tarafa za Nyakakika na Nyakabanga zikitarajiwa kuwa na mafunzo haya tarehe 28/06/2017 na 29/06/2017.

   Mada zinazotarajiwa kutolewa kwenye mafunzo haya zitahusisha Uhamasishaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu, Usimamizi wa Fedha za Halmashauri na Umuhimu wa Kusoma Mapato na Matumizi.

   Nyingine ni Manunuzi ya Umma Katika Serikali za Mitaa, Uendeshaji wa Mikutano ya Halmashauri na Ngazi za Chini (Kata na vijiji/mitaa), Uongozi na Utawala Bora na Uandikaji na Usimamizi wa Miradi kwa Kushirikiana na Jamii.

Matangazo

  • MATOKEO DARASA LA SABA 2022 December 01, 2022
  • WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA SEKONDARI 2023 December 14, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI July 09, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI February 21, 2022
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • ZAWADI

    September 26, 2022
  • WAJERUMANI WASAINI KITABU KWA DED

    September 26, 2022
  • KARAGWE YAPOKEA WAJERUMANI

    September 25, 2022
  • KAMATI YA FEDHA MAFUNZONI

    September 16, 2022
  • Angalia zote

Video

BARAZA LA MADIWANI LAWASIMAMISHA WATUMISHI
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • History
  • Dira na Dhamira
  • Fomu za mbalimbali
  • NEEMA INAKUJA KWA WAKULIMA
  • FEDHA ZILIZOPOKELEWA KWA AJILI YA MFUKO WA JIMBO

Viunganishi vihusishi

  • NECTA
  • UTUMISHI
  • TOVUTI YA TAIFA
  • TAMISEMI
  • FFARS
  • SALARY SLIP

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    KARAGWE KAGERA TANZANIA

    Anuani ya posta: BOX 20 KARAGWE

    Simu: 028-2227148

    Simu ya mkononi: 0754653409

    Barua pepe: ded@karagwedc.go.tz ded.karagwedc@kagera.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright©2017 karagwedc. All rights reserved.