• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
KARAGWE DISTRICT COUNCIL
KARAGWE DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KARAGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na dira
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu
        • Sekondari
        • Msingi
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Mazingira na Taka ngumu
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Ufugaji na Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Inayokuja
    • Iliyotekelezwa
    • Inayoendelea
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Taarifa
    • Sheria
    • Mpango mkakati
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha

Karagwe Yapendekezwa kujenga Kiwanda cha Nyama

Imewekwa: October 1st, 2017

   

Karagwe  yapendekeza kujenga Kiwanda cha Nyama 

Na, Geofrey A.Kazaula – Karagwe 

Kufuatia mapendekezo ya Mkoa wa Kagera ya kila Wilaya kuwa na kiwanda kimoja na bidhaa moja, Wilaya ya Karagwe imefikia makubaliano ya kujenga kiwanda cha nyama ili kuendana na Mapendekezo ya Mkoa pamoja na  kutekeleza Sera ya Serikali ya awamu ya tano ya kuwa na Uchumi wa viwanda.

Awali akifungua kikao cha wadau mbalimbali wa maendeleo pamoja na wataalam wa Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe , Mkuu wa Wilaya ya Karagwe Mh, Godfrey Mheluka amesisitiza kuwa wadau hao wahakikishe wanapendekeza kiwanda ambacho kitawanufaisha wananchi wote bila kujali hali zao za kiuchumi

Kwa upande wake , Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe  Bi, Ashura Kajuna ameeleza kuwa tayari Halmashauri imetenga eneo la viwanda lililopo katika Kata ya Kihanga.

Aidha, ame eleza kuwa eneo hilo lina sifa ya kuwa eneo la viwanda kwani tayari lina umeme, lina maji na lina barabara ya lami na hivyo lina fikika kwa urahisi.

Naye  Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe Mh, Wallace Mashanda ameeleza kuwa wafugaji kwa sasa wanapaswa kujiunga katika ushirika kama lilivyo agizo la serikali na kueleza kuwa Serikali itawawezesha wafugaji hao ikiwa watakuwa katika ushirika huku akifafanua  kuwa kigezo kimoja wapo cha kuunda ushirika ni kuhakikisha wahusika wote ni wale wenye mifugo tu.

Kikao hicho kilihusisha pia wananchi na wadau mbalimbali ambao nao walitoa mapendekezo juu ya sababu muhimu za kuwa na kiwanda cha nyama  badala ya zao lingine.

Baadhi ya sababu zilizotolewa na wadau juu ya kutakiwa kujenga kiwanda cha nyama ni pamoja na kwamba mazao mengine kama matunda, mahindi, ndizi, Arizeti, maharage na kahawa tayari yana viwanda vyake na kwamba  kiwanda cha nyama bado hakijajengwa.

Aidha wameeleza kuwa Wilaya ya Karagwe ina ng’ombe wengi watakao uzwa katika kiwanda hicho na kuwapatia wananchi kipato tofauti na hivi sasa ambapo bei ya ng’ombe ipo chini kutokana na umbali wa kuwafikisha sokoni .

Sababu nyingine zilizo pelekea kufikia makubaliano hayo ni kwamba mapendekezo ya Mkoa yaliyotolewa kwa kila Wilaya, hakuna Wilaya iliyopendekezwa kujenga kiwanda cha nyama na kwamba kwasababu Wilaya ya Karagwe inao uwezo wa kuingiza ng’ombe 1500-2000 sokoni kila mwezi  uwezo wa kuendesha kiwanda cha nyama ni mkubwa  ambapo ng’ombe wote wa ukanda huu wanaweza kupata soko .

Licha ya ng’ombe wadau hao wameeleza kuwa kuna mifugo mingine kama mbuzi ambayo pia inaweza kuchakatwa katika kiwanda hicho na kuwaingizia wananchi kipato

Ili kufikia lengo hilo la kujenga kwanda cha nyama, wadau hao wamependekeza kuwa elimu iendelee kutolewa kwa wafugaji ili kuhakikisha wanafuga kisasa kwa maana ya kuwa na mifugo kidogo yenye tija, kuwa hamasisha wakulima kulima mazao ya kutosha ikiwa ni pamoja na kulima chakula cha mifugo, kutafuta madume bora ya ng’ombe ili kupata ng’ombe wakubwa na wenye tija, kutenga maeneo ya wafugaji na wakulima, na kwamba wazo hilo la ujenzi wa kiwanda cha nyama liendane sambamba na ujenzi wa kiwanda cha ngozi.

Hata hivyo, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe Mh, Wallace Mashanda ametoa wito kwa wadau mbalimbali ambao tayari wanatengeneza bidhaa hasa zinazotokana na ndizi kuhakikisha bidhaa hizo zinawekewa mkakati endelevu ikiwa ni pamoja na kuhamasisha ulimaji wa mazao husika.

Aidha amesisitiza kuwa mazao hayo yaongezwe ubora kwa kushirikisha vyombo kama TBS  na TFDA ili kuyawezesha kupata soko na kuondoa hofu kwa walaji jambo ambalo amesema lifanyiwe kazi kwa wakati.

                                 

Matangazo

  • MATOKEO DARASA LA SABA 2022 December 01, 2022
  • WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA SEKONDARI 2023 December 14, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI WATENDAJI May 19, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI July 09, 2022
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • Ujenzi shule 'Kagera river' unaendelea vizuri.

    April 12, 2023
  • Ujenzi shule 'Kagera river' unaendelea vizuri.

    April 12, 2023
  • Hospitali ya wilaya ya Karagwe kuzalisha gesi

    April 12, 2023
  • Hospitali ya wilaya ya Karagwe kuzalisha gesi

    April 12, 2023
  • Angalia zote

Video

BARAZA LA MADIWANI LAWASIMAMISHA WATUMISHI
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • History
  • Dira na Dhamira
  • Fomu za mbalimbali
  • NEEMA INAKUJA KWA WAKULIMA
  • FEDHA ZILIZOPOKELEWA KWA AJILI YA MFUKO WA JIMBO

Viunganishi vihusishi

  • NECTA
  • UTUMISHI
  • TOVUTI YA TAIFA
  • TAMISEMI
  • FFARS
  • SALARY SLIP

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    KARAGWE KAGERA TANZANIA

    Anuani ya posta: BOX 20 KARAGWE

    Simu: 028-2227148

    Simu ya mkononi: 028-2227148

    Barua pepe: ded@karagwedc.go.tz ded.karagwedc@kagera.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright©2017 karagwedc. All rights reserved.