• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
KARAGWE DISTRICT COUNCIL
KARAGWE DISTRICT COUNCIL

United Republic of Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KARAGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na dira
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
        • Sekondari
        • Msingi
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Mazingira na Taka ngumu
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Ufugaji na Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Inayokuja
    • Iliyotekelezwa
    • Inayoendelea
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Taarifa
    • Sheria
    • Mpango mkakati
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha

KIJIJI CHA KAGUTU CHATUMIKA KAMA DARASA SIKU YA ‘AFYA NA LISHE YA KIJIJINI’.

Imewekwa: February 19th, 2021

Na Innocent E. Mwalo.

Baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Lishe na wataalam wa Afya wilayani hapa, mnamo tarehe 19/02/2021 wameshiriki ‘Siku ya Afya na Lishe Kijijini’ iliyofanyika katika Kijiji cha Kagutu katika Kata ya Ndama na kufanya mafunzo kwa wananchi wa kijiji hicho juu ya namna bora ya kuandaa chakula cha watoto wa chini ya miaka mitano.

Mafunzo haya ambayo hufanyika kwa kila robo mwaka kwa vjiji vyote wilayani Karagwe yakiwa na lengo la kupambana na utapiamlo unatokana na lishe duni, yalienda sambamba na utoaji wa Elimu ya lishe, namna ya kuandaa au kupika chakula na kupima uzito pamoja na utambuzi wa watoto wenye utapiamlo.

Kwa kupitia mafunzo hayo, Bi Lustica Mgumba, ambae ni Afisa Lishe wilayani hapa, aliyataja makundi matano ambayo ni mlo kamili wa chakula ambapo kundi la kwanza lilikuwa ni vyakula vya protini ambavyo husaidia kukarabati sehemu zilizochakaa, kuimarisha kinga ya mwili, kuzuia upungufu wa damu na kuuwezesha mwili kufanya kazi kwa ufanisi ambapo orodha ya vyakula hivi ilihusisha vyakula vya asili ya wanyama kama vile nyama, samaki, dagaa, maziwa, mayai, maini, figo, senene, kumbikumbi na wadudu wengine

‘’Kundi la pili ni vyakula vya wanga ambavyo hutokana na nafaka, mizizi na ndizi na vyakula hivi ndivyo vinavyochukua sehemu kubwa ya mlo wa kawaida na hivyo basi ndio vyakula vikuu na mfano wake ni mahindi, mchele, mtama, ulezi, ngano, uwele, viazi vitamu, viazi vitamu, muhogo, magimbi, viazi mviringo na ndizi ambapo vyakula vya kundi hili husaidia kuupa mwili nguvu ya kufanya kazi’’, alisisitiza Bi. Lustica.

Bi Lustica alendelea kutaja kundi la tatu, la nne na tano la vyakula hivyo ambapo katika kundi la tatu alitaja vyakula kama vitamini na madini vikijumuisha matunda ya aina zote yaaani yale yale yanayolimwa na yale ya porini  huku akitaja mananasi yanalimwa kwa wingi katika eneo la kijiji cha Kagutu kama mfano wa chakula cha kundi hilo na alisisitiza kuwa hili ni kundi la vyakula vinavyopupa mwili uwezo wa kuzuia na kupambana na maradhi ili kuwezesha mwili kufanya kazi kwa ufanisi.

Aidha kupitia mafunzo hayo, Bi Lustica alilitaja kundi la nne kuwa ni vyakula vinavyohusisha mboga mboga za aina zote yaani zile zinazolimwa na zile zisizolimwa ikiwa ni pamoja na mchicha, majani ya maboga, kisamvu, bamia, mnafu, mchunga na ambazo husaidia  mwili kupambana na maradhi

Kundi la tano na la mwisho lilihusisha vyakula vya mafuta lakini yakihitajika kwa kiasi kidogo mwilini ambayo hupatikana kutokana na mbegu za mime kama vile alizeti, pamba, korosho, karanga na mawese ambapo alivielezea kama vyakula vya kuupa mwili nguvu kwa kiasi kikubwa.

Nao wananchi waliokuwa wakifuatilia mafunzo hayo kwa umakini mkubwa walionesha shauku kubwa ya kutaka kujua mambo kadhaa wa kadhaa kuhusua masuala ya lishe ambapo Bi. Jesca Phason mkazi wa Kagutu aliwauliza wawezesha wa mafunzo hayo juu ya muda wa kupika mboga za majani ambapo alidai kuwa kumekuwa na madai ya kwamba upikaji wa muda mrefu huharibu ubora wa chakula hicho ambapo Bi Lustica alimweleza kuwa kwa kawaida upikaji wa mboga z majani unapaswa usizidi dakika tano.

Kwa upande Bi. Beatrice Laurent, Afisa Afya wilayani hapa pamoja na mambo mengine aliihamasisha jamii ya Kagutu na wilaya ya Karagwe kwa ujumla juu ya umuhimu wa ujenzi na matumizi bora ya vyoo ambapo alitoa wito kwa wananchi hao kuwa licha ya umuhimu wa mlo kamili katika vyakula wanavyokula, kazi hiyo inawezaisiwe na tija kutokuwa kama hawatazingatia ujenzi na matumizi bora ya vyoo kwani bila kufanya hivyo kinyesi cha binadamu na mkojo vinaweza kuchafua vyakula hivyo na kueneza vidudu na minyoo ambayo husabisha matatizo makubwa kiafya.

Naye Claudia Nkuba ambaye ni Mratibu Msaidizi wa Huduma ya Afya ya Uzazi na Mtoto wilayani hapa aliwasihi akina mama wajawazito kuhakikisha kuwa wanajifungulia katika vituo vya tiba ili kujihakikishia usafi wa usalama wakati wa kujifungua.

Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO YA ASILIMI 10 October 04, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI KADA YA DEREVA II NA WAANDISHI WAENDESHA OFISI II September 30, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI WASAIDIZI KUMBUKUMBU DARAJA LA II NA MTENDAJI WA KIJIJI WA III October 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI February 21, 2022
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KAMATI YA LISHE YAKETI KUJADILI UTEKELEZAJI WA AFUA ZA LISHE, KIPINDI CHA ROBO YA TATU 2024/2025.

    April 22, 2025
  • KUELEKEA MSIMU WA KAHAWA 2025/2026: MAAFISA UGANI KARAGWE DC WAPEWA MAFUNZO ILI KUWASAIDIA WANANCHI KUONGEZA THAMANI YA ZAO HILO.

    April 11, 2025
  • WALENGWA WA TASAF KARAGWE DC WANUFAIKA NA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA KIFEDHA WALIZOANZISHA.

    March 17, 2025
  • DC LAIZER AWATAKA WANAWAKE WA KARAGWE KUJIIMARISHA KIUCHUMI.

    March 08, 2025
  • Angalia zote

Video

SHIRIKI UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 KARAGWE TUMEJIPANGA
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • History
  • Dira na Dhamira
  • Fomu za mbalimbali
  • NEEMA INAKUJA KWA WAKULIMA
  • FEDHA ZILIZOPOKELEWA KWA AJILI YA MFUKO WA JIMBO

Viunganishi vihusishi

  • NECTA
  • UTUMISHI
  • TOVUTI YA TAIFA
  • TAMISEMI
  • FFARS
  • SALARY SLIP

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    KARAGWE KAGERA TANZANIA

    Anuani ya posta: BOX 20 KARAGWE

    Simu: 028-2227148

    Simu ya mkononi: 028-2227148

    Barua pepe: ded@karagwedc.go.tz ded.karagwedc@kagera.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright©2017 karagwedc. All rights reserved.