• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
KARAGWE DISTRICT COUNCIL
KARAGWE DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KARAGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na dira
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
        • Sekondari
        • Msingi
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Mazingira na Taka ngumu
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Ufugaji na Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Inayokuja
    • Iliyotekelezwa
    • Inayoendelea
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Taarifa
    • Sheria
    • Mpango mkakati
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha

MAADHIMISHO YA UPANDAJI WA MITI 'YAFUNIKA' WILAYANI KARAGWE

Imewekwa: March 28th, 2018

Maadhimisho ya upandaji miti ‘yafunika’ Wilayani Karagwe.

Na Innocent E. Mwalo, KARAGWE.

Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mhe. Meja Jenerali (Mst.) Salum Mustafa Kijuu ameagiza Halmashauri zote katika mkoa wa huu kutekeleza kwa vitendo agizo lake la upandaji wa miti kwa kupanda miti milioni moja na laki tano (1,500,000) au zaidi kila mwaka.

Haya yamesemwa hivi karibuni na Mh. Godfrey Mheluka ambaye ni Mkuu wa Wilaya Karagwe na ambaye kwenye maadhimisho hayo alimwakilisha Mkuu  huyo wa Mkoa wa Kagera.

Maadhimisho haya ambayo kitaifa yatafanyika Aprili 05, 2018 wilayani Kishapu mkoani Shinyanga, katika mkoa wa Kagera yamefanyika katika Wilaya ya Karagwe huku yakipambwa na kauli mbiu isemayo “Tanzania ya Kijani Inawezekana Panda Mti kwa Maendeleo ya Viwanda”.

“Mkoa wa Kagera unakabiliwa na tatizo la utapiamlo,udumavu na upunguvu wa vitamini hususani kwa watoto walio chini ya umri wa miaka mitano, miongoni mwa sababu ni kutozingatia matumizi ya lishe bora na ulaji wa matunda. Kwa sasa Mkoa wa Kagera  unaendeleza kampeni ya upandaji miti ya matunda kampeni iliyozinduliwa tarehe 26/1/2018 kwa lengo la kuhamasiha na utoaji wa elimu ya umuhimu wa lishe bora na ulaji wa matunda”, alisisitiza Mkuu wa Mkoa kupitia hotuba yake.

Aidha kwa mujibu wa Mkuu wa Mkoa huyo  kila Halmashauri za Wilaya , taasisi za Serikali na Binafsi Mkoani Kagera zimeagizwa kuhakikisha zinapanda miti ya matunda mbalimbali kuzunguka maeneo yao.

“Pia Halmashauri za Wilaya Mkoani Kagera zihakikishe kila Kaya inapanda angalau miti ya matunda kuanzia mitano kuzunguka maeneo yao ya makazi na  ikumbukwe pia kama hatua ya kuanzia katika mwaka wa fedha unaoendelea tulikubaliana kuanza kupanda miti ya matunda katika taasisi za afya”, aliendelea kusisitiza Mkuu wa Mkoa. 

 Katika hatua nyingine Mkuu wa Mkoa ameziagiza mamlaka za Serikali za vijiji , watendaji na Maofisa  wote wa Serikali wakiwemo Maafisa wa kada ya misitu kuchukueni hatua kwa Mujibu wa sheria ya Misitu Na.14 ya 2002 pamoja na sheria ya mazingira ya Namba 20 ya Mwaka 2004 kwa wale watakaobainika kuchoma moto ovyo.

Nao uongozi wa Halmashauri ya Wilaya Karagwe kupitia risala iliyowasilishwa na Processius Rweyendera kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmshauri ya Wilaya Karagwe umebainisha kwamba kwa mwaja jana Halmashauri ya Wilaya Karagwe ilifanya upandaji wa miti 1,862,720 kutoka kiasi ilichojiwekea kupanda ambayo ni miti 1, 500,000 ikiwa ni ongezeko la takribani asilimia 24 ya lengo lililowekwa.

Aidha uongozi wa Halmashauri ya Wilaya kipekee ulizipongeza Taasisi za kidini zinazofanya kazi  kubwa ya kushiriki katika kupanda miti ambapo taasisi kama CHEMA, ELCT, MAVUNO, KARUPOA zikiwa ni baadhi  zimetajwa kuwa na mchango mkubwa katika kufanikisha jitihada hizi za upandaji wa miti.

Katika shamrashamra hizi jumla ya miti 600 ya matunda imependwa katika maeneo mbalimbali hapa wilayani na kazi hii inatarajiwa kuendelea katika siku zijazo.

Kwa namna ya pekee Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya Karagwe, Mh. Wallace Mashanda ametoa wito kwa Menejimenti kuhakikisha kwamba mkakati unawekwa katika uundwaji wa klabu za Mazingira ili ziwe chachu katika kuhimiza jitihada hizi za upandaji wa miti.

 

Matangazo

  • MATOKEO DARASA LA SABA 2022 December 01, 2022
  • WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA SEKONDARI 2023 December 14, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI July 09, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI February 21, 2022
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • ZAWADI

    September 26, 2022
  • WAJERUMANI WASAINI KITABU KWA DED

    September 26, 2022
  • KARAGWE YAPOKEA WAJERUMANI

    September 25, 2022
  • KAMATI YA FEDHA MAFUNZONI

    September 16, 2022
  • Angalia zote

Video

BARAZA LA MADIWANI LAWASIMAMISHA WATUMISHI
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • History
  • Dira na Dhamira
  • Fomu za mbalimbali
  • NEEMA INAKUJA KWA WAKULIMA
  • FEDHA ZILIZOPOKELEWA KWA AJILI YA MFUKO WA JIMBO

Viunganishi vihusishi

  • NECTA
  • UTUMISHI
  • TOVUTI YA TAIFA
  • TAMISEMI
  • FFARS
  • SALARY SLIP

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    KARAGWE KAGERA TANZANIA

    Anuani ya posta: BOX 20 KARAGWE

    Simu: 028-2227148

    Simu ya mkononi: 0754653409

    Barua pepe: ded@karagwedc.go.tz ded.karagwedc@kagera.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright©2017 karagwedc. All rights reserved.